Wanawake tujikumbushie vituko vya leba

Wanawake tujikumbushie vituko vya leba

Pamoja na yote mnayoyasema uchungu sijui maumivu mwisho wa siku unakuta mwanamke anasema ohoo nina hamu na mtoto mchango. Ukweli kama wanaume tungekua tunaenda jando mara mbili ningefikiria sana kurudi Jando. Sio jando la hospital hili la kwetu huku Mara.
 
Mwanamke uliyefundwa huwezi kusema haya mambo hadharani

Ni eidha ulizaa ukiwa mwanafunzi/mwanachuo au umekuwa mama kabla ya wakati wako.

Vinavyofanyika/kutokea leba ni siri, kuvimwaga hadharani hapa ni kujivua nguo. Ndio maana hata manesi/wakunga hawavitoi nje.
 
Pamoja na yote mnayoyasema uchungu sijui maumivu mwisho wa siku unakuta mwanamke anasema ohoo nina hamu na mtoto mchango. Ukweli kama wanaume tungekua tunaenda jando mara mbili ningefikiria sana kurudi Jando. Sio jando la hospital hili la kwetu huku Mara.
Kubalini basi tuzae mmoja tu, nyie si ndo mnapendaga timu ya football?
 
Uchungu wa pilipili au ndimu au kidonda au vp nyie c amfanyag kazi kaz ndo hiyo acha wanaume tupige kaz nakula bata nyie tafunen na kujaza dunia
 
Jamani jamani jamani kila nikiingia leba naanza na neno nitatoka salama humu? Huwa nakata tamaa kabisaaa hasa maumivu ya mgongo na kiuno yakichachamaaa euwiiiììii huwa naomba msaada hata wa mtu asiehusika.

Sitakaa nisahau mwanangu wa kwanza niliteseka uchungu siku 2 mpka muda wa ku push nguvu sina ikabidi wamvute mtoto kwa vacuum thanks God nilikua kwa hospital yenye specialist mtoto hakupata madhara.

Uchungu wa kuzaa hakuna mfanowe ndipo wamama wengi hufariki kwa sbb kuna wengine presha zinapanda au kushuka ghafla kwa maumivu. Wababa kule ni nusu kifo muwe mnatuombea tutoke salama
 
Nakuambia shogaa siku mbili nikiona mwakaa
Ila mtoto akitoka tu maumivu yanaisha,,nesi akawa ananiona nahangaika mara natandika pale maana mvua ilikuwa inanyaesha nasikia baridi huku natokwa jasho hapo hapo
Kuna muda nilitamani wamvute wamtoe ili nipone
Nilizabwa makofi ya mapaja nikawaambia pigeni tu sisikiii maumivu,,niliwasumbua

Kuja kunyonyesha napo chuchu zinatoka vidonda mtoto akinyonya yaan zinachubuka ,,ulikuwa ukifika muda wa kunyonyesha nalia kwanza maana namdolishia mtoto nyonyo mpaka anazila kunyonya
Hiki kipindi sitaki kabisa,ntazaa wa pili lakin baadae
Bado unataka kuzaa tena,umeyamiss maumivu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom