Nebuchadneza
JF-Expert Member
- Oct 6, 2023
- 415
- 1,032
Habari wa ndugu wa tanzania??
Nimepitia site mbalimbali humu,ila site iliyonifanya kuwaza sana ni hii ya UJENZI,nimepitia nyuzi nyingi sana humu,yani kila niliyosoma imenifanya moyo kuuma kwa machungu sana na kuna kitu kipo kwenye koo kinanifanya machonzi kunilenga lenga kwa huzuni juu ya maisha yangu.
Sijaandika haya ilinipate comment nyingi au kuhave fun,lakini nimeandika nikiwa na uhalisia kwa kile nachokipitia katika maisha yangu.
Nina umri wa miaka 33,nina mke na watoto 2,mwanamke mwenyewe sijamuoa kwa ndoa wala nini,ni ile sogea tuishi,mwaka 2018 ndio niliyeamua kuishi naye sasa toka kipindi hicho maisha kwangu yamekua magumu sana.
Mimi mzaliwa wa ARUSHA,nilikuja dar 2016 baada ya kusota chuga kutafuta kazi bila mafanikio,maana nilihitimu chuo 2015 na toka kipindi hicho nimesota kutafuta kazi bila mafanikio yoyote.
Niliamua kuja Dar kutafuta maisha baada ya kuchoka kuishi home na kula ugali wa shikamoo ndio nikaja Dar 2016,baada ya kuja Dar nilifikia maeneo ya ubungo kibangu nakumbuka nilikua na 300000 niliyopata kwa kazi ya kuchimba msingi na saidia fundi,mpaka kuikusanya hiyo pesa nilisota asikuambie mtu,kuchimba mashimo ya vyoo na kujaza vifusi kwenye nyumba za watu.
Baada ya kufika ubungo kibangu,nilifikia kwa brother kipindi hicho kaka alikua na duka la bidhaa za nyumbani,ila duka hilo lilikua lishaanza kufilisika maana alikuwa na kesi na mwanamke mmoja aliyezaa naye mtoto alimsingizia amemfira kipindi akiwa mjamzito.
Basi brother akawa ashindi dukan kila siku akawa anaenda mahakamani mpaka duka likafilisika na kujikuta Anarudi Bush KILIMANJARO,ndio kipindi hicho ndo nilikua nimefika Dar,nilikua nasiku 3 tu kufika Dar na mwenyeji wangu anaamua kurudi bush.
Nikiwa na 300000 nilitafuta chumba maeneo ya kibangu nikapata chumba cha 35000 mwenye nyumba alitaka kodi ya miezi 6 nilimbeleza sana nimpe kodi ya miezi 3 aligoma katu katu basi nikampa 210000,kwenye ile 300000 nikabaki na 90000 kutoa pesa ya Dalali 35000 nikabaki na 55000,nikakabidhiwa ufunguo wa chumba nikiwa sina chochote zaidi ya begi langu.
Basi ile 55000 nikaenda pale darajani, ubungo nikauziwa godoro la futi 4 ulimi kwa 25000 nikanunua maji ya kunywa, carton 1 kwa 3000,mapazia 2 ya 8000 kwa 16000 mpaka hapo nkawa nimetumia 44000 kwenye ile 55000 nikabakiwa na 11000.
Siwenzi kuandika yote hapa mambo ni mengi sana
Nimepitia site mbalimbali humu,ila site iliyonifanya kuwaza sana ni hii ya UJENZI,nimepitia nyuzi nyingi sana humu,yani kila niliyosoma imenifanya moyo kuuma kwa machungu sana na kuna kitu kipo kwenye koo kinanifanya machonzi kunilenga lenga kwa huzuni juu ya maisha yangu.
Sijaandika haya ilinipate comment nyingi au kuhave fun,lakini nimeandika nikiwa na uhalisia kwa kile nachokipitia katika maisha yangu.
Nina umri wa miaka 33,nina mke na watoto 2,mwanamke mwenyewe sijamuoa kwa ndoa wala nini,ni ile sogea tuishi,mwaka 2018 ndio niliyeamua kuishi naye sasa toka kipindi hicho maisha kwangu yamekua magumu sana.
Mimi mzaliwa wa ARUSHA,nilikuja dar 2016 baada ya kusota chuga kutafuta kazi bila mafanikio,maana nilihitimu chuo 2015 na toka kipindi hicho nimesota kutafuta kazi bila mafanikio yoyote.
Niliamua kuja Dar kutafuta maisha baada ya kuchoka kuishi home na kula ugali wa shikamoo ndio nikaja Dar 2016,baada ya kuja Dar nilifikia maeneo ya ubungo kibangu nakumbuka nilikua na 300000 niliyopata kwa kazi ya kuchimba msingi na saidia fundi,mpaka kuikusanya hiyo pesa nilisota asikuambie mtu,kuchimba mashimo ya vyoo na kujaza vifusi kwenye nyumba za watu.
Baada ya kufika ubungo kibangu,nilifikia kwa brother kipindi hicho kaka alikua na duka la bidhaa za nyumbani,ila duka hilo lilikua lishaanza kufilisika maana alikuwa na kesi na mwanamke mmoja aliyezaa naye mtoto alimsingizia amemfira kipindi akiwa mjamzito.
Basi brother akawa ashindi dukan kila siku akawa anaenda mahakamani mpaka duka likafilisika na kujikuta Anarudi Bush KILIMANJARO,ndio kipindi hicho ndo nilikua nimefika Dar,nilikua nasiku 3 tu kufika Dar na mwenyeji wangu anaamua kurudi bush.
Nikiwa na 300000 nilitafuta chumba maeneo ya kibangu nikapata chumba cha 35000 mwenye nyumba alitaka kodi ya miezi 6 nilimbeleza sana nimpe kodi ya miezi 3 aligoma katu katu basi nikampa 210000,kwenye ile 300000 nikabaki na 90000 kutoa pesa ya Dalali 35000 nikabaki na 55000,nikakabidhiwa ufunguo wa chumba nikiwa sina chochote zaidi ya begi langu.
Basi ile 55000 nikaenda pale darajani, ubungo nikauziwa godoro la futi 4 ulimi kwa 25000 nikanunua maji ya kunywa, carton 1 kwa 3000,mapazia 2 ya 8000 kwa 16000 mpaka hapo nkawa nimetumia 44000 kwenye ile 55000 nikabakiwa na 11000.
Siwenzi kuandika yote hapa mambo ni mengi sana