Ninawaomba na tena nina wasihi kutoka ndani ya moyo wangu, msifungue sanduku hili la kujadili mambo ya chumbani ya viongozi au madhaifu ya kibinadamu ya viongozi wetu endapo mambo hayo hayahusiani moja kwa moja na nafasi zao, pesa za walipa kodi au maslahi yoyote yale ya kitaifa. Na msilazimishe kuwa kiongozi akienda msalani basi hilo ni jambo la kitaifa na mnataka details zake, kisa tu alionekana akienda msalani kwa jirani yake! Kipimo ambacho mnataka kukitumia kwa Zitto kikikubalika siyo kwamba kitaonesha umakini wa forum hii bali kutaishusha hadhi yake kuliko tunavyofikiria. Nawahakikishia kama mnafikiri mambo yanayojulikana ni ya Zitto peke yake fikirini tena. Wenye data za viongozi au wanaotaka kujua mambo ya viongozi siyo nyinyi peke yenu! Kuna watu wanajua viongozi wanaposafiri huja na kina nani, wanakaa wapi, na kina nani wanakutana nao. Tukikubali kuwa Zitto LAZIMA azungumze hapa (licha ya kuwa tayari amezungumza) na akiri (licha ya kuwa ameshakanusha) kuwa amefanya kitendo fulani (ambacho tayari amesema hakufanya) basi siyo kwamba tunataka kutenda haki bali kufurahisha tu udadisi wetu wa kibinadamu. Nawasihi tena, kama kweli ninyi mnaitetea forum hii, basi heshimuni mambo ya binafsi ya viongozi na hilo litumiwe kwa viongozi wote.
Hata hivyo endapo mambo yale ya binafsi yanahusiana na nafasi, vyeo, au yanaweza kuwa ni matendo ya kihalifu (criminal acts) basi hilo halina mjadala kwani hakuna mtu yeyote aliyejuu ya bodi au juu ya wanachama. Wote wako chini ya ukweli, ukweli mtupu, na si kingine bali ukweli.