'Wapiganaji' walioko CCM wanapigania nini hasa?

Rev Ushauri mzuri.

Lakini sometimes is easy said than done kama uwanja wa mpira kwenye mashindano ambayo timu uipendayo inacheza na wewe uko bench unavyoweza kukosoa mchezaji wakutegemewa alivyojifunga goli.

Tatizo kubwa linalotusumbua ni life after the action you decide to take. Kwa nchi kama za kwetu unaweza kujikuta wewe kwa mob psychology ukaishia kuwa Bangusilo maana kati ya hao kumi na moja walio ji identify huenda wawili tu ndo wanamaanisha na wengine sitaki na taka. Ukiangalia wewe ndo tegemeo la ukoo mzima na family iliinvest kwa wewe kufika hapo what do you do?

Vita kama hiyo rahisi kwa watu ambao calculated risk is more than 50% sasa who knows may be thats what they are doing sasa si ndiyo na wewe ukawa mpiganaji wa wanyuma (comanding unit) msituni na wao wako front line? Kama hata waliweza kuwa consult at certain point huoni hata hapo wali dare?

Felister,

If they are FEARFUL of life after sction, then they do not deserve an audience!

Mandela was Bangusilo, and so was Mrema, Lumumba, Kenyatta, Njelu Kasaka, Jumbe, Hamad including Kawawa and Nyerere.

Wao wanaogopa Chama na hatua za Chama kuwminya haki yao? Sasa mlalahoi atasemaje?

Kwa wao kuogopa Life After Action, kunatangazia umma wazi kuwa Chama chao na Serikali yao si kwa ajili ya Wananchi, haifuati haki wala kujali utu, haina Demokrasia na ni Chama na Serikali gandamizaji.

Let say walipokutana Butiama, waliwakilisha hoja ya Chama kutoa karipio na adhabu kwa Lowassa, Chenge, Karamagi na msabaha kwa kuliingiza Taifa hasara kutokana na Uzembe na mazingira ya Rushwa? Je waliwasilisha hoja kutaka hawa Wanne wavuliwe Ujumbe wa CC na NEC? Je walishurtisha hawa jamaa Wanne na Rostam waombe radhi kwa makosa waliyofanya?

Kama walifanya hivyo na hawakusikilizwa na kupuuzwa, kwa nini wanaendelea kuinadi CCM na kudai CCM ni chama bora?

Hivyo vita vyao vinapaswa kuwa dhidi ya mfumo mbovu na si kung'ang'ania kutajana majina ya waliohujumu!
 
Sehemu ya pili itaendelea kesho; hasa tukiangalia mikakati wanayotumia kwanini itawaangusha. Mkakati mmojawapo ambao umewatengenezea kushindwa kwa wapiganaji walioko CCM ni kumhusisha Mfanyabiashara maarufu nchini Bw. Mengi. Ni mkakati unaomhatarisha Mengi, na kwa hakika unatishia uhai wa kisiasa wa wapiganaji.
 
Mzee Mwanakijiji,

Vita dhidi ya Ufisadi hailipi kisiasa. Angalia chaguzi zote ndogo tangu tugundue kuna Ufisadi, imekuwaje Wapinzani wakaangushwa kila kona kasoro Tarime!
 
Wanaipigania ccm huku wakiialaumu kwa kulea Ufisadi, huu ni Unafiki wa Daraja la Juu
 
Kulipwa posho mara mbili mbili, kulilia kutaka huruma ya wananchi.

Huku spika wao akiwatetea

Jamani hakuna jema linalotoka CCM!
 
Rev Kishoka,
Mkuu wangu hoja yako kubwa ni kama vile una question Upiganaji wa Obama na senate wote kuhusu Terrorism wakiwa bungeni wakati wapiganaji haswa wako mstari wa mbele huko Afghanistan na Pakistan.
Nitarudia kusema kwamba siku zote mbunge anayekuunga mkono HOJA yako ni mtu wa kumsifia kwa sababu katambua umuhimu wa vita yako badala ya kufikiria mtu huyo ni tapeli tu kwa sababu yuko chama tawala...Nguvu ya hawa wapiganaji ikiunganishwa na nguvu ya vyama pinzani, sisi wananchi tunaweza kushinda vita hii lakini kama sisi wenyewe tutaanza kugawanyika na kunyoosheana vidole, trust me tunavunja nguvu ya UMOJA na waathirika watakuwa sisi wenyewe.
Iwill always stand with Wapiganaji..Na labda nikupe kali kuliko zote.. Lowassa kesho akisema atnataka Azimio la Arusha lirudishwe.. nitampa tano maanake yupo mbioni kuungama.. haya maswala ya ku question kuungama kwake yatakuja baadaye kwani yawezekana kabisa amekiri makosa yake na yupo tayari kuadhibiwa..lakini kama tutamkana yeye pamoja na hoja yake basi bila shaka tumetokomeza hata wazo kubwa la vita dhidi ya Ufisadi.
 
Kulipwa posho mara mbili mbili, kulilia kutaka huruma ya wananchi.

Huku spika wao akiwatetea

Jamani hakuna jema linalotoka CCM!
Mzee huu ni mfumo mbaya wa nchi kiujumla toka baada ya uhuru. haya ya posho hayajaanza leo. Lakini tatizo sio CCM bali ni mfumo, na kutatua sio kumwita mmoja mmoja bali ni kutunga sheria. nani atunge mlaji? hapo nipo ipo kazi. lakini hata wapinzani wanafanya nini bungeni kama nao si kula tu? hawana jipya pia ndio maana unaona kwenye uchaguzi mdogo wamepigwa buti na CCM.
 


Na Mbasha Asenga

RAFIKI yangu mmoja raia wa Kenya alinisimulia siasa za Wasomali kwamba pamoja na kujitia vichwa maji, kuna kitu kimoja tu kinawafanya wawe na suluhu ya muda katika mapambano yao.

Alisema kwa kawaida wakati wababe wa vita wakiwa wanaendesha ubabe wao wakipambana kwa kutumia kila aina ya silaha, kuna wakati huweka chini silaha zao, wakati huo si mwingine isipokuwa ni wa kupokea shehena ya mirungi.
Kwamba mzigo wa mirungi ukiingia mjini, Wasomali wanasahau tofauti zao, wanagawana kwanza mirungi kila mmoja anaondoka na hapo mapambano huanza upya.

Hakuna ubishi kwamba Wasomali wanapenda mirungi, huitafuna kwa bidii kubwa. Sina uhakika juu ya madhara yake katika mfumo wa chakula mwilini, lakini ni ukweli usiopingika kuwa watu hawa wamekuwa mateka wa mirungi. Huu ni ulevi mbaya kwa wasomali wengi.

Pamoja na ujeuri wa Wasomali na tamaa yao ya kuonyeshana ubabe katika vita, ulevi wa mirungi ni moja ya vitu vinavyowashawishi kusitisha vita japo kwa muda.

Ulevi huu wa Wasomali unafanana na hamu ya kutaka madaraka kwa wale wanaoitwa wapambanaji na watuhumiwa wa ufisadi ndani ya CCM.
Kwa muonekano wa nje, tangu serikali ya awamu ya nne iingie madarakani imejipambanua katika makundi makuu mawili; moja ni kundi la wapinga dhuluma, wizi, unyang’anyi na aina zote za matendo ya ukingeukaji wa maadili ya kiuongozi na utumishi. Hawa ni wapambana dhidi ya ufisadi.

Mbili, ni kundi la watu waliokuwa wanatuhumiwa kwa kila uchafu; wameitwa chanzo cha njaa, umasikini na masaibu yote ya Watanzania. Wameitwa watu walafi, wanaopenda kujilimbikizia mali kwa njia za hila, na kwa ujumla wao ni watu wasiokuwa na huruma na kudumaa kwa maendeleo ya nchi kwani wao ndiyo kiini cha kudumaa huko.

Katika mazingira ya kawaida, makundi haya hayana tofauti na makundi ya wababe wa vita wa Kisomali kwa maana ya uhasama uliojijenga baina yao. Makundi haya ndani ya CCM yamepambana kwa takribani miaka mitatu, kila mmoja likitaka kuangamiza jingine. Mbinu sahihi na chafu zimetumika kumalizana.

Katika mapambano yao makundi haya yalijijengea uhasama wa kweli, chuki isiyoelezeka, lakini kwa mashangao wa wengi hivi karibuni waliweka tofauti zao pembeni kama vile Wasomali wanaosubiri kugawana shehena ya mirungi. Kwa Wasomali inajulikana, lakini kwa hawa wenzetu imekuwa ni vigumu kujua ni kitu gani hasa kiliwapa suluhu hiyo.

Kwa Wasomali suluhu ni mirungi, kwa makundi ya CCM ni uchaguzi. Kwa maneno mengine, wanasiasa wa CCM wanaweza kuweka rehani chochote; utu wao, hadhi yao, hisia za wananchi, matarajio ya wapigakura wao na hata imani ya umma kwao ili mradi tu wawe na uhakika walau wa kukubalika kuteuliwa kushiriki uchaguzi mkuu.

Kwa hali hii si jambo la kushangaza tena kusikia kwamba Wasomali wana kitu kinachowagusa kwa undani sana kiasi cha kutundika bunduki zao; kiasi cha kusahau ubabe wao japo kwa kitambo kidogo tu, kwani hata makundi mengine kama hapa nchini wana vitu vinavyofanana na hivyo.

Kwa Wasomali watu wanawashangaa, huku wakisahau kwamba hata ndani ya CCM makundi yake ambayo ni hasimu kwa maana ya neno hilo, yana ulevi wake mkali kama wa mirungi.

Yaani Wasomali wanapokuwa hawaelewi kitu wakati wanakosa mirungi, makundi ndani ya CCM hata kama yalikuwa na hoja gani za kimsingi dhidi ya kundi jingine?
Hata kama kundi moja lilikuwa limejikita kwenye hoja gani ya kukomboa wananchi, kutetea haki zao na kujitoa kwa nguvu zao zote kuendesha mapambano hayo, inapokuwa sasa ni kuamua juu ya uchaguzi, tofauti zao zinazikwa hapo hapo, tena kwa mbwembwe za ajabu kutaka kuusadilisha umma kwamba kazi imekamilika na kilichobakia ni umaliziaji tu.

Ulevi ni hali ya mtu kupoteza fahamu zake, aghalabu mlevi hufanya vitu ambavyo asilani hasingevifanya akiwa na akili timamu, ulevi humjengea mtu ujasiri wa kitambo, lakini nguvu ya ulevi ikimwacha, basi hujikuta katika sononeko kubwa la moyo; majuto makubwa na pengine kujilaumu ambako hakurejeshi kwa hali yoyote ile hali ya awali.

Ndiyo maana hadi leo wiki kadhaa sasa baada ya makundi ndani ya CCM kuonyesha wanavyolewa uchaguzi, kuthibitisha kwa kauli, mawazo na matendo halisi kwamba kwao hapendwi mtu ila ulevi –uchaguzi, wengine tungali tunajiliza hivi baada ya Oktoba mwaka huu, wakishachaguana na kurejea bungeni, nani atathubutu kunyanyua kinywa chake na kutamba kwamba eti yeye ni mpambanaji dhidi ya maovu?

Je, nini sasa kitazuia hukumu ya umma kwa makundi yote hata ndani ya chama hiki kwamba wao ni ndugu mmoja, baba mmoja na mama mmoja, wao ni waumini wa kusaka madaraka ya wananchi, wapo tayari kuhadaa kwa njia zozote, lakini asilani si watetezi wa kweli wa hoja wanazojaribu kuzibeba kwa njia ya kuigiza.

Katika hali ya kawaida ilitarajiwa kwamba katika harakati za kuelekea uchaguzi ndipo makundi haya yachujane, kwamba wale wanaojipambanua ni watetezi wa wananchi, wenye uchungu na nchi hii wangejitwika hoja yao ili sasa umma uwaunge mkono kwenye sanduku la kura, lakini walichofanya wamegeuka na kukumbatiana na wenzao, katika dini moja na imani moja ya kuchaguana huku wakiuacha umma kwenye machungu na mashaka makubwa.

Kama kweli makundi haya hasimu ya CCM yameweza kufuta tofauti zao hata kama ni kwa kitambo kidogo tu ni uthibitisho kwamba wananchi kama wanataka ukombozi basi watasubiri sana , hakika hautaletwa na hawa wanaojitia kuwakilisha maslahi ya wananchi kwa sasa.

Kwa mara nyingine tena makundi ya CCM yamethibitisha kwa undani sana jinsi yanavyofungamana, kwao makundi ni igizo la muda kabla ya uchaguzi, uchaguzi ukiwadia ambao ndiyo ngazi muhumu kutafuta majemedari wa kuongoza mapambano ya ukombozi wa kweli wote ni wamoja, waugizaji na walaji, hawana nia wana sababu ya kukomboa nchi.

Kwa hili wamefanana na wale Wasomali wanaoweka chini bunduki za rashasha, jeuri na ubabe wote ili tu wagawane mirungi, kwa CCM wanatupa tunu ya uadilifu, uchapakazi, utumikiaji wa umma na ujemedari wa ukombozi kwa sababu tu ya kupata fursa ya kuchaguliwa kuwania madaraka ndani ya mchakato wa chama.


Source: MwanaHalisi
 
MWANAHALISI RUDINI KWENYE MSTARI, MNACHEZA NGOMA YA MAFISADI!

Na Doulton Kamauma
Nimesoma mfululizo wa makala za MwanaHalisi (Toleo Na.178 la Machi 3-9, 2010) juu ya Bunge na sakata la Richmond kwa umakini mkubwa. Makala hizo ambazo zimeandikwa na Mbasha Asenga (Wapambanaji wa CCM sawa na walevi wa Mirungi wa Kisomali) na Saed Kubenea (Kufunga Mjadala Bungeni ni kukejeli Umma), zinalalama kwa ukali kwa nini mjadala wa Richmond umefikia hatma yake Bungeni badala ya kuendelea tu pengine mpaka baada ya Bunge jipya kuzinduliwa mwishoni mwa mwaka huu kufuatia kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu.
Kwa maoni yangu, makala zote mbili zinaonesha udhaifu mkubwa tulionao katika uandishi wa habari nchini wa kukosa uchambuzi wa kina wa taarifa, uelewa mpana wa taratibu za kibunge na vilevile wa sheria na Katiba. Matokeo yake ni MwanaHalisi kushindwa kuupa umma picha halisi na kuishia kucheza ngoma ya Mafisadi bila kujua.
Naomba nitoe tahadhari kuwa mimi si msemaji wa Bunge au wa Spika wa Bunge la Tanzania. Ni Mtanzania wa kawaida mwenye uelewa wa kutosha katika fani za siasa na uandishi wa habari ambaye ningependa mawazo yangu juu ya suala hili yajulikane na wengi.
Kwa uelewa nilionao, moja ya kanuni za msingi za uandishi bora wa habari ni kwa mwandishi kujiweka kwenye nafasi ya hakimu au refa asiye na upande au kwenye nafasi ya kurunzi ya jamii. Udhaifu unajitokeza pale ambapo mwandishi anajirahisisha na kuwa sehemu ya washitakiwa mahakamani wakati huo huo akiwa ameshikilia kirungu cha uhakimu au pale ambapo uzalendo unamshinda, anaingia uwanjani kusakata kabumbu huku akiwa na filimbi ya urefa mdomoni! Huu ndio udhaifu mkubwa wa waandishi wengi wa Kitanzania: kujiruhusu kubebwa na hisia katika jamii, hivyo kushindwa kufanya uchambuzi wa kina, kuwapa wasomaji nyama ya kutosha ya kutafuna ili wacheue wenyewe, hivyo kushindwa kutoa picha yenye pande mbili za sarafu.
Nianze na makala ya Kubenea inayomshutumu Spika Sitta kwa kufunga mjadala wa Richmond, hatua ambayo Kubenea (kwa bahati mbaya sana) anadhani ni sawa na mwisho wa dunia na kuishia kulalama. Kwa tafsiri yangu ambayo naamini ni sahihi, Sitta hajaua mjadala. Alichofanya ni kufunga mjadala Bungeni kwa maana ya suala hilo kutoendelea kuwa suala tarajiwa kwenye Orodha ya Shughuli za Bunge, lakini ambalo laweza kuletwa upya tena kwa umakini zaidi kama hoja mahsusi chini ya Kanuni ya 64(1)(c) na 54(4) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2007. Sasa kilio cha Kubenea ni nini kama si kuwapotosha wasomaji wake; kama si kumvunja moyo Spika Sitta aliyeleta, tupende tusipende, mapinduzi makubwa ya Bunge nchini na katika kipindi kifupi sana?
Kauli kali ya kwanza ya Kubenea kuwa “Spika Samwel Sitta ameng’olewa meno na kurejeshwa katika dini yake ya asili. Viwango na kasi -standard and speed- … vimepigwa kikumbo …” ni hukumu za mkato tulizozoea kuzisikia vijiweni na kwenye ushabiki wa kandanda ambazo kwa hulka yake hazihitaji urari wala ushahidi wa kuridhisha. Ni jazba na “kukandiana” tu ambako hakustahili kuwa sehemu ya sifa ya gazeti makini kama MwanaHalisi!
Pamoja na kukosea kunukuu jina la kwanza la Spika na vilevile neno la kwanza la kauli mbiu yake, Kubenea anataka dunia nzima ikubaliane naye kuwa kwa uamuzi huo wa kawaida tu wa kikanuni, Sitta si lolote, si chochote! Yote makubwa na mazuri ambayo Sitta kayafanya kuliinua Bunge la Tanzania kuwa moja ya Mabunge imara duniani, ni bure kwa sababu Richmond haitakuwa kwenye Order Paper mkutano ujao wa Bunge! Badala ya kulalama na kutunga mashairi ya kejeli dhidi ya Sitta, Kubenea awahamasishe wananchi watumie Kanuni ya 34 kuleta maombi maalum (petition) kwa Spika ili kumjadili Lowassa na Richmond yake; awahamasishe Wabunge kutumia Kanuni za 54 na 64 kulirejesha suala hilo Bungeni!
Aidha, haimsaidii Kubenea au mwananchi yeyote yule kudai kuwa hakuna azimio lolote la Bunge lililotekelezwa ila moja tu la kufutwa kwa kampuni ya Richmond kwenye daftari la usajili. Hii ni hoja nzuri kwa kuuzia gazeti (maana Kubenea ameahidi kuendelea na makala yake toleo lijalo), lakini haina ukweli.
Kwa kifupi sana nadiriki kusema suala la Richmond limezalisha maamuzi mengi makubwa nchini ambayo utekelezaji wake hauwezi kukamilishwa kwa hatua moja bali kwa mchakato utakaochukua muda. Nitatoa mifano michache tu inayotokana na taarifa zinazopatikana kwenye tovuti ya Bunge la Tanzania.
Utekelezaji wa maazimio mawili ya kwanza kuhusu marekebisho ya Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2004, ulishaanza tokea mwaka 2008. Kubenea lazima aelewe kuwa utungaji au urekebishaji wa sheria haufanani hata kidogo na uchapaji wa gazeti la MwanaHalisi ambapo anaweza usiku moja tu akaandika habari za Sitta zenye upande moja na kuamua kuzichapisha asubuhi yake. Utungaji sheria ni mchakato mrefu wa kisheria unaoanzia Serikalini kupitia Baraza la Mawaziri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Baadaye hupelekwa kwenye Kamati husika za Bunge, Wadau mbalimbali na hatimaye kuishia Bungeni kujadiliwa na kupitishwa. Zaidi ya yote, sheria hiyo ya manunuzi ina vifungu 91 na vifungu vidogo zaidi ya 300 na majwedali matatu; ina Kanuni mbili zenye jumla ya vifungu 244, vifungu vidogo zaidi ya 500 na majedwali 13 yenye vifungu vidogo kemkem! Si kazi ya kupelekana joshi hiyo!
Maazimio ya tatu na nne yaliyotaka mikataba na makampuni ya kuzalisha umeme ipitiwe upya, hayakujadiliwa sawasawa na Kubenea pengine kutokana na kukosa taarifa sahihi. Mkataba kati ya TANESCO na Alstom Power Rentals ulikoma tarehe 19 Machi, 2008; ule kati ya TANESCO na AGGREKO ulikwisha Novemba, 2008 na wa Richmond/Dowans ulisitishwa tarehe 1 Agosti, 2008! Hivyo huwezi kuirekebisha mikataba hiyo, haipo!
Kilichoamuriwa na Serikali, tena kutokana na ushauri wa Kamati ya Nishati na Madini, ni kuandaa mikataba elekezi katika sekta ya nishati yaani Model Power Purchase Agreements (MPPA) ambayo itatumika katika majadiliano ya mikataba yote ya sekta ya umeme na wawekezaji. Serikali ililiabia Bunge katika Mkutano uliopita kuwa tayari kampuni ya Kimarekani ya International Consulting Corporation imepewa kazi hiyo ambayo itakamilika mwishoni mwa waka huu.
Kuhusu mkataba kati ya TANESCO na SONGAS, mchakato wa kupunguza mzigo wa malipo ulianza miaka miwili iliyopita. Matokeo yake ni kwamba kuanzia mwezi Septemba, 2009 malipo ya TANESCO kwa SONGAS yamepungua kutoka dola za kimarekani milioni 3.05 kwa mwezi hadi dola za kimarekani milioni 1.8 kwa mwezi! Haya si yangu, yako kwenye taarifa ya Serikali ya utekelezaji maazimio ya Bunge ya mkutano uliopita. Kwa kuwa uandishi wa Kitanzania ni wa “fault-finding”, haya yaliwapita wanahabari wetu!
Kuhusu IPTL, Kubenea anashindwa kuelewa kuwa upitiaji upya wa mkataba husika hauwezi kufanywa na upande moja tu bali pande zote mbili kwa kuketi pamoja kama ilivyokuwa kwa SONGAS. Utaendeshaje majadiliano ya maana wakati pande zote mbili ziko Baraza la Usuluhishi la London na Mahakama Kuu ya Tanzania ambapo tayari Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) ameteuliwa na Mahakama Kuu kuwa mfilisi wa muda wa IPTL?
Kutokana na utekelezaji wa Azimio la sita, wizara, idara za serikali na taasisi zake haziwezi tena kuingia michakato ya kimkataba na makampuni ya nje bila kuhusisha Balozi zetu. Kujiuzulu kwa Waziri Mkuu na mawaziri wengine wawili ambako kulifuatiwa na kuvunjwa kwa Baraza la Mawaziri, ni matukio yaliyotokana na maazimio ya Bunge ambayo, kwa bahati mbaya, Kubenea haoni uzito wake kisiasa wala kikatiba.
Mchakato wa sheria ya kutenganisha dhamana ya siasa na shughuli za kibiashara za viongozi wa umma, uko kwenye hatua mbalimbali za majadiliano kabla ya kuletwa Bungeni. Mchakato huu, ambao Kubenea hauoni, ni utekelezaji wa maazimio hayo ya Bunge!
Nimalizie kwa kuongelea maazimio mawili ambayo pengine yanamsumbua Kubenea kuelewa: azimio la kuwachukulia hatua watumishi wa umma waliohusika na mchakato wa Richmond na azimio la kumwajibisha Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU. Kwa uchambuzi wa kina, majibu ya Serikali yalibeba ujumbe wa kwamba watumishi wote wa Serikali hawakuwa na hatia kwa sababu walitumwa, na waliowatuma walishawajibika kwa kujiuzulu nyadhifa zao: Uwaziri Mkuu na Uwaziri! Hapa ndipo udadisi wa ziada unahitajika.
Kwa kuwa Serikali imekiri kwa kauli na vitendo kuwa makosa yalitendeka kwenye zabuni ya Richmond, na kwa kuwa (kama Mhe. Christopher Ole Sendeka alivyowahi kusema) haiwezekani kosa likatokea bila kuwepo mkosaji au wakosaji, ni nani sasa mkosaji katika sakata la Richmond ikiwa watumishi wote wa Serikali waliohusika hawana hatia? Jibu dhahiri ni kama nililolieleza hapo juu: Waziri Mkuu aliyepita Mhe. Edward Lowassa na Mawaziri wa Nishati na Madini kwa vipindi tofauti, Mhe. Dk. Ibrahim Msabaha na Mhe. Nazir Karamagi.
Aliyepigilia msumari tafsiri hii si mwingine bali Waziri Mkuu Mizengo Pinda alipokuwa anahitimisha hoja ya Richmond kwa upande wa Serikali tarehe 10 Januari, 2010. Alisema, namnukuu: “… uwajibikaji uliojitokeza kwa baadhi ya viongozi wetu akiwemo Mheshimiwa Edward Lowassa, Waziri Mkuu aliyestaafu sasa pamoja na Mawaziri wawili ndani ya Serikali ya Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, na mtikisiko wa kuvunja Baraza la Mawaziri uliofuata. Ni ishara tosha ya Serikali ambayo inakubali kuwajibika kwa Watanzania.
“Mheshimiwa Spika, katika mjadala liko swali limekuwa likijitokeza mara nyingi sana, Serikali mmejifunza nini, na mmejipanga namna gani ili mambo haya yasirudie tena. Kwanza ni watumishi wa umma kujaribu kuwa waadilifu sana katika utumishi wetu ndani ya Serikali kwa sababu suala la uadilifu ni kigezo muhimu, ndio kigezo kinachoweza kukutoa katika matatizo yoyote yale. Si hoja kwamba unajua sheria sana, si hoja kwamba wewe umesoma sana. Kama si mwadilifu, kama ni mtu ambaye wewe mwenyewe ni mpenda rushwa, mwizi, mbadhirifu wa mali ya umma, hivyo vyote ulivyonavyo havitakusaidia kulijenga Taifa hili hata kidogo. … Tujaribu sana kujiepusha na tama zinazoweza kuliingiza Taifa hili katika vitendo ambavyo vinaliingizia Taifa hasara kubwa…”.
Tunachoambiwa hapa na Waziri Mkuu ni kuwa sakata la Richmond lilitokana na ukosefu wa uadilifu miongoni mwa watumishi wa umma. Nani hao? Kwa kuwa Serikali yenyewe imewaondolea lawama watumishi wote wa Serikali walioshiriki kwenye mchakato wa zabuni ya umeme wa dharura, wenye tatizo la ukosefu wa uadilifu sasa ni wale viongozi watatu waliojiuzulu! Hivyo basi kujiuzulu kwao kusichukuliwe kama kujiuzulu kisiasa kwa makosa ya watendaji waliokuwa chini yao, ila ni kujiuzulu kwa makosa yao wenyewe! Kwa mantiki hii hawana budi kuchukuliwa hatua za ziada za kinidhamu au hatua za kijinai ikiwa ushahidi wa rushwa utaonekana. Huu ndo mkondo wa uchambuzi nilioutegemea kutoka kwenye vyombo vyetu vya habari na siyo kulalama tu na kutunga ngonjera za vijembe!
Matokeo ya uandishi uliokosa uchambuzi wa kina ni wanaharakati kupata taarifa za juu juu tu na hivyo kuamua kuandamana kulipinga Bunge, badala ya kujipanga upya kuileta hoja iliyokomaa zaidi mbele ya Bunge na mbele ya wapigakura mwaka huu!
Bunge lilishatamka kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU aliboronga, hivyo aondolewe! Baada ya kuona Serikali inalipiga chenga azimio hilo, Kamati ya Nishati na Madini ikaamua kumpa Mhe. Rais Kikwete kamba ile ile ambayo rafiki yake Lowassa alipewa mwezi Februari, 2008: JIPIME MWENYEWE! Kwa tafsiri yangu, Kamati ilibaini kuwa badala ya Mhe. Rais kumwajibisha mteule wake, yaani Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, amempa kichwa kikubwa kiasi cha kwamba amewageuzia Wabunge kibao na kuanza kuwachunguza kwa madai yasiyo na kichwa wala miguu: posho mbili, posho ambazo TAKUKURU yenyewe inatajwa kuwa mstari wa mbele kuwapa Wabunge! Huu si utawala wa sheria hata kidogo, ni vurumai!
Nakubaliana na Kamati kuamua kuliacha suala hilo mikononi mwa Rais mwenyewe! Akitaka asuke, akitaka anyoe, si uchaguzi unakuja? Rais atawaambia nini wapiga kura huku amembeba mgongoni Edward Hosea wa TAKUKURU? Hamu ya Kubenea ya kuwaona Wabunge waking’ang’ania utekelezaji wa azimio hili, haiendani na maadili na utamaduni tuliourithi wa kibunge wa Westminster. Mbunge hawezi kukifikisha Chama chake kikang’olewa madarakani!
Kamati ya Nishati na Madini, baada ya kuvutana na Serikali kwa muda mrefu kumwajibisha Edward Hosea, ilikuwa na njia mbili tu za kufanya: kumwambia Rais ajipime mwenyewe au kuomba kura ya kutokuwa na imani na Rais ipigwe! Lakini nani angeruhusu Wabunge wa Chama tawala wafike huko wakati wanafungwa na utaratibu wa kinidhamu wa kibunge wa three-line whip? Kazi ya Kubenea na wanaharakati wengine sasa ni kupiga kelele sana tubadilishe mfumo wetu wa Katiba ili mawaziri wasitokane na wabunge na utaratibu wa kumwajibisha Rais mwenye tabia ya ukaidi urahisishwe.
Hoja zangu zote kwa Kubenea, zinamfaa vilevile Asenga anayedhani kilichotokea Bungeni ni utaratibu walionao Wasomali wala-mirungi peke yao! Hapana, ni utaratibu wa nidhamu ya vyama ndani ya Bunge tuliourithi kwa Waingereza. Ndiyo sababu wapenda demokrasia nchini wanalilia uwepo wa wagombea binafsi ili kupunguza nguvu za vyama Bungeni dhidi ya maslahi mapana ya wananchi (wanachama na wasio wanachama wa vyama vya siasa). Ushauri wangu kwa Kubenea na Asenga: ubora wa MwanaHalisi utaimarishwa na nguvu ya hoja na si hoja za nguvu!

-mwisho-
 

Attachments

  • Mwanahalisi Rudini Kwenye Mstari3.doc
    60 KB · Views: 91
No siwaogopi naona kwa muda wa miezi nane sasa karibu kila post inasema mwanahalisi wajirekebishe,

sasa post yangu inaonyesha woga mkuu! unaweza kunifafanulia una maanisha nini?

Nilikuwa nakutani tu Mkuu Waberoya.Dont take it serious
 
Ijapokuwa mwanahalisi wanavitabia fulani vya kuandika habari ambazo itabidi ulize maswali mengi sana.Ila hii title nimeikubali

Wapambanaji wa CCM sawa na walevi wa mirungi wa Kisomali !

Unaweza ukaondoa neno mirungi ukaweka bangi!!

wapi Mwakyembe, Kilango, sijui nani...usikute watakaoenda kufanya kmapeni kyela ni Rostam na Lowassa , kwani wana aibu hawa???
 
Ijapokuwa mwanahalisi wanavitabia fulani vya kuandika habari ambazo itabidi ulize maswali mengi sana.Ila hii title nimeikubali

Wapambanaji wa CCM sawa na walevi wa mirungi wa Kisomali !

Unaweza ukaondoa neno mirungi ukaweka bangi!!

wapi Mwakyembe, Kilango, sijui nani...usikute watakaoenda kufanya kmapeni kyela ni Rostam na Lowassa , kwani wana aibu hawa???

Mkuu, let me be the devil's advocate for a while. Hivi kweli wote tunategemea msuli wa wapambanaji wanne au watano tu (akina Mwakyembe, Sitta, Kilango, Ole Sendeka, Selelii) katika Bunge la watu 320 na Watanzania milioni 40 ambao tumejiweka pembeni as spectators? Mchango wetu sisi wengine Watanzania uko wapi wakati akina Sitta wanapambana na kunyanyaswa kwa fedha chafu za akina Rostam? Contribution ya Doulton Kamauma imenifungua macho. Cheers!
 
Na MbashaAsenga

RAFIKI yangu mmoja raia wa Kenya alinisimulia siasa za Wasomali kwamba pamoja na kujitia vichwa maji, kuna kitu kimoja tu kinawafanya wawe na suluhu ya muda katika mapambano yao.

Alisema kwa kawaida wakati wababe wa vita wakiwa wanaendesha ubabe wao wakipambana kwa kutumia kila aina ya silaha, kuna wakati huweka chini silaha zao, wakati huo si mwingine isipokuwa ni wa kupokea shehena ya mirungi.

Huyu Asenga ana mijadala ya kitoto kwelikweli. Hivi ni nani anayefikiri ataamini kuwa Wasomali wanaolipuana na risasi wanaweza wakaacha kufanya hivyo kwa vile tu wamepata mirungi? Uandishi naona sasa unawashinda Mwanahalisi kwa sababu ya kuwa too biased.




Ulevi huu wa Wasomali unafanana na hamu ya kutaka madaraka kwa wale wanaoitwa wapambanaji na watuhumiwa wa ufisadi ndani ya CCM.
Hivi ni lini akina Mwankyembe wamekuwa mashoga na akina Lowassa, RA? Kwa nini Mwanahalisi wanataka kuwachafua hawa wapiganaji, au ni kwa vile wako CCM?

Akina Mwakyembe wanaweza wasiwe perfect, lakini kuwapakazia kuwa hawana nia ya kupambana na ufisadi ni kuvuka mipaka ya fitina.
 
Mwaka jana kajitokeza shujaa moja tu ndani ya CCM kwa jina Fred Mpendazoe na kweli hivi sasa kaungana na wapiganaji wa kweli kutetea maslahi ya taifa.

Je mshikamamo uliopo sasa ndani ya CCM kati ya waliojiita wapiganaji na wale waliojulikana kama vinara wa ufisadi, tuuelezeje ?

Tumeshuhudia wanavyokaa pamoja, wanavojadiliana pamoja na wanavyotoa maamuzi ya pamoja, hii hali yaashiria nini ?

Binafsi siamini kuwa kuna msafi hata moja ndani ya CCM lakini kama wapo nawaomba wana JF muwataje kwa majina na kwa nini mnaamini ni wasafi.
 
mag3, mwaka jana Mzee Mwanakijiji alilizungumzia hili kwa kina kwenye mada ya "Wapiganaji Walioko CCM, Wanapigania Nini?".
 
Watu hawa wana thibitisha usemi usemao "MGANGA HAJIGANGI" na Huwezi kumtukana mamba ukiwa ndani ya Maji.
 
Back
Top Bottom