Wadau wa JF,
Haiitaji mjadala mkubwa kwamba waanzilishi wa JF wanastahili pongezi nyingi sana kwa kufikiria kuwa na kitu kama hiki. Hatupashwi kuwashukuru kwa kuwa na wazo kuanzisha JF tu, bali pia kuhakikisha JF inakua na kufikia ilipo sasa. Najua haikuwa kazi rahisi, lakini mmeweza. Nawapeni pongezi.
Kwa sisi wadau, tunalo jukumu la kuhakikisha kwamba JF inaendelea kuwepo kwa kutoa michango ya hapa na pale mara tunapotakiwa kufanya hivyo. Tuwaunge mkono waanzilishi.
Labda niitumie nafasi hii pia kusema kwamba JF ya miaka ile ya 2008 wakati najiunga, si kama JF ya sasa. Nilikuwa nikiingia JF, natarajia kupata mambo mapya ambayo hatuyasomi hata kwenye magazeti, constructive contrbutions kutoka kwa members na mambo kama hayo. Ilikuwa ni sehemu ambayo mbali na kupata habari, lakini pia mtu ulikuwa unajifunza mengi usiyoyajua. JF ya sasa imebadilika kuwa uwanja wa mipasho, kejeli na matusi na hasa kutoka kwa wale waliojiunga JF kama sehemu ya ajira yao. JF hongera kwa hili pia kwamba sasa mmesaidia kutoa ajira kwa Watanzania. Ningependa kupendekeza kwamba kuna haja ya kuongeza idadi ya moderators ili kuwa na monitoring ya karibu ya post za watu. Hatuna haja ya kutukanana na kutumia lugha za kejeli. Siku hizi majina kama mburula, kima, nyani, mjinga, --------, Ms$ng3 ni order of the day. Tunapashwa tujenge utamaduni wa kuheshimiana hata kama haujafurahia mchango au mawazo ya mwenzako. JF bado ina nafasi ya kukua na kuwa na faida zaidi ya sasa, tuwaunge mkono waanzilishi.
Nawatakia maandalizi mema ya Xmas na mwaka mpya 2014.
Tiba