Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,897
- 6,933
Binafsi simkubali SAS si kwa sababu ulizotaja, bali namuona muungwana mno!! Hii nchi ipo kwenye decaying zone hivyo sizani kama inahitaji mtu muungwana na mtaratibu kama SAS.
Ama kwa sababu ulizotaja, niseme wazi kwamba wakati mwingine kutoonesha msimamo wakati una malengo mazuri kwa nchi basi ni jambo zuri sana. Ni bora watu wasipokuelewa elewa kuliko wakikuelewa!
Umenielewa?
Say unakerwa sana na mwenendo wa rushwa ndani ya chama na kutamani kwamba endapo ungepata nafasi kubwa kabisa basi ungeng'oa mizizi yote ya rushwa nchini! Kama mawazo yako ni haya au sawa na haya, basi ni 100% much better kutoonesha msimamo wa wewe ni mtu wa aina gani especially tunapozungumzia African Politics! Ukijifanya wewe unaichukia sana rushwa....basi hapana shaka yoyote kabisa kwamba utapendwa na wananchi lakini chama chako kitakutenga na katu hakitakupa nafasi ya kuongoza jahazi!! Hii maana yake ni nini? Ni kwamba, hutakuja pata nafasi ya kutekeleza ndoto zako za kutokomeza rushwa!
Ngoja nikupe mifano midogo miwili ambayo imepata kutokea duniani! Hapa nawazungumzia Fredrick De Clerk, kiongozi wa mwisho wa Afrika ya Kusini yenye ubaguzi na Mikhail Gorbachev, kiongozi wa mwisho wa USSR!
UKiangalia kwa makini, unaweza gundua kwamba viongozi hao hawakupenda mifumo ambayo ilikuwamo kwenye nchi zao; kwa maana U-Communist in USSR na Apartheid System in South Africa! So, hao watu kama wangeonesha misimamo yao mapema, si ajabu wasingepata nafasi ya kuongoza hata kata! Walibaki kimya na misimamo yao na kuyadondosha yale ambayo hawakuyapenda pale walipopata nafasi.
Unaweza ukawa sahihi kwa upande fulani, lakini ulimwengu wa leo wapiga kura wanapenda kuonyeshe msimamo katika yale ambayo wananchi wanaona utawala uliopo haujawaridhisha. Jambo la msingi kama unataka kusimama kupitia tiketi ya chama ambayo kinaongoza na kama kuna malalamiko mengi ambayo wananchi hawaridhishwi na kinachoendelea, bora kuonyesha msimamo wako.
Mifano uliyotolea kama ya SA au USSR wahusika hawakufanya kwa makusudi, kwa malengo yao walifikiria kwa kufanya hivyo wanaweza kuteka upande wa wanaoleta mgogoro waingie kwanye mfumo wao, kwamba wanakubaliana nao na hivyo kuendelea kujihakikisha kushika dola, kumbe hawakuona ufa uliopo ukatumika upande wa pili kufanikisha malengo ya muda mrefu.
Kwa vyo vyote ulimwengu wa leo hata Afrika uwazi kwa viongozi ni muhimu, watu wanataka msimamo wa mtu. Ukimya wake hauwezi kutupatia picha ya nini kilichomo moyoni mwake, tunajua yanayojilia, watanzania wa sasa ni sawa na aliyejeruhiwa na nyoka, hukimbia hata kamba tu ikigusa mguuni.