Warioba: Mimi na Salim urais basi

Warioba: Mimi na Salim urais basi

Jamani mwaka 2015 si ni zamu ya wakristu kushika inchi sasa haya ya Salim yanatoka wapi tena? Kumwingiza kwa CC naona ni namna ya JK kujikosha na matusi aliyompa last time na kampeni zake za maji taka
 
Hata mimi nashindwa ku-connect mkuu, sikutegemea kama kuna Watanzania wano litakia mema Taifa letu anaweza kuanza ku-question sifa za ndugu Salim, jamaa huyu si nusura awe katibu mkuu wa umoja wa mataifa lakini akaondolewa na kura ya trufu ya Merikani? Kila mtu unajua kilicho mponza - misimamo yetu ya wakati huo, mpaka ikabidi Barozi wa Merikani katika Umoja wa Wataifa bibi KirkPatrick kumuomba msamaha ndugu Salim kwa kumwambia kwamba yeye hana chuki na Salim as a person, alipiga kura ya trufu kumpinga kutokana na mahagizo ya Serikali yake - mama huyo kamweleza wazi wazi ndugu Salim kwamba kilicho mponza ni misimamo ya Serikali ya Tanzania ya wakati huo!!

Lakini unaweza kukuta baadhi ya Watanzania awamtaki ndugu Salim kutokana na point yako ya mwisho, sio wengi lakini WAPO! Wako radhi wamtose mtu ambaye anajulikana kimataifa, kuheshimika na ambaye ana uwezo mkubwa wa kutukwamua kimaendeleo simply because creed yake ni ya KI-UKARA!
images

Henry A. Kissinger (USA)

Nimeleta mfano wa huyo kwenye picha Henry A. Kissinger ambaye alikuwa waziri wa mambo ya nje ya Marekani, tangu miaka ya 1960 Marekani haijapata jabali kama Kissinger ambaye alitikisa ulimwengu na walimwengu waliona kwa nini asiwe Rais wa Marekani. Ukweli nafasi yake kama mwanadiplomasia kimataifa aling'aa sana, lakini kwa nafasi ya urais hakufua dafu, nini tatizo ni kama Salim hakuonyesha sera na mlengo gani anao kwa wamarekani. Wakampiga chini. Uwazi na kuinyesha msimamo ni mambo muhimu katika uwanja wa siasa kugombea kuongoza nchi. Uadilifu na uzoefu wa kimataifa tu haisaidii.

Kikwete amekuwa waziri wa nchi za nje kwa miaka kumi, alizoea kuzurura, tabia hiyo ndiyo anayoiendekeza hadi sasa. Tukimchagua Salim maana yake atajishughulisha zaidi na mambo ya kimataifa badala ya dhamani aliyokabidhiwa kwa taifa lake. Lets be careful.

 
Jamani mwaka 2015 si ni zamu ya wakristu kushika inchi sasa haya ya Salim yanatoka wapi tena? Kumwingiza kwa CC naona ni namna ya JK kujikosha na matusi aliyompa last time na kampeni zake za maji taka

Katiba ya nchi inataka mtanzania ye yote anayefaa na kukidhi kiwango cha kikatiba anaweza kugombea urais, hakuna kifungu kinachotanabaisha kupokeza vijiti vya kuingia magogoni kwa msingi uliousema.
 
Candid scope,

Kwanza ungedeclare interest kwanza wewe unamtaka nani apitishwe na CCM, maana yupo unayemfagilia na inakua reflected na michango yako ya siku za nyuma sana. Huko Chadema ni kama vile ikitokea CCM wakimtosa candidate wako basi nawe kura yako Chadema.

Suala la Salim, yeye mwenyewe hajawahi kutamka kutaka urais 2015, lakini inaonekana kuingia kwake CC ya CCM imeleta kiwewe kwenye kambi flani flani za urais ndani ya CCM.

Ungedeclare interest ya unayemuunga mkono, ingesave a lot of energy za watu hapa.
 
Candid scope,

Kwanza ungedeclare interest kwanza wewe unamtaka nani apitishwe na CCM, maana yupo unayemfagilia na inakua reflected na michango yako ya siku za nyuma sana. Huko Chadema ni kama vile ikitokea CCM wakimtosa candidate wako basi nawe kura yako Chadema.

Suala la Salim, yeye mwenyewe hajawahi kutamka kutaka urais 2015, lakini inaonekana kuingia kwake CC ya CCM imeleta kiwewe kwenye kambi flani flani za urais ndani ya CCM.

Ungedeclare interest ya unayemuunga mkono, ingesave a lot of energy za watu hapa.

Jambo lisilozoeleaka Tanzania watu kutoa maoni nani anafaa na nani hafai katika nafasi ya urais katika vyombo vya habari na majadiliano ya kijamii mitandaoni. Wazoefu katika demokrasia maoni ya wananchi ndiyo yanayochukuliwa kama kishawishi cha mtu kufanya uamuzi wa kugombea nafasi fulani hasa uongozi wa juu nchini. Maoni ya wananchi yanapompa nafasi zaidi anakuwa na mategemeo ya kupata wafuasi wenye kumkingia kifua na hivyo kuushawishi umma umchague.

Mada yangu haina maana kwamba watanzania wote wana maono yangu, bali kwa mada hii inaweza kusaidia kuyaanika hata mazuri ya mtajwa na hivyo tukafikia hitimisho la kwamba anafaa au la. Kwa vile anasemwa na wengi kwamba CCM ikimsimamisha yeye watakuwa na candidate mzuri, basi wengine mtazamo wetu juu yake ndio kama nilivyouanisha hapo juu.
 
"Katiba ya nchi inataka mtanzania ye yote anayefaa na kukidhi kiwango cha kikatiba anaweza kugombea urais, hakuna kifungu kinachotanabaisha kupokeza vijiti vya kuingia magogoni kwa msingi uliousema"
Kupokezana vijiti imekuwa ndio utaratibu wetu toka uhuru na ninatarajia JK atautekeleza pia maana mkristo anapokuwa madarakani kiuchumi kunakuwa na ahueni yaani ni kama JENGA then BOMOA
 
"Katiba ya nchi inataka mtanzania ye yote anayefaa na kukidhi kiwango cha kikatiba anaweza kugombea urais, hakuna kifungu kinachotanabaisha kupokeza vijiti vya kuingia magogoni kwa msingi uliousema"
Kupokezana vijiti imekuwa ndio utaratibu wetu toka uhuru na ninatarajia JK atautekeleza pia maana mkristo anapokuwa madarakani kiuchumi kunakuwa na ahueni yaani ni kama JENGA then BOMOA

Waswahili bana, eti urais wa kupokezana, kwa utaratibu huu kila dhehemu litataka mtu wao apate nafasi, wazenj nao awe anafaa au la mtu wao ashike dola, kwa mwendo huu tutafika?
 
Hawa wazee waliokuwa wakiimba nyimbo ujamaa na kujitegemea za Nyerere na kuishia kucheza mchezo wa ubepari uchwara kwenye awamu zilzofuata siwaamini wote. Hawaeleweki eleweki.
 
kama unataka mtu anayepayuka kama kina makamba huyu sio wa aina hiyo, huyu ni mtndaji na kama unahudhuriaga midahalo mingi ya wanazuoni udsm utamwona na utajua misimamo yake na ndio mana hutamwona akipaza kelele kwenye siasa za ccm, anajua anachokifanya ni moja ya viongozi wazalendo tuliobaki nao katika taifa hili na ndo maana unamwona wamemweka hapo alipo coz wanajua umuhimu wake,
 
Mazoea yaliyopo kwa nchi hii, kunaweza kufanyika kila kiwezekanacho kumwubua hata ajuza ili mradi anaweza kuwa tegemeao la kuokoa jahazi lisizama, kwamba anafaa au la.
Najaribu kuangalia aiana ya watanzania tulionao sasa na tabia na hulka za huyu mzee ni vitu viwili tofauti. Sasa hivi tunahitaji mtu ambaye ni mkali unaweza kumwita dikteta lakini asiye mwizi wa fedha za umma. Tunahitaji kiongozi ambaye atafuta vijiwe vyote na kuhakikisha vijana wanafanya kazi badala ya kukaa vijiweni na kuzulula mijini eti wanatafuta deal au wanajiita mention town. Tunahitaji kiongozi ambaye anajua kabisa kuwa jukumu la kuteua na kufukuza ni la kwake na anafukuza mchana kweupe mara tu baada ya kupata ushahidi wa kutosha. Tunahitaji rais ambaye kama hajaridhishwa na ripoti basi anafana ziara a kushitukiza na matokeo yake ni kupandisha mtu cheo au kumfukuza. We need a no nonsense president
 
kama unataka mtu anayepayuka kama kina makamba huyu sio wa aina hiyo, huyu ni mtndaji na kama unahudhuriaga midahalo mingi ya wanazuoni udsm utamwona na utajua misimamo yake na ndio mana hutamwona akipaza kelele kwenye siasa za ccm, anajua anachokifanya ni moja ya viongozi wazalendo tuliobaki nao katika taifa hili na ndo maana unamwona wamemweka hapo alipo coz wanajua umuhimu wake,

Sir oby,
Kwanza nikupongeze kwa uwazi na kuweka kando ubinafsi, maana ungekuwa kama salim na kukaa kimya ningekuona u mbinafsi, usiyeshirikisha uliyo nayo kwa sisi wenzako. Lakini wewe ni tofauti na Salim ambaye si mshirikishaji wa aliyo nayo moyoni mwake. Kama hashirikishi sasa tutegemee akishika nchi ndio atabadilika? Hapana, sasa si wakati wa kudanganyana tena.

Ningependa kurudia nilichokijadili hapo nyuma kwamba siasa za leo si za kusubiria nikifanikiwa kushika ofisi ndio nitaweka mikakati, hapana. Leo watu wanataka ujibu maswali wanayotaka, wanataka uonyeshe msimamo wako. Kwa yale wanayolalamikia uonyeshe unakubaliana nayo au upo kinyume chake. Lakini kukaa kimya si mfumo wa zama hizi za utandawazi.
Tunaweza kujiuliza maswali ambayo hayana majibu juu ya Salim Ahmed Salim kama mada ilivyodondosha vidokezo.

  • Hakuna kumbukumbu hata vyombo vya habari kumnukuru kauli ye yote aliyowahi kutoa kwa wananchi kuhusu masuala mazito yanayowaumiza na kulalamikiwa na wananchi.
  • Sijapata kusikia mchango wake hata kwa CCM ulio wazi katika uongozi wake ndani ya nchi hii ingawa ni mhudhuriaji mzuri wa vikao kama kuna mwenye kujua hilo atuwekee nukuru hapa.
  • Sijapata kuona anaposhirikisha uzoefu, au kushirikisha aliyo nayo moyoni mwake kwa watanzani, kwa maneno mengine ni mbinafsi, vinginevyo asingekuwa mbinafsi angekuwa mshirikishi mzuri kwa serikali na chama cha CCM kutokana na uzoefu wake kimataifa.
  • Hata siku moja sijawahi kumwona yupo pamoja na walala hoi, maskini, wakulima, wafugaji nk. Yuko juu mno. Haonyeshi dalili za kuteremka, amebaki palepale juu. Anayemhitaji inabidi afanye jitihada za kumfikia kule mawinguni. Kwa kiongozi wa wananchi hali hiyo ni dalili ya kutokuwa karibu na wapiga kura wake. Pengine vyeo alivyoshika tangu ujana vimemfikisha alipo, hivyo kwa umri wake wa sasa vigumu maana mifupa imeshakomaa maana ilipokuwa bado laini hakufanya maamuzi ya kuwa flex-able.


  1. [*=2]Yule aliyekuwa naibu katibu mkuu umoja wa mataifa alionyesha kila dalili ya upendeleo kwa Tanzania kuliko nafasi nyingi za kimataifa alizoshika Salim alibaki na jina kubwa tu nchini.
    [*=2]Samweli Sitta pamoja na mapungufu yake yuko mwazi, bora ameonyesha hata mwelekeo mzuri wa bunge lililopita, kuna dalili ya kitu anachoweza kuvijunia.
    [*=2]Lowasa pamoja na kashfa zake, haoni aibu kuikosoa serikali na ajenda za Kikwete anapoona haridhiki nazo, pia kuna alipokuwa waziri kuna mambo hakuyakenulia meno bali kuwapiga bakora wahusika kama aliposhika wizara ya maji.
    [*=2]Rostam amediriki kutamka wazi hayuko tayari kuendana na siasa uchwara bora ajikite kwenye mambo yake ya biashara zake, pamoja na kashfa ambazo hazina vithibitisho vya kisheria lakini ukomavu wa kuamua kung'atuka ni sifa mojawapo katika uongozi uliotukuka.
Kuna mifano mingi ya watu ambao wamekuwa na kashfa lakini walifanya, wanafanya na kuonyesha dalili ya kufanya mazuri, lakini Salim hapa, kwa mtazamo wangu amevaa gwanda kubwa lililomzidi kimo, linampwaya mno
(over size), bora atulie na kula mafao yake sasa inatosha.
 
Najaribu kuangalia aiana ya watanzania tulionao sasa na tabia na hulka za huyu mzee ni vitu viwili tofauti. Sasa hivi tunahitaji mtu ambaye ni mkali unaweza kumwita dikteta lakini asiye mwizi wa fedha za umma. Tunahitaji kiongozi ambaye atafuta vijiwe vyote na kuhakikisha vijana wanafanya kazi badala ya kukaa vijiweni na kuzulula mijini eti wanatafuta deal au wanajiita mention town. Tunahitaji kiongozi ambaye anajua kabisa kuwa jukumu la kuteua na kufukuza ni la kwake na anafukuza mchana kweupe mara tu baada ya kupata ushahidi wa kutosha. Tunahitaji rais ambaye kama hajaridhishwa na ripoti basi anafana ziara a kushitukiza na matokeo yake ni kupandisha mtu cheo au kumfukuza. We need a no nonsense president

Mpitagwa,
Wewe umeona hili, wengine wanachoangalia bora tu kuwa na rais bila kuangalia mazingira na hali ya siasa na kiuchumi ilivyo sasa nchini. Mgombea urais anatakiwa aonyeshe yale ambayo wananchi wanaona ni tatizo kwa maisha na maendeleo ya nchi. Pamoja na kutokuwa na nafasi ya kutenda, lakini hata kauli tu inaweza kutoa picha ya kile anachokifikiria ndani ya moyo wake. Ndio maana siku hizi kuna debate kwa wagombea, licha ya debate, kuna vigezo ambavyo kabla ya uteuzi vinaangaliwa kama mtarajiwa anafaa kutokana na mwenendo wake wa maisha katika taifa letu. Mtazamo wake kwa watanzania, ubunifu wa mipango ya maendeleo na mfumo wa serikali.

Tunahitaji rais licha ya kuwa na panga la makali kuwili, aonyeshe ubunifu wa kuigeuza Tanzania kuwa taifa lenye kuwa na dira ya maendeleo kwa ulimwengu wa leo tokana na utajiri wa mali asili tulizo nazo. Ahadi za barabara zimekuwepo tangu tunapata uhuru, shule hali kadhalika, lakini sijaona hoja mbadala kwa marais waliomfuata Nyerere kujenga msingi wa uchumi wa kitaifa unaotegemea utajiri wa rasilimali za nchi yetu.

Tahadhari:
Vigumu kumgeuza aliyezoea kuruka angani aanze kutembea kwa miguu, kupanda baiskeli na kwenda vijijini kwa wananchi, kuamua kula mihogo Ikulu kwa kikombe cha tangawizi, kuzoea kula bilinganya zinazozalishwa na bustani za bonde la msimbazi badala ya vyakula vya mahoteli ya kitalii duniani.
Nadhani hoja yangu mwaipata. Somo tunalo, tumeliona. Je, tumejifunza nini na tumejenga tahadhari gani?
 
Salim ni janga na hana msimamo, alitumiwa na wamarekani kumwangusha Boutros Boutros Ghali. "What goes around, will come around" Thanx JK kwa kazi mzuri uliyoifanya kumchafua Salim. Hakuna maji ya kutosha kumsafisha 2015
 
Salim ni janga na hana msimamo, alitumiwa na wamarekani kumwangusha Boutros Boutros Ghali. "What goes around, will come around" Thanx JK kwa kazi mzuri uliyoifanya kumchafua Salim. Hakuna maji ya kutosha kumsafisha 2015

Hata siku moja sijawahi kumwona yupo pamoja na walala hoi, maskini, wakulima, wafugaji nk. Yuko juu mno. Haonyeshi dalili za kuteremka, amebaki palepale juu. Anayemhitaji inabidi afanye jitihada za kumfikia kule mawinguni. Kwa kiongozi wa wananchi hali hiyo ni dalili ya kutokuwa karibu na wapiga kura wake. Pengine vyeo alivyoshika tangu ujana vimemfikisha alipo, hivyo kwa umri wake wa sasa vigumu maana mifupa imeshakomaa maana ilipokuwa bado laini hakufanya maamuzi ya kuwa flex-able.
 
Najaribu kuangalia aiana ya watanzania tulionao sasa na tabia na hulka za huyu mzee ni vitu viwili tofauti. Sasa hivi tunahitaji mtu ambaye ni mkali unaweza kumwita dikteta lakini asiye mwizi wa fedha za umma.
Hata mimi base yangu imesimamia hapo na ndio maana hata ktk mada hii nilieleza wazi kwamba simkubali SAS si kutokana na hoja zilizotolewa na mto mada bali kutokana na hulka yake. Namuona kama ni muungwana mno; hakika hatuhitaji hata kidogo mtu wa aina hii! Nchi imeoza kila mahali....inahitaji kiongozi mkali na aliye dikteta kwa maslahi ya taifa!! Na ndio maana hadi leo naamini solutiona ya nchi hii ilikuwa ni kuwa na Approved Dictatorship Governance! Utawala Bora ni mzuri lakini kwa nchi iliyooza kama hii inasaidia tu kuwa kichaka muafaka cha wezi, mafisadi, na wale wasiotaka kuwajibika!
 
Thanx JK kwa kazi mzuri uliyoifanya kumchafua Salim. Hakuna maji ya kutosha kumsafisha 2015
Hata kama tunaaminishwa kwamba SAS alichafuliwa na JK, ukweli bado uko pale pale kwamba SAS aliathiriwa na siasa za ZNZ ambazo hadi leo kule kuna makovu ya ASP na HIZBU!! Wanaojiita Wana Mapinduzi katu hawapo tayari kuona mtu wa HIZBU anakuwa juu...!! Narudia, SAS alihujumiwa na Wazanzibari wenyewe!
 
Hata mimi base yangu imesimamia hapo na ndio maana hata ktk mada hii nilieleza wazi kwamba simkubali SAS si kutokana na hoja zilizotolewa na mto mada bali kutokana na hulka yake. Namuona kama ni muungwana mno; hakika hatuhitaji hata kidogo mtu wa aina hii! Nchi imeoza kila mahali....inahitaji kiongozi mkali na aliye dikteta kwa maslahi ya taifa!! Na ndio maana hadi leo naamini solutiona ya nchi hii ilikuwa ni kuwa na Approved Dictatorship Governance! Utawala Bora ni mzuri lakini kwa nchi iliyooza kama hii inasaidia tu kuwa kichaka muafaka cha wezi, mafisadi, na wale wasiotaka kuwajibika!

Sijawa mbali na maoni yako, lakini kuna kitu kingine nimekiona kwa Salim, sijui kama unaweza kuona tatizo ambalo mimi nimeliona kama ifuatavyo:

Hata siku moja sijawahi kumwona yupo pamoja na walala hoi, maskini, wakulima, wafugaji nk. Yuko juu mno. Haonyeshi dalili za kuteremka, amebaki palepale juu. Anayemhitaji inabidi afanye jitihada za kumfikia kule mawinguni. Kwa kiongozi wa wananchi hali hiyo ni dalili ya kutokuwa karibu na wapiga kura wake. Pengine vyeo alivyoshika tangu ujana vimemfikisha alipo, hivyo kwa umri wake wa sasa vigumu maana mifupa imeshakomaa maana alipokuwa bado laini hakufanya maamuzi ya kuwa flex-able.
 
Sijawa mbali na maoni yako, lakini kuna kitu kingine nimekiona kwa Salim, sijui kama unaweza kuona tatizo ambalo mimi nimeliona kama ifuatavyo:

Hata siku moja sijawahi kumwona yupo pamoja na walala hoi, maskini, wakulima, wafugaji nk. Yuko juu mno. Haonyeshi dalili za kuteremka, amebaki palepale juu. Anayemhitaji inabidi afanye jitihada za kumfikia kule mawinguni. Kwa kiongozi wa wananchi hali hiyo ni dalili ya kutokuwa karibu na wapiga kura wake. Pengine vyeo alivyoshika tangu ujana vimemfikisha alipo, hivyo kwa umri wake wa sasa vigumu maana mifupa imeshakomaa maana alipokuwa bado laini hakufanya maamuzi ya kuwa flex-able.

Kwa sasa, hilo naliona kabisa.....ni kweli, si tu kwamba inabidi mtu afanye jitihada kumfikia mawinguni bali ni kama hafikiki kabisa! Hata hivyo sina uhakika wakati anafanya domestic politics alikuwa ni mtu wa aina gani. Labda kwa wale ambao walikuwa na ufahamu wa kutosha enzi za uongozi wake nchini, huenda wakawa na la kusema katika hili!

Lakini vilevile inawezekana historia ya huyu bwana imechangia aonekane kuwa "si mtu wa watu!" Manake, according to Wikipedia personal profile ya SAS, ni kwamba alizaliwa 1942, and:
· Deputy Chief Representative of the Zanzibar Office based in Havana, Cuba 1961–1962
· Tanzania Ambassador to the Arab Republic of Egypt 1964–1965
· Tanzanian High Commissioner (i.e. Ambassador) to India 1965–1968
· Tanzania Ambassador to the People's Republic of China 1969–1970

So, at the age 19 jamaa tayari akawa completely excluded from the local community! Yaani, ameishi hivyo since his teenage! Hizi post za mapema mapema zilimkosesha kabisa nafasi ya ku-interact na local people! Na ikumbukwe kuwa hapo ilikuwa ni baada ya kuwa ameshakua shahada yake nchini India!! Sijui alikuwa ni mtu wa aina gani...at 19, ameshachukua shahada na kuwa ubalozini!
 
vita ya udhalimu ufisad yapaswa ipiganwe na watu wote. wengine wapambane hata wakiwa nje ya system. wasiachiwe wachache. au anaogopa akianza kupinga ushenz hadharan na xake mabovu yataibuliwa? hatutak watu waoga kupinga maovu. na wala hatutak watu wakaao kimya wakat kuna mambo meng ya ovyo yanaendelea
 
Back
Top Bottom