Kimsingi heshima ni kiunganishi kikubwa sana baina ya wanyama, binadamu wote hata kazini, barabarni, kwenye familia, bus n.k. Panapoishi watu zaidi ya wawili yawapasa kuheshimiana.
Tunamfundisha mwanamke heshima tunamuacha mwanaume kwenye mafundisho haya tunakosea. Mwisho tutakuwa na familia zenye mama mwenye heshima ila baba ni mkiritimba, hashauriki, anafanya lolote na haulizwi, anasaliti ndoa ila anapaswa aulizwe kwa unyenyekevu wakati kaumiza mwenzake.
Madhara yake ni kuzalisha vizazi vya wanawake wenye visasi kulipiza kulingana na maumivu waliyoyapitia muda mrefu.
Kina baba, kina mama, watoto hebu tuyeyushe mioyo yetu! Tujaliane, tuombane radhi tunapokoseana, tusichepuke, tusiwe na masiri mazito mazito yakuangamiza familia.
N:B. Familia lazima iwe na kiongozi mmoja ambaye anatambulika ambaye atatoa kauli ya mwisho baada ya kusikiliza kwa makini maoni ya mwezake.