Wanajeshi wamenipiga mbele ya mke wangu

Wanajeshi wamenipiga mbele ya mke wangu

ilikuwa juzi kwenye heka heka za kusheherekea pasaka mimi na demu wangu.

Maeneo ya barabara ya chuo kikuu (udsm) inayoelekea changanyikeni nikawa nimepaki gari pembeni kidogo na barabara siku ipaki pembeni kabisa kiukweli kwa namna fulani nikamuacha demu wangu mi nikaingia sehem (hillpark) kununua vocha pamoja kumtumia mtu hela, nilipo maliza nikawa natoka nje nikakuta lile gari kubwa kabisa la jeshi limesimama nyuma ya gari yangu halafu kuna wanajeshi wawili wapo kwenye gari yangu wanaongea na wife wakimuuliza mwenye gari yupo wapi namimi nikawa natokea akasema huyo hapo... Mamamamaaaaaaaa............... Kabla hawajaniuliza kitu walinipokea kwa makofi na vibao, walinipiga sana kwa kweli, sikuweza kupigana nao hata kidogo kwasababu kuna wengine walikuwa wametulia tu kwenye gari lao. Mke wangu alishuka kuamulia waniache hawakumpiga lakn walimsukuma akadondokea mkono wa kushoka umeteguka.

Namshukuru sana mungu, akashuka mwanajeshi mwingine sijui ni boss wao akawaambia waniache ndipo wakaondoka.

Mke wangu amewekewa muhogo mkononi huku mimi naugulia tu maumivu, nimeaibika sana mbele ya mke wangu japo naona aibu lakni najifanya uso mkavu kama ndimu.

wewe unastaİlİ kuchapwa mke wako unamwita demu kwelİ kichapo kinakufaa.
 
Kwa akili ya kawaida tuchukulie wewe Dina ni mwanajeshi na unawahi kwenda kazini au ulilala zamu ukilinda taifa halafu unamkuta mtu Mtu jamii ya SUPU YA MAWE kapark gari lake barabarani je utakaa usubiri arudi na akisharudi toka zake shopping umwambie jamani wewe raia siyo vizuri kupark barabarani na kukwamisha magari mengine, kwa hiyo SUPU YA MAWE husirudie vinginevyo unavunja sheria. Haya ondoa gari lako na sisi tupite jamani SUPU YA MAWE halafu akishaondoa gari na wewe mwanajeshi upate ruhusa ya kuondoka. Je ungefanya hivyo Dina kama ungekuwa ni mjeshi?
Bado swali litabaki kuwa hiyo ni sahihi kwa kuvunja sheria za barabarani? Makofi kwa mtu mzima yanadhalilisha jamani... Hata hao watoto tumeacha 'kuwazibua' makofi kwa hofu ya kuwatia uziwi...
 
Ulivuna Ulichopanda, Pole Ila Usirudie Tena, Cku Ukimpiga Mkeo Atakutishia Kuwaita Hao Jamaa
 
ningekuwa mimi ni live or die, siwezi ogopa mtu eti kisa ni mjeshi, ningepigana nao hata kama wangenipiga ila sio eti nitulie tu wanipige
Ilikuwa juzi kwenye heka heka za kusheherekea pasaka mimi na demu wangu. Maeneo ya barabara ya chuo kikuu (UDSM) inayoelekea changanyikeni nikawa nimepaki gari pembeni kidogo na barabara siku ipaki pembeni kabisa kiukweli kwa namna fulani nikamuacha demu wangu mi nikaingia sehem (hillpark) kununua vocha pamoja kumtumia mtu hela, nilipo maliza nikawa natoka nje nikakuta lile gari kubwa kabisa la jeshi limesimama nyuma ya gari yangu halafu kuna wanajeshi wawili wapo kwenye gari yangu wanaongea na wife wakimuuliza mwenye gari yupo wapi namimi nikawa natokea akasema huyo hapo... mamamamaaaaaaaa............... kabla hawajaniuliza kitu walinipokea kwa makofi na vibao, walinipiga sana kwa kweli, sikuweza kupigana nao hata kidogo kwasababu kuna wengine walikuwa wametulia tu kwenye gari lao. Mke wangu alishuka kuamulia waniache hawakumpiga lakn walimsukuma akadondokea mkono wa kushoka umeteguka. Namshukuru sana Mungu, akashuka mwanajeshi mwingine sijui ni boss wao akawaambia
 
Kama nitakuwa ni mimi japo mimi nazijua sheria za barabarani na siwezi kufanya hivyo hata siku moja ila kama ningekuwa nimefanya hivyo japo siotei kufanya hivyo basi ningekaa kimya maana nilichofanya ni kosa la na pili kama nimepigwa mbele ya mke wangu ni dhahiri mimi mwenyewe nimejidhalilisha kwa kuvunja sheria na kama ni mtoto wangu atakuwa amejifunza somo
Wewe ungekuwa ni wewe na kama mwanasheria na umbebe mke wako na na kumwacha katikati ya barabarani au uzibe barabara na umwache kwenye gari halafu uchepuke kwenda kwenye manunuzi yako je kuna busara hapo? Na je ungerudi ukute ndio hivyo gari la jeshi limesimamishwa kwa kupark vibaya na likashindwa kupita ungesemaje, ungeomba samahani uondoe gari? Ungesema nimevunja sheria nipeleke tarafiki? Au ungesema ni kawaida yangu japo sheria nazijua?
How would you feel ukiwa umefanyiwa ivi wewe?
How would you feel kitendo hichi akafanyiwa mtoto wako tena kipigo hicho kikampelekea kupata madhara makubwa ya mwili?
 
Kama nitakuwa ni mimi japo mimi nazijua sheria za barabarani na siwezi kufanya hivyo hata siku moja ila kama ningekuwa nimefanya hivyo japo siotei kufanya hivyo basi ningekaa kimya maana nilichofanya ni kosa la na pili kama nimepigwa mbele ya mke wangu ni dhahiri mimi mwenyewe nimejidhalilisha kwa kuvunja sheria na kama ni mtoto wangu atakuwa amejifunza somo
Wewe ungekuwa ni wewe na kama mwanasheria na umbebe mke wako na na kumwacha katikati ya barabarani au uzibe barabara na umwache kwenye gari halafu uchepuke kwenda kwenye manunuzi yako je kuna busara hapo? Na je ungerudi ukute ndio hivyo gari la jeshi limesimamishwa kwa kupark vibaya na likashindwa kupita ungesemaje, ungeomba samahani uondoe gari? Ungesema nimevunja sheria nipeleke tarafiki? Au ungesema ni kawaida yangu japo sheria nazijua?
Unadhani adhabu za waenda kinyume wa sheria za barabarani zilizowekwa/kutungwa, zilikosewa?
 
hao jamaa, kuna mfumo nwameanzisha wa kuwachapa fimbo makonda watakaosimama ovyo eneo ambalo si kituo halali, juzi nilishuhudia konda na abiria wakichezea fimbo za maana kwa kuparking sehemu isiyo halali, hivyo basi na wewe umepata haki yako, halafu usiseme wamekupiga hao wamkegusua sema uso wako laini umeumuka, hao jamaa wakikufungia kazi hata usingekuja kupost hapa, maana mikono ungekuwa huna. ila poleee, tumia majani ya mnyaa kujikanda.
 
Kwa akili ya kawaida tuchukulie wewe Dina ni mwanajeshi na unawahi kwenda kazini au ulilala zamu ukilinda taifa halafu unamkuta mtu Mtu jamii ya SUPU YA MAWE kapark gari lake barabarani je utakaa usubiri arudi na akisharudi toka zake shopping umwambie jamani wewe raia siyo vizuri kupark barabarani na kukwamisha magari mengine, kwa hiyo SUPU YA MAWE husirudie vinginevyo unavunja sheria. Haya ondoa gari lako na sisi tupite jamani SUPU YA MAWE halafu akishaondoa gari na wewe mwanajeshi upate ruhusa ya kuondoka. Je ungefanya hivyo Dina kama ungekuwa ni mjeshi?

Mwananchi wewe hakika unanukia harufu ya 'mwanajeshi' nshakustukia.... Kwa utawala wetu wa sheria, basi angekabidhiwa kwa askari wa barabarani ili sheria ichukue mkondo wake...Lakini kwa kuwa hata huo utawala wa sheria haufanyi kazi, ndio maana hata Supu ya Mawe kaishia kuja kulalamika huku, kujiuguza na kumuuguza mwenza wake basi...

Na kwa vile wanajeshi nyie mnaamini katika kutumia maguvu na si akili (kumradhi kwa ukweli huu), basi mnaamini vibao na mateke ndio suluhisho lenu...Isije ikawa wa kupigwa kapigwa kwa hasira za mtu kulala zamu...
 
Mkuu Nameless girl naomba unisaidie kunifafanulia nini maana ya inchoate offences or crime labda mimi naielewa vibaya je huyu jamaa Supu Ya mawe yawezekana amefanya kosa ilo tukija kwenye upande wa sheria?
How would you feel ukiwa umefanyiwa ivi wewe?
How would you feel kitendo hichi akafanyiwa mtoto wako tena kipigo hicho kikampelekea kupata madhara makubwa ya mwili?
 
...ungekoki mashine,wote wangechuchumaa maana hawatembei na ngoma,ukiwazidi maarifa wanakuwa wapole...
 
Hukunijibu swali langu. Na hata ilo la kutaka apelekwe tarifi nilipendekeza. Kwa hiyo kwa maoni yako ulitaka bado waendelee kupoteza muda waite polisi waje kumchukua na kumpeleka trafiki ili apigwe faini? Na je unajua anaweza kukataa kulipa faini na akataka apelekwe mahakamani, je akishapelekwa mahakamani basi hao wanajeshi waitwe tena kuja kutoa ushaidi muda uendelee kupotea. Mimi ingawa siyo mwanajeshi kama unavyotaka kuniita adhabu aliyopewa ni mhafaka na najua hatakaa hata siku moja kurudia kosa ilo, na mimi namwona ni mtu mzuri maana baada ya funzo amejileta kwetu kutwambia ehee!! jamani msifanye makosa kama yangu vinginevyo mtaambulia adhabu kama niliyopata na kama wewe Dina ulikuwa na nia ya kufanya hivyo hutafanya hivyo kwa kupitia somo la Supu Ya Mawe
Mwananchi wewe hakika unanukia harufu ya 'mwanajeshi' nshakustukia....Kwa maelezo ya Supu ya Mawe, hakuwa amepaki barabarani. Na kwa utawala wetu wa sheria, basi angekabidhiwa kwa askari wa barabarani ili sheria ichukue mkondo wake...Lakini kwa kuwa hata huo utawala wa sheria haufanyi kazi, ndio maana hata Supu ya Mawe kaishia kuja kulalamika huku, kujiuguza na kumuuguza mwenza wake basi...

Na kwa vile wanajeshi nyie mnaamini katika kutumia maguvu na si akili (kumradhi kwa ukweli huu), basi mnaamini vibao na mateke ndio suluhisho lenu...Isije ikawa wa kupigwa kapigwa kwa hasira za mtu kulala zamu...
 
Kwa wrong parking uliyoifanya ulistahili kichapo, watu wanashughuli zao mnawakwamisha bila sababu!!!!
 
Ilikuwa juzi kwenye heka heka za kusheherekea pasaka mimi na demu wangu.

Maeneo ya barabara ya chuo kikuu (UDSM) inayoelekea changanyikeni nikawa nimepaki gari pembeni kidogo na barabara siku ipaki pembeni kabisa kiukweli kwa namna fulani nikamuacha demu wangu mi nikaingia sehem (hillpark) kununua vocha pamoja kumtumia mtu hela, nilipo maliza nikawa natoka nje nikakuta lile gari kubwa kabisa la jeshi limesimama nyuma ya gari yangu halafu kuna wanajeshi wawili wapo kwenye gari yangu wanaongea na wife wakimuuliza mwenye gari yupo wapi namimi nikawa natokea akasema huyo hapo... mamamamaaaaaaaa............... kabla hawajaniuliza kitu walinipokea kwa makofi na vibao, walinipiga sana kwa kweli, sikuweza kupigana nao hata kidogo kwasababu kuna wengine walikuwa wametulia tu kwenye gari lao. Mke wangu alishuka kuamulia waniache hawakumpiga lakn walimsukuma akadondokea mkono wa kushoka umeteguka.

Namshukuru sana Mungu, akashuka mwanajeshi mwingine sijui ni boss wao akawaambia waniache ndipo wakaondoka.

Mke wangu amewekewa muhogo mkononi huku mimi naugulia tu maumivu, nimeaibika sana mbele ya mke wangu japo naona aibu lakni najifanya uso mkavu kama ndimu.

Doh! Pole sana mkuu,kumbe ndo ww, mana kuna mtu aliandika uzi kuhusu mtu kupigwa na wajeda kwa kupaki vibaya,
 
Mkuu Nameless girl naomba unisaidie kunifafanulia nini maana ya inchoate offences or crime labda mimi naielewa vibaya je huyu jamaa Supu Ya mawe yawezekana amefanya kosa ilo tukija kwenye upande wa sheria?

Mkuu.. kwa mimi ninavyofahamu inchoate offences ni matendo ambayo si makosa kamili ila yanakua ni hatua moja wapo ya kuelekea kwenye kosa. Crime ni unlawful act ambayo ina adhabu yake.
 
Nafikiri Kituo cha Polisi kiko hatua chache toka eneo hilo. Ulitakiwa kutoa taarifa Polisi. Hilo ni 'shambulio la kudhuru mwili' na kwa sheria zetu linatoa adhabu nzuri tu.Hutakiwi kuwaachi hivihivi tu hata kama ulikuwa umefanya kosa.
 
Back
Top Bottom