Ukiongea na mama yako dada yako shangazi yako na shoga zako hutapata majibu sahihi
Tafuta muda ongea na baba yako mchungaji au shehe wako kaka zako wajomba zako boss wako na wanaumee wengine swali waulizee moja tu JE WALISHAWAI KUCHEPUKA TOKA WAMEOA
Jibu la kweli ni ndiyo hapo jibu ni kuwa mumeo ni mwanaumee kamili ameungana na kundi la wanaume wenzake lingine ni je anakuheshimu kama zamani jibu ni ndio jiamini wenzako kuanzia mama yako walikubali na kuvumilia yakapita SASA WW JIFANYE MWANAMKEE SHUJAA ONDOKAA UONEE HASARA YAKE NA KWA WANAO
Barikiwa kwa ushauri mzuri maana wanawake wengi wanadhani kutunisha misuli ndiyo solution kumbe wanaharibu zaidi tena kwa kiwango cha kutisha na matokeo ya hasira yanaharibu zaidi ndoa na maisha kwa ujumla wake.Kisasi hakisaidii bali kinaharibu zaidi nyumba ambayo ingedumu kama kujipa moyo kungezingatiwa.
Kila mwanamke ajiulize swali hili , wale wanawake walionenwa katika Biblia walipigania kuwa na wanaume nje ya ndoa au kuolewa na wanaume wawili? Kama hawakupigania hayo mbona waume zao walikuwa na wanawake zaidi ya mmoja na maisha yakasonga vema tu?
Shida ni kwamba dunia ya leo wanawake wanapenda kuaminishana vitu visivyowasaidia , badala ya kuwatii waume zao leo wanapambana kuwapenda kwa kuwaletea maua , yaani mwanamke anajua unapenda kula wali na unamsisitiza apike ule anapika ugali kisa anapenda ugali.Mwingine eti akitoka nyumbani anajipodoa hadi mwisho ila akiwa nyumbani hana tofauti na mpiga debe wa zama zile.Mwingine anabeba maua kumletea mmewe kuonesha anampenda ila mmewe akimwambia aache jambo fulani au afanye jambo fulani hafanyi.Kiukweli kama mwanamke akimudu majukumu yake hasa ya utii basi ni wazi ndoa nyingi zitapona na wanaume wengi watakuwa watulivu tu.
Siku hizi kuna tatizo jingine na hilo ndilo huwa nawashauri wanawake msilipe kipaumbele japo ndilo mnalifanya mno , kumnyima tendo la ndoa mwanamme yaani hiyo ni balaa zaidi maana kiukweli wanaume ni dhaifu mno katika tendo hilo na si rahisi wakamudu kulikosa kwa muda mrefu yaani chukia ,zira nk ila ukifika mida ya usiku kuwa free kutumika la sivyo hii michezo ya nje itaibuka tu hata kama mmeo ni Mchungaji maarufu kuliko wote anaweza kuanguka tu.Na nadhani huwa mnalifanya hili bila kutafakari , kama unamnyima tendo ambalo kwake ni muhimu unategemea akalipate wapi?Maandiko yenyewe yalishauri katika hili tendo tusinyimane
[emoji116]
3 Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.
1 Wakorintho 7:3
4 Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.
1 Wakorintho 7:4
5 Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.
1 Wakorintho 7:5
Na pia wanawake makini hampaswi kamwe kuishi kwa kuwasikiliza waliofeli kwa kisingizio cha urafiki kamwe usifuate mawazo ya watu walioshindwa maana watakufelisha tu maana wakati wanaume hushauriana mambo ya msingi zaidi katika maisha , wanawake hushauriana zaidi mambo ya kuwaangusha japo katika maneno yao hudhani yanawaimarisha sana kwa kuwa huwa na wingi wa maneno kumbe yanawaingiza shimoni.Simameni kumtii Mungu wanawake maana ninyi ndiyo walinzi wa nyumba ,bila ninyi future ya familia ni kudra za Mungu tu