Mwl Philemon

Member
Nov 29, 2018
61
67
WANAOFAIDI KEKI YA TAIFA​

Na Thadei Ole Mushi.

Kwa Mwezi anapokea Milioni 11,000,000

Kwa mwaka atapokea 132,000,000

Kwa miaka mitano atapokea Jumla 660,0000

Huu ni mshahara tu hujaweka kiinua Mgongo, bado Sitting allowance, bado Posho mbalimbali nk. Tuachane na mawaziri na manaibu waziri ambao fedha hii inaongezeka.

Mshahara huu uliingia Moja kwa moja kwenye account Ina maana labda ulikuwa na Makato ya kodi nk au Hauna hayo Makato lakini take home yake ni hiyo iliyoingia kwenye Simu.

Kazi yake kubwa Bungeni Ni kupiga makofi meza, kuitikia ndio au hapana Bungeni.

Huyu mbunge Sifa zake kitaaluma anatakiwa kujua kusoma na kuandika tu.

Njoo kwa Mwalimu anayeajiriwa na Degree moja.

Anaanza na msahahara wa TGTS D1 mshahara wake Ni 733,000 akikatwa Kodi, bima, NSSF, CWT, Loan Board, anabakiwa na shilingi 500,000 plus kwa Mwezi.

Kwa mwaka atachukua 6,000,000 huu mshara wa mwaka haujafikia mshahara wa Mbunge kwa Mwezi mmoja.

Kwa miaka mitano atachukua Milioni 30 plus huku mmbunge akichukua Milioni 660,000, 000.

Majukumu ya huyu mwalimu Sitaki kuyataja kwani ni Mengi mno.

Daktari anayeanza na Degree Moja.

Huyu analipwa 1,400,000 bila makato Kama akikatwa vikorokoro vyote anabakiwa na 900,000 kwa Mwezi.

Kwa mwaka atachukua 10,800,000 bado hajafikia mshahara wa Mbunge.

Kwa miaka mitano atachukua Milioni 54,000,000 huku Mbunge akichukua Milioni 660,000,000.

Majukumu ya Daktari unayajua hatuna haja ya kuyataja.

Ole Mushi
0712702602

Viva
Ambakisye Mwakisyala Mlima
Msemakweli Daima
 
Mushi kwanini umepotosha umma nilitarajia useme hivi

1. Mbunge kwamwezi mshahara wake ni million 3.8(million 4) huo ndo mshahara wa mbunge anaokatwa kodi.

2. Hizo zote zinazobakia zinaingia kwenye account yake matumizi mbalimbali ya shughuli zakibunge na ofisi ya mbunge .eg ,mafuta ya gari wakati anafanya shughulu zake kibunge asikwame, kumlipa dereva wake, kumlipa katibu wake wajimbo, kununua furniture's za ofisi..

Siafiki namna ambavyo wao hua wanapewa bandolote lafedha hizo moja kwa moja mana wabunge wengine hata majimboni huwa hawafiki lakini mpunga anapokea wamefuta kila kitu.
 
Sasa fikiria wangekuwa sio wabunge.. hao ndio mabahiri balaa,wanataka kuonesha wananchi wao hali ni ngumu hadi wao wanalazimika kupata bodaboda ama bajaji.

Kupanga ni kuchagua..ndiyo maana 2020 robo ya watanzania walichukua fomu za kugombea ubunge.
Pamoja na pato hilo lote bado wabunge wanatumia bodaboda na bajaji kuhudhuria vikao vya bunge...!!
 
Sasa fikiria wangekuwa sio wabunge.. hao ndio mabahiri balaa,wanataka kuonesha wananchi wao hali ni ngumu hadi wao wanalazimika kupata bodaboda ama bajaji.

Kupanga ni kuchagua..ndiyo maana 2020 robo ya watanzania walichukua fomu za kugombea ubunge.
Hatari sana...!!
 
Huu Uzi naona ni Kuwapandisha tu Hasira Watanzania na labda Kuwaelekeza na wale Vijana 854 wa JKT waliotimuliwa ni wapi waanzie kama wanataka Kupata Pesa za haraka haraka huku wakiwa na Mafunzo mazuri ya Kimedani.
 
Utashangaa bado watu wanaamini siasa ya vyama.
Yaan mtu anakula pesa ambayo mkichanga ukoo mzima hamfikishi hata nusu?

Yanatokea majanga mengi sana Tanzania,husikii hawa wanasiasa wakisema tusilipwe mishahara yetu na pesa ikahudumie waathirika!
Bunge letu ni moja ya mizigo kubwa kwa taifa,nadhani pia tunahaja ya kubadili hata idadi ya wawakilishi bungeni.

Katiba mpya ilete majibu na suluhisho la walaji keki hii ya taifa,kama taifa ni letu sote kwanini wachache wawe wanufaikaji wakubwa?! Tutafakari
 
Yaani katika watu ninge suggest walipe mkwanja mrefu

Ni waalimu
Nawaheshimu sana hawa watu na kweli wanapitia mengi sema ndo wanaongoza kwa kudharauliwa .. wengine mazingira ya kazi wanapofanyia ni magumu

Matabibu
Hawa wanahakikisha tunakuwa na afya na afya ni muhimu ni uhai hivyo tuendelee kulitumikia taifa vizuri .ila cha ajabu kuna zahanati vijijini utakuta yupo mmoja .. zahanati iyo ipo kwenye jimbo la mbunge mwenye makazi dar anayetibiwa agha khan au ocean road

Vyombo vya ulinzi
Hawa watu Mungu awabariki tuu japo kama kuna mapungufu ni kawaida kwa kada nyengine


Yaani wanasiasa inabidi mishahara yao ipunguzwe kuanzia mawaziri ,makatibu wakuu,wabunge,rc,dc, ded, nk ije kujalizia huku maana sijaona umuhimu wao kuzidi hao watu niliotaja hapo juu

Kazi kukaa ofisini kwenye kiyoyozi nakutoa order tu wengine hata kutembelea watu wajue kero zao mda huo hawana
 
Hii iangaliwe upya, kuna haja ya kuwa na bunge kubwa ilhali wengine wanakaa miaka mitano bila ya kuchangia? Wabunge wawe wa kujitolea kama wana uchungu na maendeleo ya wananchi au iwe ajira kama ajira nyingine wapokee mshahara wa kawaida tu. Tuwe na wabunge wa kila wilaya wanatosha
 
Back
Top Bottom