George Smiley
JF-Expert Member
- Oct 24, 2011
- 471
- 267
Mpitagwa,
Wewe umeona hili, wengine wanachoangalia bora tu kuwa na rais bila kuangalia mazingira na hali ya siasa na kiuchumi ilivyo sasa nchini. Mgombea urais anatakiwa aonyeshe yale ambayo wananchi wanaona ni tatizo kwa maisha na maendeleo ya nchi. Pamoja na kutokuwa na nafasi ya kutenda, lakini hata kauli tu inaweza kutoa picha ya kile anachokifikiria ndani ya moyo wake. Ndio maana siku hizi kuna debate kwa wagombea, licha ya debate, kuna vigezo ambavyo kabla ya uteuzi vinaangaliwa kama mtarajiwa anafaa kutokana na mwenendo wake wa maisha katika taifa letu. Mtazamo wake kwa watanzania, ubunifu wa mipango ya maendeleo na mfumo wa serikali.
Tunahitaji rais licha ya kuwa na panga la makali kuwili, aonyeshe ubunifu wa kuigeuza Tanzania kuwa taifa lenye kuwa na dira ya maendeleo kwa ulimwengu wa leo tokana na utajiri wa mali asili tulizo nazo. Ahadi za barabara zimekuwepo tangu tunapata uhuru, shule hali kadhalika, lakini sijaona hoja mbadala kwa marais waliomfuata Nyerere kujenga msingi wa uchumi wa kitaifa unaotegemea utajiri wa rasilimali za nchi yetu.
Tahadhari:
Vigumu kumgeuza aliyezoea kuruka angani aanze kutembea kwa miguu, kupanda baiskeli na kwenda vijijini kwa wananchi, kuamua kula mihogo Ikulu kwa kikombe cha tangawizi, kuzoea kula bilinganya zinazozalishwa na bustani za bonde la msimbazi badala ya vyakula vya mahoteli ya kitalii duniani.
Nadhani hoja yangu mwaipata. Somo tunalo, tumeliona. Je, tumejifunza nini na tumejenga tahadhari gani?
Acha kuwa na mawazo mgando
nchi hii ina watu milioni 45 ambaoa kati ya hao walio na umri wa chini ya miaka 20 ni asilimia 70
bado tuu unalalamika kwa mtu mmoja kutosema jambo?
Mbona husemi kitu kuhusu kimya cha Mzee ABOUD JUMBE?