Warioba: Mimi na Salim urais basi

Tunatamani tuwe na rais mwenye kudhubutu bila kuuma uma maneno pale inapotokea maswala nyeti yanayotishia... kwani swala la kuchinjana na kuchoma nyumba za ibada wewe unaliona ni zuri... udini kwa sasa siyo jambo la kuficha....
Ndio maana nikawashangaa Njiwa na Doula walipoingiza udini badala ya sifa kama alivyosema mleta mada.
Hata sasa sijamsikia yoyote miongoni mwa wanotajwa kugombea via CCM
kuzungumzia kadhia ya udini, kwangu huo ni upungufu mkubwa kiuongozi.
 
tunachagua rais kutokana na dini yake lakini tunapokea mashehe na mapadri bila hata kuwapima imani zao. Mbona wabongo tuko upside down?
 
Ndio maana nikawashangaa Njiwa na Doula walipoingiza udini badala ya sifa kama alivyosema mleta mada. Hata sasa sijamsikia yoyote miongoni mwa wanotajwa kugombea via CCM kuzungumzia kadhia ya udini, kwangu huo ni upungufu mkubwa kiuongozi.
hili jambo la mauaji ya znz na kwengineko ni jambo pana sana! hujui nani katenda na kwa faida gani! kisiasa au kidini? naona mauwaji haya yamekaa kisiasa siyo kidini
 
Kwa jinsi siku zinavyopita, Kuna hatari ya nchi kupata Rais 2015 ambaye ni bogus zaidi ya Marais waliopata kuliongoza Taifa tokea tupate uhuru. Jamii kwa sasa imeanza kuona Rais bora ni yule mwenye imani ya dini kama wao bila kujali uwezo wake. Taifa limeanza kuonyesha dalili zote za kuelekea Taifa Mfu. Kwa Watanzania wengine wenye upofu wa fikra, Mwanasiasa mahili ni yule anayepiga kelele majukwaani bila hata ya kujua mipaka ya matamshi yake. Unfortunate, Salim Ahmed Salim hayupo kwenye haya makundi na siyo ajabu, kwa sasa ameanza kuzodolewa kwa sababu kwao, anaonekana hana vazi la Urais.

SAS ni mwanadiplomasia, na msingi mkuu wa kuwa mwanadiplomasia mahili ni kuwa CALM, COLLECTED AND ON BALANCE.

Ni kitu cha kushangaza pale watu wanamtaka aende sokoni kujiuza kama wanaSiasa wengine wanavyofanya kwa sasa. Salim Ahmed Salim hahitaji kwenda sokoni kujiuza kwa sababu kazi hiyo aliisha ifanya siyo kwa Tanzania tu bali hata katika mataifa. Pale alipopewa kazi ya kufanya katika nchi au mataifa, aliifanya kwa uadilifu na ufanisi mkubwa. What more you want!!.

Please Candid Scope , usichanganye bidhaa za kisiasa zinazojiuza kwa sasa na bidhaa iliyojipambanua tayari ndani ya soko la kisiasa.

Unanasiplomasia ni hatari kwa maana hawako na msimamo wa uwazi, na pengine wanaweza kuwa ndumila kuwili. Uwazi ni mambo ya msingi katika utendaji kisiasa. Utendaji kisiasa ni tofauti na kazi ya kiofisi tu, kwanis unapambana na mengi katika mazingira tofauti bila kuchagua uwanja wa kurusha mpira. Awapo kwenye siasa anatakiwa acheze nafasi zote, picher, catcher and striker, huo ndio ubora wa mtandaji mkuu katika kuongoza nchi.

Tunahitaji rais mwenye kuleta ufafanuzi na kupambanua mambo bila woga, bila haha na kwa uwazi. Anatakiwa aonyesha matatizo tuliyo nayo yamesababishwaje na njia mwafaka za kuyatatua.

Mambo mazito mazito yalimetokea, yanatokea na huenda yataendelea kutokea yanayotikisa nchi, haonyeshi kushtushwa wala kuonea uchungu, yeye amenyamaza tu.

Kizazi cha leo cha watanzania ni cha mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, anatakiwa kufugua mdomo tofauti na mfumo uliozoeleka wa chama kimoja kushika hatamu hahitaji kufungua mdomo.
 
Pilipili ipo shamba wewe inakuwasha looooooh pole sana. Mtu akisema kwa nini kasema, na akinyamaza napo kwa nini kanyamaza. Acha Hizo.
 
hili jambo la mauaji ya znz na kwengineko ni jambo pana sana! hujui nani katenda na kwa faida gani! kisiasa au kidini? naona mauwaji haya yamekaa kisiasa siyo kidini

Kauli ya kiuongozi ni muhimu sana, mauaji ni jinai- iwe kidini, kisiasa au kisasi. Kwa hali iliyopo na matukio ya kidini yaliyotukia kabla, tungetarajia Kiongozi/ Mwanasiasa makini atoe hata kauli ya kulaani tu.
 
Kauli ya kiuongozi ni muhimu sana, mauaji ni jinai- iwe kidini, kisiasa au kisasi. Kwa hali iliyopo na matukio ya kidini yaliyotukia kabla, tungetarajia Kiongozi/ Mwanasiasa makini atoe hata kauli ya kulaani tu.

viongozi wakuu wote serikalini walilaani kitendo hicho na nasikia hadi fbi wameletwa kwa uchunguzi wa kina. ulitaka na dkt salim nae aseme?
 
Unanasiplomasia ni hatari kwa maana hawako na msimamo wa uwazi, na pengine wanaweza kuwa ndumila kuwili. Uwazi ni mambo ya msingi katika utendaji kisiasa. Utendaji kisiasa ni tofauti na kazi ya kiofisi tu, kwanis unapambana na mengi katika mazingira tofauti bila kuchagua uwanja wa kurusha mpira. Awapo kwenye siasa anatakiwa acheze nafasi zote, picher, catcher and striker, huo ndio ubora wa mtandaji mkuu katika kuongoza nchi.

Tunahitaji rais mwenye kuleta ufafanuzi na kupambanua mambo bila woga, bila haha na kwa uwazi. Anatakiwa aonyesha matatizo tuliyo nayo yamesababishwaje na njia mwafaka za kuyatatua.

Mambo mazito mazito yalimetokea, yanatokea na huenda yataendelea kutokea yanayotikisa nchi, haonyeshi kushtushwa wala kuonea uchungu, yeye amenyamaza tu.

Kizazi cha leo cha watanzania ni cha mfumo wa demokrasia ya vyama vingi, anatakiwa kufugua mdomo tofauti na mfumo uliozoeleka wa chama kimoja kushika hatamu hahitaji kufungua mdomo.
Candid Scope Kwanza Hatumtendei haki Salim Ahmed Salim kumuongelea swala la Urais kwa sababu tunajitwika wajibu wake kitu ambacho ni kinyume hata kwenye macho ya haki. Kama atajitokeza na kusema atagombea basi hapo ndipo tunaweza kuanza kumzodoa.

Vilevile, unataka ajitokeze kwa sasa na kusema kama nani?. Kumbuka kwa sasa ana jukumu kubwa katika mchakato wa katiba huru halafu ni mjumbe wa kamati kuu ya CCM ambapo Mwenyekiti wake ni Rais wa nchi. Inahitajika hekima ya kiwango cha juu kisiasa ku manoeuvre katika majukumu hayo.

Siyo kelele zote zinazopigwa majukwaani zinajenga na kuleta ustawi nchini. Kelele zingine niza kibinafsi kisiasa. Kizuri chajiuza kibaya chajitembeza
 
kwani Rais huwa anahaguliwa kwa dini yake,kwani Waisilamu hawawezi kuongoza....inferirity,inferity....gona kill u guys

Aaah Wapi,

Mmeshaanza siasa zenu za majitaka sasa,,

Hebu niambie wewe sasa.humpendi huyu kwa chuki zako binafsi au humpendi kwa kuwa yuko CCM??

Akisimama huyo 2015 hatuna budi kumpatia nchi hii,mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni..

Au kwa kuwa ni Muislam??
 
Mbona Kikwete alipewa,au naye si mwislam? BTW, Jemedali Mwislam Kikwete alimfanyia Zengwe na Fitna Mwislam mwingine Dr Salim A Salim. Hivyo MBWA KALA MBWA. The rest ni chuki na upungufu wa hekima kichwani.

kwa nini amuwezi kujadili jambo bila kuweka udini?:A S cry:inasikitisha na ni udhaifu mkubwa,kwani dini yake yy ina nini chakufanya na urais wa nchi yetu
 
L.Col_Members_SalimSalim.jpg
images

Dr. Salim Ahamed Salim (Tanzania) and Henry A. Kissinger (USA)

Dr. Salim Ahmed Salim ana jina kubwa nchini na kimataifa katika masuala ya kimataifa. He is a diplomatic figure. Naweza kumlinganisha na baadhi ya wanadipolamasia kama Henry Kissinger pamoja na umaarufu wao kimataifa hawakufaa kushika dola katika taifa.

Majukumu mazito aliyowahi kuyafanya kitaifa na kimataifa ni pamoja na:
  • Mwenyekiti wa Baraza la Usalama Umoja wa Mataifa
  • Katibu Mkuu Umoja wa nchi Za Afrika
  • Mgombea Ukatibu Mkuu umoja wa Mataifa - hakupita
  • Nafsi ya juu aliyowahi kuishika Tanzania ni kuwa Waziri Mkuu
Pamoja na umaarufu alioweza kuwa nao katika masuala ya kimataifa na kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania:

  1. Hajaonyesha msimamo wake katika masuala ya kitaifa,
  2. Hayuko wazi
  3. Mkimya asiye weza kushirikisha aliyo nayo.
  4. Pamoja na kwamba ni mwana CCM sijawahi kuona ushirikishaji wa uongozi wake kwa CCM zaidi ya kuwa mhudhuriaji.
  5. Anaonekana kupokeleka zaidi kwa sura badala ya vitendo na fikra.
  6. Anaonekana kufaa shughuli za kiofisi zaidi kuliko siasa za majukwani.

Kwa mtazamo huu ana dira gani katika kuongoza Tanzania ya leo kama atagombea urais?
Je, Tanzania tuendelea kunadishwa majina makubwa ya wagombea urais pasipo kuonyesha uwezo wao?

Nikweli mie pia nafikiri ni mnafiki fulani hivi....
Ni mtu aliefanya kazi karibu kabisa na mwalimu lkn waislam wenzie wanapo mpaka mwalimu matope anakaa kimya kama vile anakubaliana nao....unlike Jenerali Ulimwengu mara nyingine anasema ukweli tu kuhusu mwalimu....

Then amepoa sana, amezoea vyeo vya kupewapewa, hajawahi kufight kupata cheo kama mwalimu, Dk Slaa Nk....
 
MWANDISHI UMEFANIKIWA KUONYESHA TOPE ZAKO ZA KICHWANI,TOFAUTI NA WENZIO AMBAO TOPE ZAO HUWA ZA MCHANGA,WEWE UMEONYESHA TOPE ZA MFINYANZI-Shame. On you! KWANI KAKWAMBIA ANATAKA URAIS,AU UNATAFUTA BWANA TUKUTOLEE POSA.
 
Candid Scope , kwa kweli kumlaumu Salim Ahmed Salim katika siasa za maji taka za siku hizi ni kumwonea tu.
Huyu ni mmoja wa viongozi waadilifu na watiifu mno nchi hii.

Tumeona jinsi alivyoumizwa katika kinyang'anyiro cha urais wa mwaka 2005.
Lakini alivyo mstaarabu hkujibu neno, na yuko kimya kabisa.
Hii ni pamoja na ukweli kuwa alishafikiaa ngazi ya juu kabisa katika uongozi wa Tanzania -Uwaziri Mkuu.

Sasa kumtaka zaidi naona n kumwonea tu, na wala hajatamka kuutaka urais, maana hata kwa kutazama tu waliomuumiza mwaka 2005 ni mitandao ile ile iliyopo.

Mkuu utiifi tu na uadilifu hautoshi! Anaweza kuthubutu kufanya maamuzi? haumiumi maneno linapokuja suala gumu la kitaifa? hajawahi kuonyesha msimamo huo sasa nchini, tuote tu kuwa anaweza kuwa hivyo?
 
Huyu jama kweli hajajibu hoja ila amejibu kimipasho nadhani kwa nchi yetu tunahitaji mtu ambaye ana maamuzi si mtu muoga asiyeweza kutoa sauti kukemea jambo tukichagua mtu wa jinsi hiyo nchi haitaenda. Tunahitaji kiongozi mwenye mamlaka na mzalendo anayeweza kusema hapana.
 
No research no right to speak! naona umeparaza research; hukuzamia! kabla ya kupitisha azimio la kumkatia chini Dr. Salim; tafadhali rudia tena!

Dr. Salim ni Presidential material ambaye Tanzania imemkosa kwa sababu ya siasa za maji taka kama nilivyoona wengine hapa jamvini wakichangia.

SIASA ZA MAJI TAKA = Akili zisizo na akili, udini, ubaguzi wa rangi, Uhafidhina, wivu; umimi; you can mention anything else na vitu kama hivyo!!

Kuropoka ropoka hadharani hakumfanyi mtu kuwa na uwezo wa kuwa kiongozi dhabiti;

Dogs who bark the loudest are not neccessarily the fiercest or the best WALINZI

Dr Salim ni kimya kingi chenye mshindo mkuu. muache mzee wa watu apumzike na wala hajatamka anautaka urais; 2005 was his last attempt by his own decleration.
 
mtazamo wangu mleta hoja ana hoja ya msingi hapa! Kama walivyosema waliotangulia, tuondoe hisia hasi au kujenga hoja ya nguvu badala ya nguvu ya hoja! Udini wa Dr. Salim si hoja na wala mleta mada haoneshi kuficha chochote katika mada yake. Labda kama kuna mtu anataka kusema kwamba ni mapema kumjadili mtu anayefaa kuwa mgombea wa urais wa nchi hii, alete hoja hiyo na uhalali wa kufikiri hivyo ili atuaminishe wengine kukubaliana naye...

Tupangue hoja moja baada ya nyengine katika hoja zake ili naye aelimike pamoja na akina sisi tusiopenda sana siasa. Inawezekana anazodhani ni hoja pengine zina majibu na hivyo asiporidhika/tusiporidhika basi tutawekwa katika kundi la watumia hoja ya nguvu badala ya nguvu ya hoja...
 
Candid Scope, DULLAH MSAVIVOR,

..hatujamsikia Dr.Salim akipinga ufisadi.

..hatujamsikia akikemea na kupinga udini na ukabila.

..hatujamsikia akikemea ubaguzi wa waZNZ dhidi ya wa-TGK.

..hatujamsikia akitetea muungano, au akipendekeza muundo bora na wa haki wa muungano.

..hatujamsikia akipinga sera za uuzwaji holela na umilikishwaji wa mali za umma.

..inasemekana ni mwanafunzi nambari wani wa Mwalimu Nyerere lakini hatetei siasa za ujamaa, wala hahubiri sera ya kujitegemea.

..hatujamsikia akitetea nafasi ya Tanzania ktk jumuiya ya Afrika Mashariki.

..hata wakati wa harakati za KATIBA MPYA hatukumsikia akieleza msimamo wako.

..the man is just silent and indifferent kwa mambo yote yanayomkaibili nchi yetu na mwananchi wa kawaida.

..inasemekana anajiweza, lakini sijawahi kusikia amechangia msikiti, kanisa, shule, kisima cha maji, timu ya mpira, popote pale nchini.

cc: Kubwajinga, Nguruvi3, Ritz, njiwa
 
Kila mara yanapojiri maswala mazito ya kitaifa kama hili la udini sasa; viongozi wote wa vyama vya siasa wangefanyiwa mdahalo wa kitaifa wa pamoja ili waeleze nini sera na mapendekezo ya vyama yao (kila chama) katika kukabiliana na uzito wa swala liwalo. Hapo tunaweza kuelewa chama kipi kitatufaa watanzania na kiongozi yupi kakomaa na hivyo kutuongoza. Tusisubiri tu kampeni za uchaguzi- ni mbali mno.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom