Wanawake wenzangu mnawezaje kumsamehe a cheating husband?

Wanawake wenzangu mnawezaje kumsamehe a cheating husband?

Ni muhimu kupima na uzito wa jambo sio kwa sababu tu linakufurahisha moyo wako ndio ulifanye, kuna side effects baada ya kukufurahisha ndio maana inakuwa ni kwa siri sana na siri ikifichuka unaomba samahani. Ila bado nakazia ushauri uliompa mleta mada haufai kutumika.


Kibomba kipo kwa niaba ya mume



Tatzo lenu baadhi ya wanawake mkichepuka mnazama jumla mnasahau mpaka njia kuu.
Sasa mbona mume wa mleta mada alifanya Ina maana hakupma, jamani furaha yangu muhimu, lazima na Mimi nitafte kitu kizuri kuliko wewe kinipatie Toto moja matata sana, hapo nakusamehe hata ukichepuka daily sijali maana na Mimi nimefanya Jambo nililolifanya kutimiza matakwa yangu.
NB usifanye Hili Jambo Kama una roho nyepesi na dhaifu na hujajiandaa kukabiliana na Hali hyo. Uwe tayari ku move on oooh
 
Yani majaribu tunayopitia huwa tunawahurumia tu basi, Sasa tukiwa kimya Wana jimwambafai mwambafai humu
Hahahahh nawacheka kwa dharau tu,, adhabu zetu ni konki wanazijua hata wakijisahaulisha
 
Wanawake tunaweza Ila lazima ulipie gharama za mwanao hyo haihusiki na ninayo fanya. Child support muhimu maana na Mimi Nina maisha yangu and I must contribute kwa watoto. Ndio tumeachana hyo haihusiki na kutotoa matunzo ya watoto wako
Njaa tu. Huna uweo wa kutunza watoto. Huna la kuwafundisha. Unataka ubaki nao ili uwe unakula hela zangu. Kama watoto watakaa kwako jua ya kwamba utalea, kama watakaa kwangu basi ntalea. Juzi tu kuna rafiki yangu katoka kushinda kesi kama hii now yupo na mwanae na bidada hajaambulia hata senti na uzuri hata mgawanyo wa mali kulikuwa hakuna katoka kama alivyokuja
 
Umesema umeachika mara saba sasa mbona hukukomaa ubaki kwenye ndoa na ukaendeleza michepuko pembeni?Unamshauri mwenzio abaki kwe ndoa ila awe na kidumu cha kumfariji ili hali we mwenyew tu ulishindwa na ukaachika mpaka mara saba,Rejea post zako huko juu,
Nimemjibu huyo nyumbu kwa kuandika utopolo wake hapo Mimi sijawahi anzisha mada hyo yeye badala ya kujibu hoja akatoka nje ya hoja. So nimemjibu alichotaka kusikia
 
Mkuu nakuhakikishia ikitokea umeoa Au ikiwa tayari una mke utakapo msaliti na amekukamata pasipo shaka

Amini atarudisha hiyo punch hawasamehi na wao ni binadamu tena usiombee yeye awe hajawahi kukusaliti

Hii kitu nakumbuka baba yangu alimwambia mdogo wake baada ya kufumaniwa na mkewe ana cheat. Alimwambia huwa hawasamehi usijidanganye na ni kweli yule mama anachokifanya mpk leo ni balaa heri wangeachana tu. Maana ishapita miaka 20 ila mke ana revenge taratibu
 
Eti talaka, huo ni uzembe. Pata kipoozeo cha kulindia ndoa yako.
Hivi zile nyimbo sijui pambio zinaimbwa bila mpangilio kumbe zina maana kubwa eee [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
Ngoja nimshtue jirani yangu
 
Mwenzenu yamenikuta na kusema za ukweli nashindwa kabisa kuelewa namna ya kutoka hapa na kusonga mbele.

Ni mume nilompenda sana sana sana. Mungu katujaalia two beautifull kids na mengine ambayo am greatfull for. Tuliishi kwa upendo,furaha na amani hadi miezi 8 ilopita nilipogundua kuwa nilivyomdhania mume wangu sivyo alivyo.

Kwakuwa nampenda na kumfahamu sana mume wangu, kuna kitu nilikuwa tu nakihisi hakiko sawa kwa muda. Baadae nikagundua he was cheating. Yaani sitaki kuelezea mstuko niloupata na jinsi ninaumia jamani. Japo aliomba sana msamaha and all that ila moyo wangu umekufa ganzi wapendwa.

Mume nilompenda sana kwasasa namuona kama jirani yangu tu, hata hamu nae sina kabisa na hata tendo la ndoa ni kama ananibaka tu. Tushaongea sana, tushakwenda hadi vacation sie wawili tu ila sioni kinachobadilika. Akisafiri kikazi au mimi nikisafiri najisikia amani zaidi and i dont miss him kabisa.

Kuna wakati nilimuomba some alone time nifikirie kuhusu mustakabali wa hii ndoa, alinipa huo muda na kwa kipindi hicho cha wiki moja kichwani mwangu nilishangaa kunazunguka watoto wetu tu na sio mume wangu. Sijamueleza mtu yeyote kuhusu hili hata mama yangu wala mshenga wetu ila linanitafuna hatari.

Wenzangu mnawezaje kusamehe wanaume wanaowacheat na kurudi katika hali zenu za kawaida? Maana mie kwasasa mume wangu namuonaje sijui, nae naona hali hii inamtesa ila ndio hivyo tena
emoji134.png

Sijisikii kumpenda wala kumheshimu tena, naona kama hadeserve kwa kutokuithamini na kuivuruga ndoa yetu.

Pole sana nyakoo .Hiyo ni misukosuko ya kwenye ndoa,sababu ndoa huwa ni safari isiyokosa misukosuko.kama lisinge tokea hili lingekuwepo lingine ,pengine baya zaidi.Sasa namna ya kuitatua inahitajika kuachia hata baadhi ya haki zako za msingi kwa manufaa yako mwemyewe na familia yako.kitu kingine unatakiwa kuelewa ni kuwa amecheat siyo kwa kupenda,hata yeye trust me anajuta sana kwa alichokifanya .Pia nikuhakikishie kwamba huyo jamaa bado anakupenda sana na anaijali ndoa yake.sababu ingekuwa hakupendi angekujibu kunya kunya na kuendeleea kukwambia usimpande kichwani shika time yako.Sababu wewe mwenyewe unajua,hakuna kinachomtisha kwako.Huyo bado ni muelewa na mume sahihi.kilichotokea ni kama ajali tuu.Cha msingi kwa sasa msaidie ili hiyo dhambi asiirudie tena.Kama ni watu wa ibada endeleeni kumsihi Mungu aendelee kuilinda ndoa yenu.Yamkini naye amekuweka kwenye matazamio usipobadilika ,huenda akaacha kuvumilia ,kiasi hali ikaharika zaidi,shetani atampa mbuni mpya ya kuivurugha ndoa yenu mazima.
kitu usichohitaji kujaribu kufanya ni kutafuta faraja kutoka kwa mwanadamu mwingine kama namna ya kulipa kisasi.

Hivi ninavyoandika uzi huu yule mwanamke aliyecheat naye anajiuliza mbona mchepuko wake amebadilika ghafla,amekuwa kimya sana,hapokei sinu zake tena,anaendelea kumfuatilia kujua kulikoni.So sababu umeamua kutokuwa na ukaribu wa faraja na mumeo basi unamfanya huyo mke mwenzio apate unafuu zaidi.

Kuna wakati wanaume wanakuwa kama watoto wanataka atention kubwa kutoka kwa wake zao.

Lastly,fanya r
 
[emoji23][emoji23][emoji23]eti akutane na mkunyenge wa uchumi wakati[emoji23][emoji23][emoji23]. Mkunyenge wa uchumi wakati vepee
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] dea weee acha tyuuuh, usaliti unaumiza mnooh. Ni kulipiza kisasi kwa sanaaah
 
Siku mwanamke atakapoamua kujutegemea na kuacha kumfanya mwanaume kama kitega uchumi..yaan yupo kwenye ndoa kwa mahitaj ya ndoa..ndipo atakua huru kufanya maamuz

Weng wanashindwa fanya maamuz sbaab anajua.dah ..niache nyumba hii.niache magar haya.niache ubwabwa wa bure huu..haiwezekan.ntakomaa nae hapa hapa

Hapo ndipo mnatupa jeur ya sis kucheat na kutoogopa kufanya hvyo sbaab tunajua huwez fanya chochote zaid ya kunilaum.kununa.kutukana..etc
Wewe umeandika kweli wanawake ndo eti wanaume wote sawa, uoga wa maisha wanateseka na kuogopa kuchekwa, Mimi nikichefukwa sirudi nyuma Bora nianze from zero kabisa hata ukiwa bilionea siwezi vumilia
Ndio maana nawashauri wanawake wenzangu hizo nguvu zakufuraisha wanaume, eti wasi cheat, wapendwe watumie kufanya maendeleo yao binafsi na ulifanya hivo unakuwa na uhakika wa maisha na furaha yako na watoto wako. Hii kujiliza Liza na kuendekeza maumivu, Sasa utaishi lini kwa furaha life expectancy yenyewe ya mtanzania ni 45 years
 
For better or for worse,

Ur pain is valid
Jipe muda
Kamuone mtaalamu/marriage counsellor/therapist ukihisi unashidwa kuvuka na inaathiri sana maisha yako ya kila siku,watoto na ndoa yenyewe
Huku unakomuelekeza ndo ataenda fanywa
 
Njaa tu. Huna uweo wa kutunza watoto. Huna la kuwafundisha. Unataka ubaki nao ili uwe unakula hela zangu. Kama watoto watakaa kwako jua ya kwamba utalea, kama watakaa kwangu basi ntalea. Juzi tu kuna rafiki yangu katoka kushinda kesi kama hii now yupo na mwanae na bidada hajaambulia hata senti na uzuri hata mgawanyo wa mali kulikuwa hakuna katoka kama alivyokuja
Wewe utalea kwa lazima Tena ikiwezekana kwa Sheria hutaki na watoto unapotezwa haki zote za watoto kuanzia ubini na kila kitu ukafie mbele ya safari Tena nawaambia watoto a to z hutaki kulea means umekana wanao natafta lawyer u sign ulivokataa kuhudumia watoto wako ili wakikua ni waonyeshe kabisa
 
Ndiyo maana naenjoy kuwa single, hakuna kitu sipendi kama kupewa stress na binadamu mwenzangu tena ambaye najua anafanya makusudi kabisa bora stress za upweke kuliko za mapenzi.
Unakosa mema ya duniani Anko,usiziogope changamoto pambana nazo.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] dea weee acha tyuuuh, usaliti unaumiza mnooh. Ni kulipiza kisasi kwa sanaaah
Kuna vitu havisameheki kabisa zaidi tu ya kusahau, ujue ukikumbuka wasikia kinyaa, Bora tu kulipiza bana ukute Kuna ntu anakubembelezzaga mda anakujali kwanini ujitese eti na mume kah
 
Back
Top Bottom