Ni kwa sababu husomi Biblia vizuri , mtu makini anaishi kwa kutazama mambo ya wengine yawe mazuri (kujifikiria wewe tu ni ishara kuwa huna upendo wa kweli popote) soma hapa Yesu alivyokuchukua uamuzi wa wokovu wako hadi kufa msalabani
[emoji116]
3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.
Wafilipi 2:3
4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.
Wafilipi 2:4
5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
Wafilipi 2:5
6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;
Wafilipi 2:6
7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;
Wafilipi 2:7
8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.
Wafilipi 2:8
Ukijaa chuki na husuda kisa umekosewa jiulize kama umefikia nusu tu ya kile kilichompata Yesu kwa ajili yako.Angeamua kubaki zake mbinguni asingepungukiwa chochote kwa hivyo kama unawapenda wanao huwezi kushangilia kuachana