Maswali ambayo viongozi wa Chama Cha Walimu (CWT) wamegoma kujibu

MIMI BABA YENU

JF-Expert Member
Mar 1, 2019
295
679
Walimu Wana maswali mengi ambayo kwa muda Mrefu CWT wakiongozwa na Kiongozi wao Japhet Maganga hawataki kujibu na wala hawaoneshi jitihaza zozote kutetea haki za walimu:

i) Mapato yatokanayo na vitega uchumi vya chama mfano: Mwalimu house na ofisi za CWT kila mkoa (rent), je vinamnufaishaje mwalimu ambaye ni mchangiaji mkuu?

ii)Kwanini C.W.T wanakusanya michango kwa wanachama kila mwezi badala ya kukusanya mara moja kwa mwaka kama vyama vingine?

iii) Kwanini kuna tofauti katika makato ya kuchangia mfuko wa C.W.T wakati huduma ni sawa? Kuna nini kinachoongezeka kwa anayekatwa zaidi na nini kinachopungua kwa anayekatwa chini? Tofauti hizo zinaletwa na mfumo wa asilimia zilizowekwa na hivyo kuweka wachangiaji katika matabaka yasiyo na tija wakati huduma ni sawa.

Mfano mwalimu mwenye TGTS I yeye kwa Mwaka CWT huchukua 674,000 kwenye mshahara wake. Huyu anasaidiwaje zaidi tofauti na mwenye TGTS E ambaye hukatwa 225,000?. CWT wanakata Fedha nyingi Sana kwa Walimu na hakuna anayejali.

Malipo ya wanayopata ni T-shirt ambazo wamekuwa wakizilalamikia kila mwaka kutokana na kukosa ubora.

iv) Je kuna uhalali gani wa kiinua mgongo cha mwanachama anayestaafu kwa uwiano na alichochangia toka uanachama wake hadi kustaafu? Ikiwa kiinua mgongo kilichopangwa na C.W.T kwa sasa ni mabati ishirini (20) au laki tatu (300,000/=)

V) Je, C.W.T kwa mwaka inakusanya kiasi cha shilingi ngapi kwa waalimu wote Tanzania kwa makato ya asilimia mbili (2%) ya kila mshahara wa mwanachama ambayo pia inatofautiana kulingana na madaraja.

Vi) C.W.T inawafanyakazi wangapi kwa kila mkoa na taifa kwa ujumla na posho zao zikoje?

Vii) Kwa kuwa waalimu wamekua wakinyanyasika na kudharaulika na kutosikilizwa katika halmashauri, Je, C.W.T inafanya nini kurudisha hadhi ya mwalimu katika ngazi ya halmashauri ilihali mambo haya yanaendelea kumgandamiza na kumnyanyasa mwalimu?

Haya ni maswali muhimu Uongozi wa Japhet Maganga umeshidwa kujibu na hivyo basi anakosa sifa za kuendelea kuwa kiongozi ndani ya chama cha walimu
 
Hizi mada hazina mashiko kwa sasa. Kama mwalimu unaona huridhishwi na CWT, hamia Chakuhawata, ili mkapambanie haki zenu huko. Kualalamika tu kila siku haikusadii chochote ndugu mwalimu.

Ni ushauri tu lakini.
Nakuunga mkono , hicho chama kimeshapoteza sifa ya kuwa chama cha wafanyakazi. Si kwa sababu hawana katiba Wala miongozo , Bali ni kwa matendo ya viongozi wao na kwa jinsi walivyojifunga kwenye gereza la ccm. Walimu wanaoona hawapati Huduma kama inavyostahili wahame, na sio kulalamika tu.
 
Nakuunga mkono , hicho chama kimeshapoteza sifa ya kuwa chama cha wafanyakazi. Si kwa sababu hawana katiba Wala miongozo , Bali ni kwa matendo ya viongozi wao na kwa jinsi walivyojifunga kwenye gereza la ccm. Walimu wanaoona hawapati Huduma kama inavyostahili wahame, na sio kulalamika tu.
Walimu Wana Nia ya kuhama nawameichoka CWT, ila changamoto ni ile nguvu cwt pamoja na maafisa Utumishi waitumia kuzuia walimu wasihame.

Pili ukimya wa serikali, licha ya madudu yote ya CWT lakini serikali iko kimyaaa, labda iko nyuma ya uwizi na dhuruma wanayofanyiwa walimu. Poleni ndugu walimu
 
Suluhu ya malalamiko yenu ni hii:

1. Itisheni kikao cha walimu wote wanachama wa CWT Tanzania nzima..

2. Wekeni hoja hizi mezani. Zijadilini na kisha wekeni maazimio na yapelekeni chamani ili hatua zichukuliwe..

3. Wakikataa kuridhia maamuzi ya wanachama, wekeni petition na isainiwe na kila mwanachama na kuipeleka Kwa mrajisi wa vyama vya wafanyakazi kuvunja chama hicho na kuunda kingine..

## Ni kweli kabisa kuwa si haki na sio sahihi hata kidogo kuweka percentage (%) toka kwenye kila mshahara wa mwalimu kama ada ya mwanachama wa chama cha wafanyakazi huku kukiwa na variation ya viwango hivyo vya mishahara kwa kila mwalimu..

## Si haki na si sahihi pia kutoza ada ya uanachama wa Chama Cha Wafanyakazi kwa Kila mwezi badala ya kiwango cha mara moja kwa mwaka..

## Kwa kutoza ada kila mwezi tena Kwa percentage ya mshahara wa kila mwalimu, hiyo inakuwa si ada ya uanachama wa chama cha wafanyakazi bali ni biashara fulani Kwa kutumia jasho la wafanyakazi wa sekta ya ualimu..!!
 
Walimu Wana Nia ya kuhama nawameichoka CWT, ila changamoto ni ile nguvu cwt pamoja na maafisa Utumishi waitumia kuzuia walimu wasihame.
Pili ukimya wa serikali,licha ya madudu yote ya CWT lakini serikali iko kimyaaa,labda iko nyuma ya uwizi na dhuruma wanayofanyiwa walimu.Poleni ndugu walimu
Mbona hili la serikali kufurahia ugoigoi WA Cwt liko wazi! Serikali inanifaika kwakuwa hawapati challenge yoyote kutoka kwa kundi kubwa la watumishi. Actually, cwt dhaifu inafanya hata vyama vingine vya wafanyakazi vitafakari mara mbili kabla ya kuanzisha harakati za madai ya wanachama wao.


Nawapongeza chama Cha madakitari wa kipindi kile Cha migomo ya madakitari, maana wao waliweza kupata walau nasilahi bora kuliko wafanyakazi wengine.


CWT hawawezi kuitisha hata mgomo wa siku Moja. Hakuna masilahi bora ya walimu yatakuja bila mgomo. Mgomo ndio silaha muhimu ya trade unions. Unafanya majadiliano na serikali ya ccm iliyojaa walafi utegemee watakupa tu masilahi?


Natamani cwt ife kabisa ili kuwe na mawazo mbadala
 
Walimu Wana maswali mengi ambayo kwa muda Mrefu CWT wakiongozwa na Kiongozi wao Japhet Maganga hawataki kujibu na wala hawaoneshi jitihaza zozote kutetea haki za walimu:

i) Mapato yatokanayo na vitega uchumi vya chama mfano: Mwalimu house na ofisi za CWT kila mkoa (rent), je vinamnufaishaje mwalimu ambaye ni mchangiaji mkuu?

ii)Kwanini C.W.T wanakusanya michango kwa wanachama kila mwezi badala ya kukusanya mara moja kwa mwaka kama vyama vingine?

iii) Kwanini kuna tofauti katika makato ya kuchangia mfuko wa C.W.T wakati huduma ni sawa? Kuna nini kinachoongezeka kwa anayekatwa zaidi na nini kinachopungua kwa anayekatwa chini? Tofauti hizo zinaletwa na mfumo wa asilimia zilizowekwa na hivyo kuweka wachangiaji katika matabaka yasiyo na tija wakati huduma ni sawa.

Mfano mwalimu mwenye TGTS I yeye kwa Mwaka CWT huchukua 674,000 kwenye mshahara wake. Huyu anasaidiwaje zaidi tofauti na mwenye TGTS E ambaye hukatwa 225,000?. CWT wanakata Fedha nyingi Sana kwa Walimu na hakuna anayejali.

Malipo ya wanayopata ni T-shirt ambazo wamekuwa wakizilalamikia kila mwaka kutokana na kukosa ubora.

iv) Je kuna uhalali gani wa kiinua mgongo cha mwanachama anayestaafu kwa uwiano na alichochangia toka uanachama wake hadi kustaafu? Ikiwa kiinua mgongo kilichopangwa na C.W.T kwa sasa ni mabati ishirini (20) au laki tatu (300,000/=)

V) Je, C.W.T kwa mwaka inakusanya kiasi cha shilingi ngapi kwa waalimu wote Tanzania kwa makato ya asilimia mbili (2%) ya kila mshahara wa mwanachama ambayo pia inatofautiana kulingana na madaraja.

Vi) C.W.T inawafanyakazi wangapi kwa kila mkoa na taifa kwa ujumla na posho zao zikoje?

Vii) Kwa kuwa waalimu wamekua wakinyanyasika na kudharaulika na kutosikilizwa katika halmashauri, Je, C.W.T inafanya nini kurudisha hadhi ya mwalimu katika ngazi ya halmashauri ilihali mambo haya yanaendelea kumgandamiza na kumnyanyasa mwalimu?

Haya ni maswali muhimu Uongozi wa Japhet Maganga umeshidwa kujibu na hivyo basi anakosa sifa za kuendelea kuwa kiongozi ndani ya chama cha walimu
Walimu ni punching bag la CCM, tulieni mfirigiswe
 
Walimu Wana maswali mengi ambayo kwa muda Mrefu CWT wakiongozwa na Kiongozi wao Japhet Maganga hawataki kujibu na wala hawaoneshi jitihaza zozote kutetea haki za walimu:

i) Mapato yatokanayo na vitega uchumi vya chama mfano: Mwalimu house na ofisi za CWT kila mkoa (rent), je vinamnufaishaje mwalimu ambaye ni mchangiaji mkuu?

ii)Kwanini C.W.T wanakusanya michango kwa wanachama kila mwezi badala ya kukusanya mara moja kwa mwaka kama vyama vingine?

iii) Kwanini kuna tofauti katika makato ya kuchangia mfuko wa C.W.T wakati huduma ni sawa? Kuna nini kinachoongezeka kwa anayekatwa zaidi na nini kinachopungua kwa anayekatwa chini? Tofauti hizo zinaletwa na mfumo wa asilimia zilizowekwa na hivyo kuweka wachangiaji katika matabaka yasiyo na tija wakati huduma ni sawa.

Mfano mwalimu mwenye TGTS I yeye kwa Mwaka CWT huchukua 674,000 kwenye mshahara wake. Huyu anasaidiwaje zaidi tofauti na mwenye TGTS E ambaye hukatwa 225,000?. CWT wanakata Fedha nyingi Sana kwa Walimu na hakuna anayejali.

Malipo ya wanayopata ni T-shirt ambazo wamekuwa wakizilalamikia kila mwaka kutokana na kukosa ubora.

iv) Je kuna uhalali gani wa kiinua mgongo cha mwanachama anayestaafu kwa uwiano na alichochangia toka uanachama wake hadi kustaafu? Ikiwa kiinua mgongo kilichopangwa na C.W.T kwa sasa ni mabati ishirini (20) au laki tatu (300,000/=)

V) Je, C.W.T kwa mwaka inakusanya kiasi cha shilingi ngapi kwa waalimu wote Tanzania kwa makato ya asilimia mbili (2%) ya kila mshahara wa mwanachama ambayo pia inatofautiana kulingana na madaraja.

Vi) C.W.T inawafanyakazi wangapi kwa kila mkoa na taifa kwa ujumla na posho zao zikoje?

Vii) Kwa kuwa waalimu wamekua wakinyanyasika na kudharaulika na kutosikilizwa katika halmashauri, Je, C.W.T inafanya nini kurudisha hadhi ya mwalimu katika ngazi ya halmashauri ilihali mambo haya yanaendelea kumgandamiza na kumnyanyasa mwalimu?

Haya ni maswali muhimu Uongozi wa Japhet Maganga umeshidwa kujibu na hivyo basi anakosa sifa za kuendelea kuwa kiongozi ndani ya chama cha walimu
Enzi hizi za ubepari bado mnahangaika na trade unions...mnaliwa hela zenu bure kabisa!
 
Tunasikia mapesa ya hao walimu ndio yanatumika kwenye kampeni.

Kama yapo hayo mapesa kwa nini hawaambii yako kiasi gani?

Nakumbuka mwaka ule wanajenga jengo lao lile pale Ilala (Mwalimu House) waliwaaminisha kuwa wataondokana na michango na waalimu watanufaika na faida itakayokuwa inapatikana.

Leo yako wapi?
 
Walimu mnaochangia Siwitiii mnaliwa. Hicho chama hakipo kwa ajili ya walimu kwani viongozi wake wapo kwa ajili ya maokoto na si kusaidia walimu.Wanalipana posho na mishahara ya kufuru mpaka wanakataa teuzi kutoka kwa mh Rais kwa kuona kwenye utumishi wa umma hakuna mishahara mikubwa na hela za bure kama ilivyo siwitii wanajichotea tu mabilioni

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
Nawapongeza chama Cha madakitari wa kipindi kile Cha migomo ya madakitari, maana wao waliweza kupata walau nasilahi bora kuliko wafanyakazi wengine.
Chama cha madaktari sio chama cha wafanyakazi ni chama cha wanataaluma,Madaktari wapo chini TUGHE NA TALGWI
 
) Je kuna uhalali gani wa kiinua mgongo cha mwanachama anayestaafu kwa uwiano na alichochangia toka uanachama wake hadi kustaafu? Ikiwa kiinua mgongo kilichopangwa na C.W.T kwa sasa ni mabati ishirini (20) au laki tatu (300,000/=)
Kwanza CWT ndio chama pekee cha wafanyakazi kinachotoa mkono wa kwaheri aliekua mwanachama wa CWT, pia CWT inarudisha 15% kwa wanachama kila Tawi
 
Hizi mada hazina mashiko kwa sasa. Kama mwalimu unaona huridhishwi na CWT, hamia Chakuhawata, ili mkapambanie haki zenu huko. Kulalamika tu kila siku haikusadii chochote ndugu mwalimu.

Ni ushauri tu lakini.
Kundi la walimu ni kama nyumbu wao kutwa kulalamika badala ya kuchukua hatua, 60% ya watumishi wa umma ni walimu lakini wanaendeshwa na HRs ambao hawafiki hata 0.5% ya watumishi wa umma.
 
Kwanza CWT ndio chama pekee cha wafanyakazi kinachotoa mkono wa kwaheri aliekua mwanachama wa CWT, pia CWT inarudisha 15% kwa wanachama kila Tawi
Sasa umekuja kulalamika nini hapa kama unapewa 15%? teacher kwanza huu ni muda wa kuingia darasani hapa JF unafanya nini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom