Hakuna kitu kama hicho, sheria hazijahalalishwa kwa wanajeshi kuwadhuru raia, na kama ikitokea basi wanashitakiwa kama raia wa kawaida au kupitia mahakama yao ya jeshi..
Kuna hii kesi ya mtoto wa Fundikira, ambapo walizidisha kipigo wakaua mtoto wa watu, mbona walishitakiwa?
Wanajeshi walioua kizimbani leo
Hayo uyasemayo basi tutafika wakati hata kupishana na mwanajeshi akitembea kwa miguu issue, baiskeli balaa, bodai boda au bajaj ndio tusigune na gari ndio watufunge kabisa.
Jeshi lina maadili yake mkuu, lakini sio kulidhalilisha na kuwapiga wananchi wake badala ya kuwalinda, naomba uulize..Hakuna kabisa kwenye manual au guide zao zinaposema pigeni raia mtaani mtakapowaona wamevunja sheria za aina yoyote ile, hizo ni zana za kizamani tulipokuwa tunawaogopa viongozi, askari, mashushu na viongozi wenginepo, tusipojua hawa watu wapo kwa ajili yetu sisi, kutuhudimia na kutulinda, na kwamba ni raia kama sisi, na sio miungu..
Acha dhana potofu na zitakazoliabisha taia na kusahau kuwa hakuna wafanyakazi nchini wanaofuata maadili kama jeshi la wananchi na jeshi la polisi...