Warioba: Mimi na Salim urais basi

Warioba: Mimi na Salim urais basi

JF tumekuwa wavivu wa kufikiri kiasi hiki?? sio haja ya kuunda tume ya matokeo ya form kama hali yenyewe ndio hii.
 
Kuna wengi tu waliotendewa mabaya zaidi ya Salim kama Mwakiembe hadi kukimbizwa hospitalini India, lakini kwenye ukweli na kupinga maovu wanajitokeza. Kunyamaza huko hakuleti picha nzuri kama anataka kuwa kiogozi bora wa wananchi. Anatakiwa kuonyesha msimamo wake katika kuwatetea na kuwapigania wananchi. Vinginevyo uadilifu katika maisha si kigezo pekee cha kufaa kuingia magogoni. Tunao waadilifu wengi lakini wengi wao hawafai kuongoza nchi.
Asante mkuu, lakini mimi naona Salim Ahmed Salim si mtu ambaye ana nia ya kuingia Ikulu, tukiacha maneno ya wapambe.
Unajua siasa si mtu ufikie apex of power, wakati mwingine kubaki kando unatunza heshima yako vizuri zaidi.
 
Asante mkuu, lakini mimi naona Salim Ahmed Salim si mtu ambaye ana nia ya kuingia Ikulu, tukiacha maneno ya wapambe.
Unajua siasa si mtu ufikie apex of power, wakati mwingine kubaki kando unatunza heshima yako vizuri zaidi.

Kwa hoja ya uadilifu naungana nawe, hajachafuka kama walivyo wengi ndani ya serikali. Lakini siasa za siku hizi ni za ushindani si kama ilivyokuwa enzi za chama kimoja kushika hatamu za uongozi. Anaakiwa kuonyesha msimamo wake katika masuala muhimu ya kitaifa ambayo yanawaumiza sana wananchi wa Tanzania na ndizo siasa zitakazotawala wakati wa kampeni zijazo. Hizi si enzi za kunadishwa bali kujinadi.
 
Aaah Wapi,

Mmeshaanza siasa zenu za majitaka sasa,,

Hebu niambie wewe sasa.humpendi huyu kwa chuki zako binafsi au humpendi kwa kuwa yuko CCM??

Akisimama huyo 2015 hatuna budi kumpatia nchi hii,mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni..

Au kwa kuwa ni Muislam??

kuna maswali nilikuuliza kwenye mada yako ya maambo ya udini hukujibu ukakimbia. Naona unaendeleza tena huku. Hata mi naona wakati wa Dk Salim ulikwisha kipindi kile anafanyiwa mizengwe na mwislam mwenzie-jk.
 
Kwenye hoja za kisiasa za kumpima mtu tujaribu kuondao kipengele cha udini.Otherwise safari hii iwe zamu ya Mpagani.Maana chochote kitakachojadiliwa kwa nini baadhi yetu wanaweka kipengele cha udini.TUjitahidi kujifunza either kukubali hoja ya mtu ,kuikataa kwa hoja au kukubali katika kutokubaliana.

Tanzania kwanza mengine baadaye.
Ni upuuzi kujibu hoja za mtu kwa kuingiza haraka masuala ya udini,tena kuna watu siku hizi humu jukwaani wameshafanya ni sifa kila kitu mara mwislam,mara mkristo...MODS tafadhali musiwaache watu wa dizaini hii watuharibie jukwaa,piga BAN ya maisha pliiiiizz!!!!
 
Kama ingekuwa ruhusa kuajili rais kutoka nje ya nchi,nadhani tanzania ingefaa sana kwa wakati huu kumpata rais wa kuajiliwa toka nje ya nchi kwani. Hakuna anayefaa kuwa rais kwa tz hii
 




sidhani kama ulinisoma sahihi.. hakuna sehemu niliyompongeza dula "kwa lile swali alilouliza" au kusema kwamba mleta uzi anamkataa salim kutokana na uislam wake...

nimempogeza dula kwa kusoma btw lines kuona kwamba hakuna lolote zaidi ya siasa za majitaka....

sijaingiza dini katika post zangu ndani ya hii thread :nono: naona umehamaki naku replay kwa hisia zaidi baada ya kuona aliyejibu ni njiwa , na kwa standard zenu JF njiwa ni mdini kwasababu anajiweka wazi yeye ni muislam humu JF


Yap Yap..

There is nothing wrong in our religion Njiwa,tell them our Islam teaches us to suffer peacefully. Our religion teaches us to be intelligent. Be peaceful, be courteous, obey the law, respect everyone; but if someone lays a hand on us,we send him to the cemetery..

Hawamtaki kwa kuwa SAS ni Muslim??..
 
Ni kweli ndugu yangu. Hakuna masuala ya kuwaza eti ni muislamu au ni mkristo. Suala hapa je ni mtu wa aina gani? Kama mtu anayetaka kuwa raisi wa nchi yetu haoneshi msimamo wake katika msuala ya msingi ni lazima atiliwe mashaka! Yametokea mambo mengi sana katika nchi hii ambayo watu wenye kulitakia mema taifa letu walipashwa kusema lolote. Dr Salim ukimya wake na kutazama mambo yanavyokwenda kunatia shaka kama naweza kuwa rais mwenye msimamo thabiti. Hebu tazameni wengine waliwahi kusema wana smile lakini smile yao inaficha ukali ndani yake kumbe si lolote. Hivyo ndivyo alivyo kucheka cheka hata katika masuala ya msingi. What if Dr Salim naye ndiyo hulka yake? Tutakuwa tumepoteza tena kwa miaka 10? Hapana, jamani tufike mahali tuseme sasa imetosha, the country must move!..
Mleta mada ameweka hoja zake, jaribu kuleta hoja za utetezi badala ya kujibu kimipasho. Hapa hatujadiri mambo mengine katika mada hii zaidi ya kupima uwezo wa presidential candidates, tunahaki ya kupima uwezo wao mapema badala ya kutumbukiza tu kura sandukuni baadaye tuje kulalamikia uwezo wao kuwa mdogo kuongoza watanzania.
 
I concur with you Mungo Park.

Labda tu la kuongezea ni kwamba nionavyo mimi SAS hafai kuwa Rais ajaye wa Tanzania na sababu ni simple sana, nayo ni kwamba hatujui msimamo wake ukoje kwenye mambo mbalimbali pamoja na ya msingi yanayoikabili nchi yetu hasa katika kipindi hiki cha mpito chenye kushuhudia a great political and socio-economic transformation katika jamii yetu, mfano mzuri ni utungaji wa katiba mpya, uchumi kuwa determined na nguvu ya soko na kuendeshwa na sekta binafisi zaidi kuliko uchumi hodhi wa serikali/nchi.

Namuona SASA kama ni mkimya sana hata kwenye mambo ya msingi yanayotokea kila siku be political, social, economical ect.

Lakini pia na muhimu sana ni kwamba hatuna track record yake kwenye utendaji, ubunifu na usimamizi katika nafaso alizowahi kuzishika au hata kwenye maisha yake binafis. Zaidi tuu ya kupata pengine 'bahati' ya kushika nyadhifa nyingi za kidplomasia na labda ilitokea tu by chance au bahati sioni any other added advantage aliyo nayo.

Labda ili tumfahamu tujaribu kumulika kule alikokuwa katibu mkuu metendaji wa OAU. Je by then ni yepi atajivunia kama ni mchango wa ubunifu au utendaji wake? Anayefahamu anitajie....

Kiukweli kosa kubwa tutakalofanya watanzania this time ni kuchagua mtu kutokana na jina lake au umaarufu wake bila kuangalia track record yake katika utendaji, ubunifu na uadilifu. Rais Kikwete alipata kuwa rais kwa sababu watanzania hatukuwahi kuhoji hayo maswala ya msingi juu yake: utendaji, ubunifu na uadilifu. Tuliangalia zaidi jina na umaarufu wake bila kuangalia track record yake katika haya. Wote leo hii kwa namna mbalimbali you can attest this country is run in auto-pilot mode, wakati JK yupo bize anakata naga daily...

Lakini pia by 2015 Salim atakuwa na miaka 70 na nadhani umri pia utakuwa umemtupa mkono. Nafasi ya rais inahitaji nguvu ya kimwili na kiakili. kwa umri huo dementia, brain atrophy and degeneration zinamhusu.na hii huwapata kwa wingi sana watu wa umri huu. Hata yeye hayupo spared katika hilo. Lakini pia siasa ya dunia ya sasa tunashuhudia ilivyo na mikiki mikiki, nadhani inahitaji zaidi 'vijana'

Kwa ufupi SAS hatufai kuwa rais wetu. Tunamhitaji rais mwenye sifa tukuta katika hayo maeneo niliyoainisha: utendaji, ubunifu na uadilifu. Short of this we are doomed kwa miaka mingine na tutakuwa tunapiga mark time sana tu wakati wenzetu wanakimbia.

Kindly naomba tujadili kwa hoja na si udini wa mtu. Dini yake inamhusu yeye na Mungu wake. Siku ya hukumu kila mtu atapeleka hesabu yake yeye mwenyewe na atahukumiwa yeye mwenyewe kadri ya matendo yake bila kujali kikundi cha dini.

Asanteni
 
Last edited by a moderator:
Mmeshaanza siasa za majitaka kama kawa... Haya endeleeni kumnanga na kumchafua kama kawaida yetu...Lunatic can destroy everything hata kinachomsaidia...
 
Candid Scope ingekuwa vizuri kama unge-declare interest, uko kundi gani la wagombea urais, uko kwa six, white hair, mzee wa ushirikiano wa kimataifa, ili tujue kama hakuna kitu kilichokusukuma kumwandika hivi mzee salim.
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli ndugu yangu. Hakuna masuala ya kuwaza eti ni muislamu au ni mkristo. Suala hapa je ni mtu wa aina gani? Kama mtu anayetaka kuwa raisi wa nchi yetu haoneshi msimamo wake katika msuala ya msingi ni lazima atiliwe mashaka! Yametokea mambo mengi sana katika nchi hii ambayo watu wenye kulitakia mema taifa letu walipashwa kusema lolote. Dr Salim ukimya wake na kutazama mambo yanavyokwenda kunatia shaka kama naweza kuwa rais mwenye msimamo thabiti. Hebu tazameni wengine waliwahi kusema wana smile lakini smile yao inaficha ukali ndani yake kumbe si lolote. Hivyo ndivyo alivyo kucheka cheka hata katika masuala ya msingi. What if Dr Salim naye ndiyo hulka yake? Tutakuwa tumepoteza tena kwa miaka 10? Hapana, jamani tufike mahali tuseme sasa imetosha, the country must move!..
Kwanza kwa hali ya afya yake sidhani kama SAS anataka kutafuta Urais tena. Naona wakati wake umeisha pita,na ni vema akajitokeza mapema akatoa msimamo. Bila hivyo atachafua hata hiyo heshima kiasi iliyobakia. Pili siyo SAS tu ndani ya CCM ambaye yupo kimya wakati taifa linapopata misukosuko ambayo tungetarajia hawa jamaa wanaojiita wasafi ndani ya CCM tusikie msimamo wao. Wote wapo kimya. Kwangu maoni yangu kama Tanzania inataka kuondoka hapa tulipo kwama,hakuna budi kuiondoa CCM na watu wake ili tuanze upya!
 
Hz sio siasa za majitaka wakuu. Binafsi sijawahi kumsikia huyu ndugu akijadili au kutoa kauli yeyote kupinga, kukubali au kusisitiza jambo. Kwa ujumla haeleweki. Penye ukweli tuzungumze jamani. Inaonyesha hana msimo.
Hivi Kiongozi au Rais ni yule anayepiga kelele majukwaani na kwenye vyombo vyahabari?Wanaokumbuka SalimA. Salim alifika Mtwara akakuta watu wanavaa mifuko ya Sandarusi (mifuko mitupu ya mbolea ya Sulphate) akauliza sababu ni nini na ndani ya wiki masharti ya kuzuia kafaUlaya yakalegezwa na mitumba ikaingia
1987-1988 akalikuta Jeshi letu lina usafiri wa Land-Rover 109 na zimechakaa akaagiza Nissan kibao kwa JKT na JWTZ bado mlitaka asimame majukwaani na kupiga kelele (........ KUWENI MACHO HAWA VIJANA NA AJIRA NI BOMU LINALOTARAJIA KULIPUKA....)
si lazima kwa kila kiongozi kuwa msemaji wa majukwaani ndio akawa kiongozi mzuri na anayethubutu
 
Candid Scope ingekuwa vizuri kama unge-declare interest, uko kundi gani la wagombea urais, uko kwa six, white hair, mzee wa ushirikiano wa kimataifa, ili tujue kama hakuna kitu kilichokusukuma kumwandika hivi mzee salim.

Du mbona umekosea kabisa huyu jamaa Candid Scope huko hayupo kabisa kwenye hilo kundi la Magamba,
 
Last edited by a moderator:
Huyu Mzee nampenda sana tena sana na anatumia busara za ajabu.kumbuka uchaguzi ule ukamweka Lowassa kuwa Waziri mkuu na Jk Kuwa Presdahh wa nchi hii?
kama utakumbuka walitaka kumchafua sana kwenye zile kampeni zao.Unakumbuka ama?
Akajionea haina sababu ya kuharibiana jina hasa kwa mtu kama yeye toka hapo akawa kimya adi leo hii anajilia vyake.
 
Sioni sababu ya ukimya kama inamantink.....

Bora raisi akawa mtu ambaye si maarufu kwan anaweza fanya makubwa zaidi....chukulia mfano mwakyembe hakuwa anajulikana lakin baada ya report ya richmond watu walifahamu utendaji wake wa kazi

Afu tuchukulie mfano wa Ben alikuwa kimya sana na hakuwa maarufu wa jukwaan lakin alifanya makubwa....

Kwan ww mtoa thread hii unadhan umaarufu wa kisiasa jukwaan unaweza ukamfanya mtu awe bora kiutendaji???????

Chukulia mfano sugu na Dr salim nan maarufu jukwaan??? Je unaweza kuwalinganisha kiutendaji????

Tunataka raisi mpiga kazi si maarufu wa majukwaaaa????





Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Dr.Sali ni mwanadiplomasia sio mropokaji kama hao tunaowasikia kila siku na hata aliposhambuliwa hakuangaika kujibu siasa zenu za maji taka ndio zinawapa hofu iwapo atachaguliwa anaweza kulipa kisasi subiri 2005 watakaojitokeza ndio tujadili nani anafaa na nani hafai wewe sio wa kutufundisha nani awe rais wa Tanzania
 
Mleta mada amefafanua vizuri kabisa hoja zake kuhusu Salim, Wala hajagusia masuala ya dini kwa kuwa inafahamika kuwa akiwa Rais hataongoza kwa kutmia dini. Tulitegemea atakayetetea naye atoe hoja, katika mshangao wa wengi ndugu hujatoa hoja yeyote na badala yake umekimbilia tu dini, Inaelekea wewe unachoangalia kwanza kwa mtu yeyote ni dini kabla ya mambo mengine. Na inaelekea ukiulizwa ni kwa nini awe rais unaweza kusema kwa sababu ni muislamu. Tafadhali nakuomba ishia hapahapa na mambo yako ya dini, usituharibie thread, haihusiani na dini.
Aaah Wapi,

Mmeshaanza siasa zenu za majitaka sasa,,

Hebu niambie wewe sasa.humpendi huyu kwa chuki zako binafsi au humpendi kwa kuwa yuko CCM??

Akisimama huyo 2015 hatuna budi kumpatia nchi hii,mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni..

Au kwa kuwa ni Muislam??
 
Salim kwa sasa hana dira ya namna ya kukabiliana na siasa za Tanzania, hana dira ya kukabiliana na uchumi mambolea wa dunia, Hana dira ya kukabiliana na wanaohoji usafi wake katika siasa za Zanzibar!

Enzi zake zimeisha hivyo ni vema tukamwacha apumzike kwa amani!

Salim ana majeraha makubwa rohoni ambayo hayatapona kamwe! Mtu kama huyu hafai kuwa kiongozi wa Taifa!
 
Back
Top Bottom