Imebidi nikuone mwanajeshi kwa jinsi ulivyokuwa 'unahalalisha' adhabu ya Supu ya Mawe.....
Kitu ninachosisitiza mimi, ni kuwa kuna mtu hafanyi kazi yake ndio maana unaishia huko kutamani mwanajeshi apewe rungu. Kama utawekewa pipa la taka na kuambiwa ukitupa taka chini faini isiyo na swali kiasi kadhaa...lazima wote tutaenda sawa tu. Kwa nini tutumie faini, kwa sababu wengine toka walikotokea hawakuwa na utaratibu wa kutupa uchafu kwenye chombo maalum/shimo la taka. Kwa sababu tabia hiyo hana, basi na tumbane mahali mpaka aende sawa...Lakini aliyeweka pipa la taka naye anakuja 'kujishangaza' kuwa mbona takataka ziko chini!
Tukubali tumetoka mazingira tofauti na ulezi wetu ulikuwa tofauti. Kuna wengine wako kwenye gari ukiangalia abiria ni kama familia, yaani baba, mama na watoto. Lakini angalia hayo mauchafu yanayorushwa kutokea madirishani, sio chupa za maji, makaratasi ya ice-cream na kadhalika....utakuja kumlaumu huyo mtoto baadaye? Kwa hiyo haya yote yanaanzia chini, na ambaye alipishana nayo basi tumuwekee sheria. Na aliyeweka sheria na ahakikishe anaitumia kisawasawa, na iwe kweli kweli, siyo akiletewa kimemo na 'ndugu' wa aliyeivunja ailegeze...(hapa nimetoa mfano mmoja tu wa taka)
Lakini kwa vile mtekelezaji wa sheria hii naye amekuwa goigoi, ndio maana unaona suluhisho ni utumiaji wa nguvu. Na je, utumiaji wa nguvu utaupimaje? Kuna huyu wa leo wa vibao, atakuja mwingine wa mikanda na mabuti, au lupango (ndio, nilipita) kabisa?