Baada ya kustaafu katelekezwa na mke na watoto wake. Anaugua ugonjwa wa akili kwa sasa

Azoge Ze Blind Baga

JF-Expert Member
Mar 8, 2019
366
1,376
Nashindwa sometimes kuelewa nini faida na umuhimu wa ndoa kama mambo yenyewe huwaga hivi.

Kuna mzee mmoja alikua jirani yangu, alikua mhandisi wa shirika moja kubwa hapa nchini

Mzee huyu kutoka kule migombani alioa mke wa migombani pia. Maisha yalikua mazuri wakati mzee bado anafanya kazi.

Alijenga nyumba mikoa mbalimbali na alijitahidi kuwasomesha watoto wake shule nzuri hizi za saint saint.

Watoto wake wote wana shughuli zao nzuri tu.

Baada ya kustaafu hapo ndo akaanza kuona rangi halisi ya mke wake. Kwanza alimtumia wakora wamfanye kitu mbaya ili mke arithi mali mapema bahati nzuri ndugu wa mume wakashtukia mapema mission ikabuma.

Tangu wakati huo mke akaanza kumtenga mume wake na kibaya zaidi hadi watoto wake aliowasomesha wakamtenga baba yao na kumsahau kabisa(sijui mama yao aliwaambia nini)

Dingi akaanza kunyimwa chakula, dingi akakimbiwa chumba na mke wake(alikua anatuambia vijana na kutuhasa juu ya makabila ya kuoa)

Baada ya muda mzee kaanza kurukwa na akili kwa maisha aliyokua anaishi.

Kwa sasa mzee karudi kwao lakini akili yake haiko sawa kaacha mali zote anaishi kijijini kwao. Watoto wake wamemtupa hawana time na baba yao

Je nini hasa wamama wanawaambia watoto wao kiasi cha watoto kuanza kumchukia baba yao na kumtenga ili hali aliwasomesha na kuwalea vizuri na juhudi zake waliziona.?

Hili ni janga kwenye familia nyingi baba akistaafu anaishi maisha magumu ya kunyanyasika juhudi zake zote alizofanya kujenga familia bora zinakua kazi bure anaishia kutengwa na kupata msongo wa mawazo na mwisho kufa.

KATAA NDOA NI UUAJI NA UTAPELI
 
Inasikitisha sana hao watoto wake itawagharimu kwa wanachokifanya kwa baba yao hata kama alikuwa na makando kando hawakupaswa kumtenga baba yao.
Yule mzee na familia yake nimeishi nao jirani sana mzee alikua mtu poa na watoto wake walisoma shule nzuri sana ila ndo hivyo wamemtelekeza. Kuna wakati alikua anahudumiwa na binti yake kama kumpikia na kumchotea maji mke wake alisepa sijui alienda kudanga wapi.
 
Yule mzee na familia yake nimeishi nao jirani sana mzee alikua mtu poa na watoto wake walisoma shule nzuri sana ila ndo hivyo wamemtelekeza. Kuna wakati alikua anahudumiwa na binti yake kama kumpikia na kumchotea maji mke wake alisepa sijui alienda kudanga wapi.
wazee wengi wakistaafu kuna maisha ya upweke na kutengwa wanayapitia hasa pale mafao yanapoisha, huenda mwanamke alikuwa na mipango yake ila hao watoto wake wamekosea sana.
 
All women are devils only your mother might be good to you, But she is still a devil to your father.

Mzee mmoja aliniambia kijana hata "Mama" awe mbaya na muovu kiasi gani na Baba awe mzuri kiasi gani, Siku zote watoto watakuwa upande wa Mama kumtetea maovu yake.

As a Man, lazima uwe na "back up plan" ya ku survive individually wakati wowote ule.
 
Ishini nao kwa akili
Unamuoa kwa gharama, u atumia gharama kulisha na kusomesha familia
Unamfungulia mradi kwa gharama zako,

Mwisho wa siku unastaafu ukiamini ile miradi uliomfungulia atakumbuka wema wako na kuendeleza familia lakini laah wapi, wanawake wana moyo wa ubinafsi sana, akitoa kidogo tuu kwa ajili yako anaanza kujiona na yeye ni mwanaume,

Unaambiwa hawa watu hata wakitumia pesa zao pia huwa inawauma,

Wanaume tuwe makini sana, kila unapopiga hatua hakikisha unajiwekea akiba yako ya uzeeni, kamwe usije ukadhania miradi unayomfungulia mkeo itakusaidia, utakuja kujihisi unaishi na shetani bure, utajisikia kuzunguzungu na kuona ndoa kama jehanamu ndogo,

Wapo tayari wafe hela zao zinakie Bank huko hawa viumbe
 
Nashindwa sometimes kuelewa nini faida na umuhimu wa ndoa kama mambo yenyewe huwaga hivi.

Kuna mzee mmoja alikua jirani yangu, alikua mhandisi wa shirika moja kubwa hapa nchini

Mzee huyu kutoka kule migombani alioa mke wa migombani pia. Maisha yalikua mazuri wakati mzee bado anafanya kazi.

Alijenga nyumba mikoa mbalimbali na alijitahidi kuwasomesha watoto wake shule nzuri hizi za saint saint.

Watoto wake wote wana shughuli zao nzuri tu.

Baada ya kustaafu hapo ndo akaanza kuona rangi halisi ya mke wake. Kwanza alimtumia wakora wamfanye kitu mbaya ili mke arithi mali mapema bahati nzuri ndugu wa mume wakashtukia mapema mission ikabuma.

Tangu wakati huo mke akaanza kumtenga mume wake na kibaya zaidi hadi watoto wake aliowasomesha wakamtenga baba yao na kumsahau kabisa(sijui mama yao aliwaambia nini)

Dingi akaanza kunyimwa chakula, dingi akakimbiwa chumba na mke wake(alikua anatuambia vijana na kutuhasa juu ya makabila ya kuoa)

Baada ya muda mzee kaanza kurukwa na akili kwa maisha aliyokua anaishi.

Kwa sasa mzee karudi kwao lakini akili yake haiko sawa kaacha mali zote anaishi kijijini kwao. Watoto wake wamemtupa hawana time na baba yao

Je nini hasa wamama wanawaambia watoto wao kiasi cha watoto kuanza kumchukia baba yao na kumtenga ili hali aliwasomesha na kuwalea vizuri na juhudi zake waliziona.?

Hili ni janga kwenye familia nyingi baba akistaafu anaishi maisha magumu ya kunyanyasika juhudi zake zote alizofanya kujenga familia bora zinakua kazi bure anaishia kutengwa na kupata msongo wa mawazo na mwisho kufa.

KATAA NDOA NI UUAJI NA UTAPELI
Duu! Ni hatari sana
 
Hila hela za kustafu sijui zina shida gani unakuta mtu anajielewa ana akili timamu kabla hajapata zile hila wakishastaf ile hela ikiingia kwenye account anaona kuna million 100 hapo akili inabadilika hela ikiisha akili zinarudi na hata sisi tunaoandika hapa tunawaponda wazee wetu lakini mwisho wa siku na sisi ni hvyo hvyo
 
Kuna jamaa yangu alikua benchi,hata hela ya kula hana,anadaiwa kodi,.jamaa anahangaika kukopa ili asogeze siku hadi apate mishe, mke wake anamchora tu na kumpa moyo,jamaa akakuta kabatini mwanamke kaficha laki tisa,.900000/= nyekundu tupu..jamaa kapita nazo kimya kimya,.
 
Dingi akaanza kunyimwa chakula, dingi akakimbiwa chumba na mke wake(alikua anatuambia vijana na kutuhasa juu ya makabila ya kuoa
Huu uongo....mwanzo umesema wote ni kabila moja la.migombani.
Harafu mtu mwenye hela kama unavyosema hakimbiwi kamwe.

Unless pesa zake alitumia kuhonga michepuko sasa amestafu pesa hakuna anataka huruma kwa wale aliowanyima
 
Nyumba alimilikisha watoto ambao ndo hao wamemtelekeza kwa hiyo kwa sasa hana uwezo wa kufuatilia tena amekua na tatizo la ugonjwa wa akili na hili limetokea miezi michache baada ya kustaafu ndo mke nae akaanza hapo hapo ukatili dhidi ya mume wake kwa kushirikiana na hao watoto wake. Na pia mzee alikuwa na watoto wengi
Mzee huyu hakujipanga kama ulivyotunga uongo hapo juu.

Mzee akistafu tu na kuanza kuumwa hizo ni stress za maisha kutokana na kipato Duni.

Sasa wewe unasema ana nyumba kika mkoa, watoto wote wamesomea saint saint mbona scenario haviendani?
 
Back
Top Bottom