Wanawake tujikumbushie vituko vya leba

Wanawake tujikumbushie vituko vya leba

Mimi mwenyewe zamani nilikuwa naenenda hivyo lakini nikapata Neema nikajifunza na kufahamu kuwa kudeka deka kipindi cha ujauzito na wakati wa kujifungua siyo sahihi kabisa, ni mapokeo tuliyoyasikia toka Kwa watu mbalimbali
 
Mama sabrina looo pole shogangu yani ulivyoelezea yote yalinikuta mimi, mtoto alisukumwa na manesi watatu huku dokta naye anavuta jamani wanaume wangejuaga kwa kweli wasingeletaga dharau, acha mama aitwe mama, toka nitoke leba aisee nimekuwa mgumu balaa hata nipitie kitu gani sijui kama maumivu yake yatafikia ule uchungu.

Shikamoooni wamama jamn
Umekuwa mgumu kutoa papuchi
 
Mwingine eti unakuta akipata ujauzito haishi nongwa!
Nakwambia mara anachukia watu, wengine anamchukia mumewe jamani
Na tabia ya kula maudongo, mikaa, sabuni, unga n.k yote hayo ni mapokeo!
 
Kuna siku nilipita karibu na labor pale General hospital Dodoma nilisikia ukunga mkali hadi nilisimama kuuliza ndio nikajua nimepita karibu na labor, niliishia kumuonea huruma tu

Na kingine kilichonishtua ni jamaa angu mkunga aliniambia wakati wa kujifungua kama njia ni haijafunguka vzr wanaiongeza kwa kuchana na kisu bila hata ganzi, duh hapo palinishtua
 
Jamani jamani jamani kila nikiingia leba naanza na neno nitatoka salama humu? Huwa nakata tamaa kabisaaa hasa maumivu ya mgongo na kiuno yakichachamaaa euwiiiììii huwa naomba msaada hata wa mtu asiehusika. Sitakaa nisahau mwanangu wa kwanza niliteseka uchungu siku 2 mpka muda wa ku push nguvu sina ikabidi wamvute mtoto kwa vacuum thanks God nilikua kwa hospital yenye specialist mtoto hakupata madhara. Uchungu wa kuzaa hakuna mfanowe ndipo wamama wengi hufariki kwa sbb kuna wengine presha zinapanda au kushuka ghafla kwa maumivu. Wababa kule ni nusu kifo muwe mnatuombea tutoke salama
Mwili umesisimka
 
Wengine ni Kweli inaweza kutokea uchungu ukachukua muda mrefu na hali tofauti huwa zinaweza kujitokeza Kabla ya kujifungua!
Lakini pia kuna wale videko ambao hawataki kuzingatia maelekezo ya mkunga
Akiambiwa lala Hivi au fanya vile hataki kazi Yake ni kujiliza na kufanya vioja tu !
Kutamka maneno yasiyompa Mungu utukufu!
Mwenyezi Mungu azidi kutusaidia siku zote !
 
Tunahitaji mafundisho zaidi lakini siyo sehemu Za wazi Kama hizi ambako wanaume wanatusoma na watoto pia!
Kila ktk maisha kinahitajika mafundisho iki kiweze kufanyika Kwa usahihi !
Hichi kitu kinafundishwa mpk shule kwenye level ya juu kwa waliochukua pcb sasa na darasani tunakuwepo wavulana na wasichana. Haya mambo yanatuhusu wake kwa waume maana hata leba mara nyingine wanazalisha wanaume. And kama sikosei humu hakuna under 18.
 
Tunahitaji mafundisho zaidi lakini siyo sehemu Za wazi Kama hizi ambako wanaume wanatusoma na watoto pia!
Kila ktk maisha kinahitajika mafundisho iki kiweze kufanyika Kwa usahihi !
Sidhani kama kuna kitu kigeni chochote duniani, uchungu na leba ni mambo ya kawaida kabisa uliza wanaosomea udaktari, kwa dunia ya leo iliyoendelea watu watakushangaa kusema jambo kama hilo, ukiingia YouTube kunazo hadi video ya kuzaa.... Sasa sielewi unazungumzia siri katika muktaza gani
 
Hichi kitu kinafundishwa mpk shule kwenye level ya juu kwa waliochukua pcb sasa na darasani tunakuwepo wavulana na wasichana. Haya mambo yanatuhusu wake kwa waume maana hata leba mara nyingine wanazalisha wanaume. And kama sikosei humu hakuna under 18.
Bora hata na wewe umeona hili, yani wanaotupatia hizo mimba ni wanaume sasa kwa nini tufanye siri uchungu yani tusiwahusishe wajue yanayotukabili hadi maandiko matakatifu yamezungumzia uchungu yaani sioni siri kwa kweli
 
Maumivu ya kisu cha ngariba tena bila ganzi ni hatar aisee!! Bora ningebak na govi langu
Haaa haaa govi? Like serious?..hizo kejeli ambazo ungezipata kwetu, ungejipeleka mwenyewe kukatwa huo mkono wa sweta!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom