Wanaume jiandaeni kupokea maisha baada ya kustaafu

Wanaume jiandaeni kupokea maisha baada ya kustaafu

Na mfe tu masikini
Dunia hii kila mmoja apambane na maisha yake tu
Huku wazee tukistaafu ndio tunauza nyumba zetu na kuhamia sehemu zingine hata iwe nchi tofauti na kuendeleza maisha mpaka mwisho wa siku

Siwezi kutegemea hata siku moja hela za mwanangu ila mimi ndio nawasaidia bado kwa hali na mali ingawa wanafanya kazi
Watoto watakuwa watoto tu na wife tunamaliza nae maisha au nitangulie au atangulie maana huyu ndie tulikuwa nae miaka yote kwa raha na tabu

Najua ni kama ndoto kwa wengi wanaoona wanawake ni wabaya
 
Mkuu watoto kujisahau ni kawaida ila watoto wote yani hata moja asikukumbuke wakati wewe ndio umewafikisha hapo. Kuna story ambayo hukuambiwa kwa hiyo usiweke conclusion maana ugomvi wa familia za kiswahili usiuingilie

Kwa experience yangu, Kuna namna wazazi wa kiume kwa zamani, walikuwa wanafanya makosa waziwazi na kujitenga na familia kiasi cha kukosa bond na watoto wao kwa kuamini watoto hawatoyashikilia dhidi yao. Sasa wanapostaafu, wale workmates na marafiki aliokuwa anawapa muda zaidi wanapotea, ghafla wanachobakiza ni watoto ambao nao hawakujenga bond nao. Hivyo, anaanza kuforce kuingia kwenye mfumo wa watoto wao ambao hakuuweka, na kinachoendelea ni majuto na lawama

Ndugu zangu, tule sana bata na kuinjoi life ila tusidhani ukishawalisha na kuwalipia ada imetosha. Toa muda kutengeneza bond na watoto hata kama ni kwa nadra 🙏🏽
yap nimependa hiyo kuweka bond na watoto na familia bond inajengwa huwezi kulazimisha etii niiwasomesha kwa hiyo lazima wanihangaikie. Na bond haijalishi unapesa au huna asante mkuu bonge la point
 
Sitaki kuamini kile ulichokiandika kama msingi wa hoja yako kina ukweli,
Mosi umesema ana nyumba isyiopungua 300M to 500M, Umesema amesomesha watoto, Umetaja neno wapangaji. Na umesema siku mbili next of kin hawaonekani.

Hili siyo kosa la marehemu, kwangu mimi amefanya kila alichopaswa kufanya hapa duniani, kwa maana ya kuhakikisha anawapatia watoto wake elimu bora na yeye anakuwa na nyumba bora ya kuishi.
Jambo lingine umetaja mzee kukosa chakula na kupewa chakula na wapangaji, umesema mzee kukosa elfu ya kumwahisha hospitali, umetaja mke wake kuwa kwa binti yake kwa zaidi ya miezi mitatu.

Kama ana wapangaji sidhani kama angeweza kukosa elfu 10 ya kumwahisha hospitali, kwa sababu bado alikuwa na uwezo wa kumwita mpangaji mmoja na wakaingia makubaliano akamsaidia kiasi cha hela ili aende hospital.

MKE kwenda kwa binti hili ni janga hasa kwa jamii zetu waafrika na binafsi wazazi nilishawapa msimamo wangu kama nikuja kwangu kusalimia waje wote kwa maana ya baba na mama, siwezi kumwita mama alafu baba akabaki nyumbani peke yake. Vivyo hivyo kwa baba. Unless iwe ni issue ya ugonjwa.

Kwa meneja ambaye amestaafu, sijui alikuwa ni meneja wa taasisi au kampuni ipi lakini naamini hakosi pesheni kuanzia laki 4 kwenda juu kwa mwezi + nyumba za wapangaji anakosaje elfu 10?

ALAFU unatuambie tuuze mali tutunze pesa how? una miaka mingapi wewe? hebu fikisha huo umri uuze mali utunze pesa. Wazungu wanakwambia life begins at 60yrs. Hebu fikiria una miaka 45 uuze pengine nyumba za kupangisha ili utunze hela nadhani wewe utakuwa miongoni mwa wazee wapumbavu kuwahi kutokea.

Alafu kama kweli watoto wa huyo mzee wako serikalini kwa maana ya JMT ni mkoa upi ambao watashindwa kufika nyumbani kwa muda wa siku mbili? Labda hao wa UK wanaweza kuchelewa kwa maana ya flght schedule na flight cancelations tofauti na hapo naona kama ni chumvi.
Mmmh!!!!, mkuu naona una ishi maisha ya kufikilika (mythical life) sio practical, hapa kwetu sio kila siku mpangaji analipishwa kodi kwamba umekosa 10k uende akamgongee mpangaji akupe loh,....... kwa maisha ya kwetu kuna kupindi unaishiea baba mwenye nyumba mpaka unakopa kwa beki 3 (house girl ) licha ya kua unamlipa wewe mshahara tena kiduchu

Mkuu life is not constant labda kwako, kuna siku kama mbili huyu mzee alilala gizani Luku eliisha mpaka alivo tumiwa na nani sijui, omba hi hali isikukute.

Wewe unashangaa watu wa mikoani kuchelewa kuja ku-sign maiti, wakati kuna wengine ndugu wanaishi mkoa moja wanakufa mpaka wanazikwa na manisipa........sawa huenda kuna ugomvi na watoto pamoja na mama yao but not to this extent.
 
yap nimependa hiyo kuweka bond na watoto na familia bond inajengwa huwezi kulazimisha etii niiwasomesha kwa hiyo lazima wanihangaikie. Na bond haijalishi unapesa au huna asante mkuu bonge la point
Mkuu bond must be inborn sio ya kutengeneza ata kama ungeitengeneza kama mitoto ina roho mbaya itakuacha tu. Nadhani DNA ina nguvu kuliko artificial bond.
 
Mm Nafikiri after kustaafu watoto walitakiwa kuweka dada/kaka wa kazi km wao hawapo yeye ndio angeweza wasaidia,they take it from kampuni za usafi and sio mtaani.
Kingine watoto wanatakiwa kua na account ya wazee kila mwezi wanaweka kiasi Kwa makubaliano ya wao wenyewe kulingana na uwezo wa kl mmoja.
Hii hata km wazazi walikula bata ujana wao as long as mmesomeshwa/wanakipato they handle those immediately stuff themselves mpk nyie mkija
Inategemea kama wana uhusiano mzuri, hakuna guarantee ya kusaidiwa na watoto hata kama uliwapa good life, na hii idea ya kufikiri watoto lazima wakusaidie imeponza wengi, na sometimes watoto nao wamechoka njaa tupu hawana msaada wowote
 
Ukitegemea watoto ulio lipia ada kubwa kwenye private schools kukutunza au ukitegemea mke ulio mvumilia siku zote eti ndo atakutunza au ukitegemea hiyo pession 33% yako na bima ya afya ulio pata baada ya kustaafu, hapo umechemsha mkuu.....

Maisha ya kustaafu yanahitaji cash flow or cash in hand sio assets au promises, mzee mstaafu jirani mwenye watoto 5 gradutes kati yao wawili wako wingereza watatu wameajiriwa serikalini, amekufa kifo cha kimasikini sana 'died like apauper' wakati mke wake ameenda kutembelea bint yake mkoani takribani miezi 3 sasa hayupo.....kweli meneja mstaafu ndo wakukosa sh 10,000 kuwayishwa dispensary, ndo wa kupewa chakula na wapangaji?????

Rai yangu if you are 45+ anza kujianda jinsi ya kustaafu kwa heshima uza baadhi ya mari zako utunze pesa sio sehemu moja never ever over trust your wife, hao wa dudu tukikua wana badilika na kuhamia kwa watoto wao. Kwa kweli nime umia sanaa mzee kajitahidi sanaa kutunza familia uwe first class nyumba yake ni 300m to 500m worthy ila bado maiti iko hospitali next of kin bado hawajafika hi ni siku ya pili.
Haya mambo ya kuzika hela kwenye kujenga jumba la kifahari halafu huna investment ni tatizo kubwa sana kwa watu weusi
 
Ushauri ulioutoa umenipa simanzi kubwa. Sisi tuliostaafu tunaona mengi. Tuna upweke, marafiki wametukimbia, mapato na matumizi hayaoani, tunapoenda mahospitalini tunaambiwa dawa hii kanunue, pensheni ya kila mwezi haitoshi, huku nyumbani matumizi yote lazima uyasimamie mfano chakula, umeme, maji n.k. Ninyi Watumishi mlio bado mnaendelea na kazi nawashauri mjipange msije mkatangulia mbele ya haki kabla ya muda kutokana na maisha kuwa magumu.
 
Mmmh!!!!, mkuu naona una ishi maisha ya kufikilika (mythical life) sio practical, hapa kwetu sio kila siku mpangaji analipishwa kodi kwamba umekosa 10k uende akamgongee mpangaji akupe loh,....... kwa maisha ya kwetu kuna kupindi unaishiea baba mwenye nyumba mpaka unakopa kwa beki 3 (house girl ) licha ya kua unamlipa wewe mshahara tena kiduchu

Mkuu life is not constant labda kwako, kuna siku kama mbili huyu mzee alilala gizani Luku eliisha mpaka alivo tumiwa na nani sijui, omba hi hali isikukute.

Wewe unashangaa watu wa mikoani kuchelewa kuja ku-sign maiti, wakati kuna wengine ndugu wanaishi mkoa moja wanakufa mpaka wanazikwa na manisipa........sawa huenda kuna ugomvi na watoto pamoja na mama yao but not to this extent.
Sikuongelea ndugu nimeongelea watoto kama ulivoandika wewe.
Kama ni mtoto wakiume na ukakubali kumwacha babako anatesa mpaka kufikia kukosa hiyo shilingi elfu hebu jitafakari, zitafakari zile siku alizokuwa kama wewe. Then hoja ya kuuza mali ili utunze hela hiyo ni hoja mfu Kabisa
 
yap nimependa hiyo kuweka bond na watoto na familia bond inajengwa huwezi kulazimisha etii niiwasomesha kwa hiyo lazima wanihangaikie. Na bond haijalishi unapesa au huna asante mkuu bonge la point
True mkuu, Bond ni moments na kama mtoto kila anachokumbuka kuhusu wewe ni kutokuwepo home bila kuwapa muda hata ukirudi, bond haiwezi kuwepo. Shukrani mkuu 🙏🏽🙏🏽
 
Maisha yana mkanganyiko sana. Ushauri wako wa kujiandaa na kustaafu ni muhimu sana na nashauri usijiandae ukifika miaka 45 unaweza kuwa umechelewa pia.

Jitahidi uanze kujiandaa pale unapoanza kazi ndio maana hata akiba ya pensheni huwekwa mara unapoanza kazi. Jitahidi sana kuwa na tabia ya kuwekeza kwenye mambo yatakayokusaidia kupata pesa ukistaafu. Weka leo kidogo kidogo ili walau uwe na uhakika utapostaafu utapata kipato sawa na ulichokuwa unapata kabla ya kustaafu.

Watoto hukumbwa na changamoto zao za kifamilia pia au malengo ya kijamii. Zipo nyakati nao huhisi mzazi yuko njema kumbe sivyo. Na hii dhana ya kuwa mtoto akiwa nje ya nchi anakuwa vizuri sijui huwa inatoka wapi. Wengi waliopo nje ya nchi wamechoka sana sometimes hata nauli ya kurudi hawana (na wasiporudi tunadhani hawatupendi). Na wengine wanatamani kurudi lakini wakiwaza wakija wanaanzia wapi, wanaona aibu jamii itawaonaje Bongo.

Kibongo bongo, diaspora wengi hawana msaada kwa wazazi wao zaidi ya kutuma gadgets ambazo hazina maana kwa wazazi wao.
 
Ukitegemea watoto ulio lipia ada kubwa kwenye private schools kukutunza au ukitegemea mke ulio mvumilia siku zote eti ndo atakutunza au ukitegemea hiyo pession 33% yako na bima ya afya ulio pata baada ya kustaafu, hapo umechemsha mkuu.....

Maisha ya kustaafu yanahitaji cash flow or cash in hand sio assets au promises, mzee mstaafu jirani mwenye watoto 5 gradutes kati yao wawili wako wingereza watatu wameajiriwa serikalini, amekufa kifo cha kimasikini sana 'died like apauper' wakati mke wake ameenda kutembelea bint yake mkoani takribani miezi 3 sasa hayupo.....kweli meneja mstaafu ndo wakukosa sh 10,000 kuwayishwa dispensary, ndo wa kupewa chakula na wapangaji?????

Rai yangu if you are 45+ anza kujianda jinsi ya kustaafu kwa heshima uza baadhi ya mari zako utunze pesa sio sehemu moja never ever over trust your wife, hao wa dudu tukikua wana badilika na kuhamia kwa watoto wao. Kwa kweli nime umia sanaa mzee kajitahidi sanaa kutunza familia uwe first class nyumba yake ni 300m to 500m worthy ila bado maiti iko hospitali next of kin bado hawajafika hi ni siku ya pili.
Noted..
Huu Ni Uzi Bora kabisa tangu kuanza mwaka huu..
 
Ushauri ulioutoa umenipa simanzi kubwa. Sisi tuliostaafu tunaona mengi. Tuna upweke, marafiki wametukimbia, mapato na matumizi hayaoani, tunapoenda mahospitalini tunaambiwa dawa hii kanunue, pensheni ya kila mwezi haitoshi, huku nyumbani matumizi yote lazima uyasimamie mfano chakula, umeme, maji n.k. Ninyi Watumishi mlio bado mnaendelea na kazi nawashauri mjipange msije mkatangulia mbele ya haki kabla ya muda kutokana na maisha kuwa magumu.
Sawa
 
MZUSHI tu huyu imagine mtu aliyestaafu akiwa Meneja hivi anajua pensheni kila mwezi ni shilingi ngapi? Mtu ana nyumba za kupangisha anakosaje elfu kwenda hospitali? Ana watoto wanafanyakazi serikalini ambao wote hao kwenye bima zao wamemregister baba yao, manake ana kadi tatu za bima. Tanzania hii ni mkoa upi mtu atakaa amalize siku mbili bila kufika mkoa mwingine? Upuuzi mtupu.
sema na wewe
 
Back
Top Bottom