Warioba: Mimi na Salim urais basi

Warioba: Mimi na Salim urais basi

Hatuhitaji Tx kwani wao wanasema zanzibar ni nchi. Pili kweli Ccm wamekosa mtu hadi wssimamishe kibabu cha miaka80???? Bye bye Ccm kama mmefika hapo.
 
Katika masuala ya uadilifu anatakiwa ajibu hoja za kuchafuliwa katika kipindi cha kampeni za kugombea nafasi ya kuwakilisha CCM kiti cha Urais. Kukaa kimya bila kujibu mapigo yale ambayo yalitangazwa waziwazi hadharani ina maanisha alihusika. La sivyo kama anajiona hakuhusika kwa nini asiwachukulie hatua waliomchafua wakati tuhuma hizo zilikuwa nzito kuhusu mauaji?



Wanafalsafa husema kukaa kimya dhiti ya tuhuma zinazomkabili mtu ni kweli zinamhusu na hivyo dhamiri inamwuma, aidha tuhuma si za kweli lakini hajiamini katika kujenga utetezi.

Iwapo anashindwa kujenga utetezi katika masuala yanayomhusu binafsi atawezaje katika mambo mazito ya kitaifa?

palepale ukumbini chimwaga alikanusha madai dhidi yake. miongoni mwa hayo madai ni kwamba alishiriki katika mauaji ya karume. mwenyewe alisema kuwa alikua balozi wa tanzania misri. hajui lolote na hahusiki na mauaji hayo.

walizua kuwa siyo raia. kuhusu hilo alichekaa tu kuonesha alama ya mshangao kisha akasema kuwa siyo baba yake tu hadi babu zake wawili wamezikwa zanzibar. yeye pia alizaliwa na kukulia znz.

alizushiwa kuwa kuna ndugu yake mmoja ni mwanajeshi mwenye cheo oman. ana mpango wa kugombea urais ili oman iteke znz na kuirudisha katika himaya yake. kwa ujumla madi haya yote aliyaita ya kitoto na yasiyo na mashiko. alikiri kuwa na ndugu oman lkn akasema hilo ni jambo la kawaida kwa sababu kuna watu wana ndugu upande wa kenya, msumbiji, zambia, malawi na uganda.
 
MWANDISHI UMEFANIKIWA KUONYESHA TOPE ZAKO ZA KICHWANI,TOFAUTI NA WENZIO AMBAO TOPE ZAO HUWA ZA MCHANGA,WEWE UMEONYESHA TOPE ZA MFINYANZI-Shame. On you! KWANI KAKWAMBIA ANATAKA URAIS,AU UNATAFUTA BWANA TUKUTOLEE POSA.

Mkuu CHIGANGA,
Yaani katika maneno yooote tuliyonayo kwenye kamusi ya kiswahili wewe umechagua kutumia haya kufikisha ujumbe wako!!
 
Last edited by a moderator:
L.Col_Members_SalimSalim.jpg
images

Dr. Salim Ahamed Salim (Tanzania) and Henry A. Kissinger (USA)

Dr. Salim Ahmed Salim ana jina kubwa nchini na kimataifa katika masuala ya kimataifa. He is a diplomatic figure. Naweza kumlinganisha na baadhi ya wanadipolamasia kama Henry Kissinger pamoja na umaarufu wao kimataifa hawakufaa kushika dola katika taifa.

Majukumu mazito aliyowahi kuyafanya kitaifa na kimataifa ni pamoja na:
  • Mwenyekiti wa Baraza la Usalama Umoja wa Mataifa
  • Katibu Mkuu Umoja wa nchi Za Afrika
  • Mgombea Ukatibu Mkuu umoja wa Mataifa - hakupita
  • Nafsi ya juu aliyowahi kuishika Tanzania ni kuwa Waziri Mkuu
Pamoja na umaarufu alioweza kuwa nao katika masuala ya kimataifa na kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania:

  1. Hajaonyesha msimamo wake katika masuala ya kitaifa,
  2. Hayuko wazi
  3. Mkimya asiye weza kushirikisha aliyo nayo.
  4. Pamoja na kwamba ni mwana CCM sijawahi kuona ushirikishaji wa uongozi wake kwa CCM zaidi ya kuwa mhudhuriaji.
  5. Anaonekana kupokeleka zaidi kwa sura badala ya vitendo na fikra.
  6. Anaonekana kufaa shughuli za kiofisi zaidi kuliko siasa za majukwani.

Kwa mtazamo huu ana dira gani katika kuongoza Tanzania ya leo kama atagombea urais?
Je, Tanzania tuendelea kunadishwa majina makubwa ya wagombea urais pasipo kuonyesha uwezo wao?

Kambi ya "mtaka urais maarufu" EDWARD LOWASSA @ WORK

Mnaweweseka sana wadau wa kambi ya mzee mzima,aliyewaambia salim anataka urais nani?yeye kaingizwa kamati kuu kwa lengo maalum,mtakuja kulikua huko mbele,ni mapema sana kwa sasa.
 
Aaah Wapi,

Mmeshaanza siasa zenu za majitaka sasa,,

Hebu niambie wewe sasa.humpendi huyu kwa chuki zako binafsi au humpendi kwa kuwa yuko CCM??

Akisimama huyo 2015 hatuna budi kumpatia nchi hii,mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni..

Au kwa kuwa ni Muislam??


Hoja ya uislamu unaileta wewe!.. Mleta hoja hajasema kataeni waislamu!... Mimi hata 2005 nilitaka huyu ndiye apewe nafasi. Lakini uhuni wa wanamtandao haufai!
 
Kambi ya "mtaka urais maarufu" EDWARD LOWASSA @ WORK

Mnaweweseka sana wadau wa kambi ya mzee mzima,aliyewaambia salim anataka urais nani?yeye kaingizwa kamati kuu kwa lengo maalum,mtakuja kulikua huko mbele,ni mapema sana kwa sasa.


Wanalia na kusaga meno kwa kuliskia jina la SAS..
 
Hatuhitaji Tx kwani wao wanasema zanzibar ni nchi. Pili kweli Ccm wamekosa mtu hadi wssimamishe kibabu cha miaka80???? Bye bye Ccm kama mmefika hapo.

vipi kuhusu slaa,huon nayeye kwa kumfananisha na Salim Ahmed salim kiafya hayuko poa??

nanona kama ule mkono wake haujakaa fresh,unahitajika kuangaliwa kwajicho pana zaid
 
viongozi wakuu wote serikalini walilaani kitendo hicho na nasikia hadi fbi wameletwa kwa uchunguzi wa kina. ulitaka na dkt salim nae aseme?

Ndiposa tungejua msimamo wake kwenye hilo sakata.
Wewe wajua msimamo wake?
 
Salim ni mwanasiasa mzuri ila kwa Tz ta sasa sio wakati wake.
 
Safi candid, na siyo Salim tu, pia tuwasikie Membe na Lowasa...sijausikia msimamo wa Membe ktk sakata la gesi ya Mtwara...na Lowasa anasemewa sana, kifupi wanasiasa hawa wanabebwa na makundi yao kuliko uwezo wao halisi...na jinsi hii ndivyo JK alivyopitishwa.
 
Salim is a toothless has been.

A lingering relic from a more innocent era.
 
Aisee bado watu wanamfikiria huyu mzee kuwa anataka kuwa Rais! aliukosa 2005.....S
 
Aaah Wapi,

Mmeshaanza siasa zenu za majitaka sasa,,

Hebu niambie wewe sasa.humpendi huyu kwa chuki zako binafsi au humpendi kwa kuwa yuko CCM??

Akisimama huyo 2015 hatuna budi kumpatia nchi hii,mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni..

Au kwa kuwa ni Muislam??

Kwa kuwa huyu ni Mzanzibari na wazanzibari wakiongozwa na kina Maalim SEIF na Aman Karume, wanaitaka Zanzibar yao iwe huru, itoke kwenye muungano, HUYU BWANA PAMOJA NA UWEZO, UADILIFU NA SIFA ALIZONAZO anakosa uhalali wa kuingoza nchi hii kwani HAITAKUWEPO!

Pili sitamuelewa hata kidogo kama chama chaka kitamtaka awe mgombea wake na yeye akakubali. HAWAMTAKI NDANI YA CCM! Rejea aliyofanyiwa na kuzushiwa kipindi kile alipojitosa kuwania nafasi hiyo!
Ni vema tukamuacha mzee wa watu akatulia na kupumzika.
 
Mbona Kikwete alipewa,au naye si mwislam? BTW, Jemedali Mwislam Kikwete alimfanyia Zengwe na Fitna Mwislam mwingine Dr Salim A Salim. Hivyo MBWA KALA MBWA. The rest ni chuki na upungufu wa hekima kichwani.
SAFI SANA! jibu mujarab.
Leo hii wameshasahau yote hayo.
 
Jaman kwani mtu kuwa kiongozi mpaka ajionyeshe kuchangia na kutolewa ktk magazeti na tv? Yu guy huwez kuwa serious coz napata wasiwasi waweza kupigia kura fisadi au kiongoz bomu kama mamvi kisa anajionyesha sana na kuchangia changia sana........read abt great writers who wrote abt and and politics they never say something like that unless yu one create and start ur own political philosophy
 
Kubwajinga,

..kwa uelewa wangu,wakati Mkapa alipoingia madarakani alikuwa msafi kuliko Salim Salim. now, look at what he did alipokuwa madarakani!! binafsi siwaamini hawa wanafunzi wa Nyerere. nadhani ni wasafi kwasababu ya kumuogopa Mwalimu.

..kuhusu uwezo wake wa kuongoza, pamoja na uelewa wake wa dunia vs mahitaji ya nchi, sidhani kama Salim Salim ana lolote jipya. binafsi rekodi yake ya OAU hainivutii kwasababu aliishia kuifanya kama kijiwe cha Muamar Gaddafi. wa-Liberia hawataki hata kumsikia huyu bwana. wakati wa mgogoro na mauaji ya DRC, OAU and Salim Salim were missing.

..mwisho, kwa hapa nyumbani Salim Salim ametumikia wizara ya mambo ya nje, pamoja na wizara ya ulinzi. sasa pamoja na umuhimu wa wizara hizo, I would rather consider mawaziri wenye uzoefu na waliofanya vizuri ktk wizara za sekta zinazogusa moja kwa moja maisha ya Mtanzania.

NB:

..Kibwajinga, kama tunataka Mtanzania na mwana CCM mwenye rekodi ya kimataifa, na aliyeipata kwa nguvu zake mwenyewe, on merit, basi ni Prof.Anna Tibaijuka[PhD].

Mkuu JokaKuu,

  1. Nakubaliana na wewe kabisaa kuhusu mama Tibaijuka. Huyu mama ana sifa nzuri sana kuliko wengi waliobebwa kufika waliko hivi sasa. Binafsi nam-rank very high.
  2. Lakini ukiangalia hawa watu wengine wanaotajwa-tajwa hivi sasa, sidhani kama wapo wanaomkaribia Salim kwa kuwa na sifa bora za kuliongoza taifa. Ulisahau pia kuwa alikuwa PM enzi za Mwalimu.
  3. Ni kweli kuwa Mkapa alikuja baadaye akawa fisadi, lakini bado hata na ufisadi wake alifanya kazi nzuri kuliko huyu mvivu na mbabaishaji, Kikwete, tuliye naye hivi sasa.
  4. Nafikiri sio vema kubuni tu kuwa labda Salim naye atakuwa fisadi kama Mkapa. Mkapa alitugeuka zaidi kutokana na ushawishi wa mke wake, kama tunavyoelewa hivi sasa. Lakini tusisahau kuwa Salim sio tu kuwa ni msafi, bali pia yuko katika board ya Mo Foundation inayochunguza ubora wa viongozi Afrika na sidhani kama akipewa madaraka atapenda kuwekwa kwenye kundi la akina Mkapa. Tumpime kila mtu kwa matendo yake bila kumuunganisha na watu mengine.
  5. Salim A. Salim ni mtu very unique Tanzania na nje ya TZ, na ni kitu cha kushangaza sana kuwa tulimchagua huyu mbabaishaji badala yake. Sina haja ya kuandika uzoefu wake hapa, bali unaweza kuangalia wewe mwenyewe kwenye Wiki- Salim Ahmed Salim - Wikipedia, the free encyclopedia.
  6. Ni muhimu sana kwa awamu ijayo tukachagua mtu ambaye ni msomi hasa wa kwenye vyuo vya kueleweka, mtu mwenye upeo wa kimataifa na mtu ambaye utendaji wake umethibitishwa na wengi kuwa effective.
  7. Tuachane na mtu yeyote aliye ndani ya mtandao au mpiga kelele asiye na historia yoyote ya utendaji bora ili tusijeibuka tena na Kikwete Part 2.
 
Mkuu nani sasa anafaa kuwa rais kwa mtazamo wako.
Kiongozi yeyote shupavu asiyetoka ccm. Mtu kama Salim akitaka kuwa kiongozi mzuri hawezi. Ni mtu asiyeguswa kabisa na uongozi mbovu na uliokuwepo na matatizo ya wananchi hivyo hatofanya kitu tofauti. Bora hata Joseph Sinde Waryoba ambaye wanaendana na Salim japo yuko ccm lakini anakerwa na upuuzi wakati mwingine anaupigia kelele. Wote hawafai.
Salim kuwa rais ni sawasawa na rubani mzee ambaye siku nyingi hajaendesha ndege siku nyingi kupewa ndege lakini iliyoharibika matairi, imetoboka kioo cha mbele na vifaa vyake ni vibovu kabisa. Ndege ikiwa ccm. Hata angekuwa rubani kijana kabisa mwenye uwezo wote wa kuendesha ndege za hao abiria hawatafika salama.
 
Kiongozi yeyote shupavu asiyetoka ccm. Mtu kama Salim akitaka kuwa kiongozi mzuri hawezi. Ni mtu asiyeguswa kabisa na uongozi mbovu na uliokuwepo na matatizo ya wananchi hivyo hatofanya kitu tofauti. Bora hata Joseph Sinde Waryoba ambaye wanaendana na Salim japo yuko ccm lakini anakerwa na upuuzi wakati mwingine anaupigia kelele. Wote hawafai.
Salim kuwa rais ni sawasawa na rubani mzee ambaye siku nyingi hajaendesha ndege siku nyingi kupewa ndege lakini iliyoharibika matairi, imetoboka kioo cha mbele na vifaa vyake ni vibovu kabisa. Ndege ikiwa ccm. Hata angekuwa rubani kijana kabisa mwenye uwezo wote wa kuendesha ndege za hao abiria hawatafika salama.

Thesi
Wachache wenye maono kama yako, wengine neno uadilifu ndio sifa ya uongozi, mbona kuna waadifu wengi ambao hawawezi kuongoza?
Ulimwengu wa leo kiongozi unapimwa kwa njia nyingi na kwa vigezo vingi na kiongozi mtarajiwa anatakiwa awahakikishie na kuwaondolea mashaka ya wananchi juu ya uwezo wake, vinginevyo ni mfumo wa kifalme, kama wa kidemokrasia tunataka atuhakikishie uwezo wake na kutoondolea mashaka mashaka yetu juu ya uwezo wake.
 
Binafsi simkubali SAS si kwa sababu ulizotaja, bali namuona muungwana mno!! Hii nchi ipo kwenye decaying zone hivyo sizani kama inahitaji mtu muungwana na mtaratibu kama SAS.

Ama kwa sababu ulizotaja, niseme wazi kwamba wakati mwingine kutoonesha msimamo wakati una malengo mazuri kwa nchi basi ni jambo zuri sana. Ni bora watu wasipokuelewa elewa kuliko wakikuelewa!
Umenielewa?
Say unakerwa sana na mwenendo wa rushwa ndani ya chama na kutamani kwamba endapo ungepata nafasi kubwa kabisa basi ungeng'oa mizizi yote ya rushwa nchini! Kama mawazo yako ni haya au sawa na haya, basi ni 100% much better kutoonesha msimamo wa wewe ni mtu wa aina gani especially tunapozungumzia African Politics! Ukijifanya wewe unaichukia sana rushwa....basi hapana shaka yoyote kabisa kwamba utapendwa na wananchi lakini chama chako kitakutenga na katu hakitakupa nafasi ya kuongoza jahazi!! Hii maana yake ni nini? Ni kwamba, hutakuja pata nafasi ya kutekeleza ndoto zako za kutokomeza rushwa!

Ngoja nikupe mifano midogo miwili ambayo imepata kutokea duniani! Hapa nawazungumzia Fredrick De Clerk, kiongozi wa mwisho wa Afrika ya Kusini yenye ubaguzi na Mikhail Gorbachev, kiongozi wa mwisho wa USSR!

UKiangalia kwa makini, unaweza gundua kwamba viongozi hao hawakupenda mifumo ambayo ilikuwamo kwenye nchi zao; kwa maana U-Communist in USSR na Apartheid System in South Africa! So, hao watu kama wangeonesha misimamo yao mapema, si ajabu wasingepata nafasi ya kuongoza hata kata! Walibaki kimya na misimamo yao na kuyadondosha yale ambayo hawakuyapenda pale walipopata nafasi.
 
Back
Top Bottom