Ni bora mtu asikusamehe ujue moja kuliko mtu akusamehe halafu akabaki na kinyongo. Nina uncle wangu mmoja alioa, changamoto kubwa kwenye ndoa yake mke wake alikua na wivu kupindukia, ilifika hatua akaanza hadi kumnyima tendo la ndoa. Uncle wangu alivumilia alijitahidi kuwatafuta ndugu wa mwanamke wafanye vikao wamalize changamoto yao lakini mke akawa hatoi ushirikiano, mwisho wa siku kwa kua nae ana hisia akatafuta mchepuko huko nje ili awe anajiliwaza + kitimiza haja zake.. Yule mke wake alipozipata taarifa ndio akajirudi, akajidai amebadilika kweli, waka solve matatizo yao wakaendelea kuishi pamoja kama awali. Kumbe yule mke wake ana kisasi kakiweka moyoni, siku moja wamelala usiku uncle wangu akasikia mtu ameamka, lakini akajidai bado amelala, kumbe yule mke wake ameenda jikoni kuchukua kisu ili aje amchome nacho, bahati nzuri alimuwahi. Mwisho wa siku kila mtu ana maisha yake, wanavyoishi hata haijulikani kama wameachana ama vipi, ila uncle amemuachia nyumba huyo mke wake maana wana watoto wawili, yeye kaenda zake kupanga.
Sasa kwa situation kama hizi si bora mtu kujiondokea tu mapema ili kuepusha madhara makubwa zaidi. Kuna mdau mmoja huko juu kaongea point kubwa sana, kama hauna uwezo wa kusamehe ni bora uachane na mhusika maisha mengine yaendelee.