Wanaume wanaotoka nje ya ndoa

Wanaume wanaotoka nje ya ndoa

Siyo mimi hommiii Kaizer, ni Yesu ndo alisema mwenye nacho ataongezewa na asiye nacho hata kile kidogo alicho nacho atanyang'anywa.

Baada ya kusema hayo, hebu niache nimalizane na PASion Lady kwanza
 
Last edited by a moderator:
let me log out
mtajijuuuuuu!!
mbona ghafla umekuwa mkali kupita ndimi za moto! hebu tulizana bana, sie tunakusuport kabisaaaaa in each every step u take!
 
mbona ghafla umekuwa mkali kupita ndimi za moto! hebu tulizana bana, sie tunakusuport kabisaaaaa in each every step u take!

step gani?tena
aaaa naona vurugavuruga style imerudi
 
Mume wa mtu ni thumu vivyo hivyo na mke wa mtu ni thumu. Lkn inasikitisha sana wanaume wanaotoka nje ya ndoa wakati mwingine hawana hata sababu ya kufanya hivi . Kuna wanawake wanatimiza wajibu wao vizuri sana kwa waume zao lkn bado mume huyo atatoka tu nje. Tena basi na huko nje anakokwenda wengine wanateswa sana na nyumba ndogo hata kupelekea kufanyishwa kazi kama watumwa. Nyumbani mwanaume huyo haoshi vyombo wala kufua nguo lkn akienda huko kwenye nyumba ndogo anafanya kazi zote na wala hakuna hayo sijui maneno mazuri au nini. Kwa upande mwingine kuna wanawake wanatoka nje ya ndoa huwezi kuamini walahi . Kuna kitu bado kinanishangaza juu ya baadhi ya wamama,nao hawana sababu za msingi zinazowafanya watoke nje . Pia nami nawapa hongera wanandoa waliodumu ktk uaminifu . Tubadiike tumche Mungu ridhika na ulie nae kama kuna unachofuata nje hebu jadili na mwenzio ili mkifanye

Maisha siyo marahisi kiasi hicho mdogo wangu...

Mshukuru Mungu wako kama umejaliwa kupata King...kuna wengine wamelamba majoka...lol!!


Babu DC!!
 
Maisha siyo marahisi kiasi hicho mdogo wangu...

Mshukuru Mungu wako kama umejaliwa kupata King...kuna wengine wamelamba majoka...lol!!


Babu DC!!
Unajua kuzaliwa mlemavu ni bahati mbaya bali kua mzinzi ni uchaguzi na si bahati mbaya. Maisha ni kupanga na kupanga ni kuchagua. Nakubaliana na wewe kaka yangu Dark City kua kuna kulamba galasa au mali. Ni vema sisi wanandoa tukatulia la kama tunaona tulichagua tukiwa bado na tongo tongo machoni basi na tuwaache hao tuliojikuta tunao ili sasa kwa vile tunaona vema tuchague upya ili tuweze kuishi maisha yasiyo na mashaka. Samahani kidogo nakua mkali unajua hatuwezi kuendelea kufuata kawaida ya ulimwengu kwa kisingizio tu eti wengi wanafanya just call a spade a spade and not otherwise eeh.
 
Last edited by a moderator:
Unajua kuzaliwa mlemavu ni bahati mbaya bali kua mzinzi ni uchaguzi na si bahati mbaya. Maisha ni kupanga na kupanga ni kuchagua. Nakubaliana na wewe kaka yangu Dark City kua kuna kulamba galasa au mali. Ni vema sisi wanandoa tukatulia la kama tunaona tulichagua tukiwa bado na tongo tongo machoni basi na tuwaache hao tuliojikuta tunao ili sasa kwa vile tunaona vema tuchague upya ili tuweze kuishi maisha yasiyo na mashaka. Samahani kidogo nakua mkali unajua hatuwezi kuendelea kufuata kawaida ya ulimwengu kwa kisingizio tu eti wengi wanafanya just call a spade a spade and not otherwise eeh.

Ndiyo maana nikasema mshukuru Mungu kama umebarikiwa......

Kunguni wa nyumba ya jirani ni ngumu kujua karaha yake...

Babu DC!!
 
Najua, nitarushiwa kijembe kuwa nawapendelea wananwake! Any way, na mimi pia ni mwanamke! Nafikiri katika mambo yanamuuma mke, ni mume kutoka nje ya ndoa! Hata hawa watu wafanyweje jamani! Kama hawajaridhika si waache wasioe kwanza?Pamoja na hayo, nifikishe hongera zangu kwa good and committed husbands, ambao ni waaminifu kwa wake zao, keep it up!
Kunasababu lukuki zinazomfanya mwanaume atoke nje ya ndoa na naamini we mwanzisha uzi huu unazijua. Perfect couple ningumu sana kuipata. Unakuta mwanaume ana nguvu zaidi ya mkewe na anampenda sana mke wake; sasa kumsurutisha kitandani inakuwa sio vizuri, kwa nini asitafute dem mwingine wa kupunguza hiyo extra iliyomshinda mke wa ndani? Na hii ni kwapande zote, naomba ieleweke hivyo; hata wanawake wanatoka nje ya ndoa.
 
Last edited by a moderator:
Last edited by a moderator:
Sijui kama wapo wanaume wasio toka nje ya ndoa. Nimesema sijui sababu sijawahi waona katika hii dotcom age.
Kwa wanawake, wapo wanaotoka nje ya ndoa ila niwachache ukulinganisha na idadi ya wanaume.
If anything, we are all guilty as charged

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom