Wanajeshi wamenipiga mbele ya mke wangu

Wanajeshi wamenipiga mbele ya mke wangu

Wanajeshi na ndugu zao askari/polisi wanatumia nguvu kuliko akili jitahidi kuwakwepa zaidi kuliko kukutana nao
 
Hakuna kitu kama hicho, sheria hazijahalalishwa kwa wanajeshi kuwadhuru raia, na kama ikitokea basi wanashitakiwa kama raia wa kawaida au kupitia mahakama yao ya jeshi..
Kuna hii kesi ya mtoto wa Fundikira, ambapo walizidisha kipigo wakaua mtoto wa watu, mbona walishitakiwa?

Wanajeshi walioua kizimbani leo

Hayo uyasemayo basi tutafika wakati hata kupishana na mwanajeshi akitembea kwa miguu issue, baiskeli balaa, bodai boda au bajaj ndio tusigune na gari ndio watufunge kabisa.
Jeshi lina maadili yake mkuu, lakini sio kulidhalilisha na kuwapiga wananchi wake badala ya kuwalinda, naomba uulize..Hakuna kabisa kwenye manual au guide zao zinaposema pigeni raia mtaani mtakapowaona wamevunja sheria za aina yoyote ile, hizo ni zana za kizamani tulipokuwa tunawaogopa viongozi, askari, mashushu na viongozi wenginepo, tusipojua hawa watu wapo kwa ajili yetu sisi, kutuhudimia na kutulinda, na kwamba ni raia kama sisi, na sio miungu..
Acha dhana potofu na zitakazoliabisha taia na kusahau kuwa hakuna wafanyakazi nchini wanaofuata maadili kama jeshi la wananchi na jeshi la polisi...

Mkuu mm nimewapiga wanajeshi wa tano na mkuu wao sema alikuwa mtu mzima nikamuacha nikawambia hapa sendi popote na gari yangu waliweka chini ya ulinzi wakaja polis ndio tukenda sote polis walikuwa wote wamelewa nimewashinda kwa point na elimu yao ya darasa la 7..Mkuu fanya mazoezi watakuu wanajeshi
 
Yaani kumbe ni wewe jamaa uliyekuwa umetuzuia kupita kwa kupaki vibaya halafu unakuja kutusema humu jf,ngoja tutakukamata tena
 
tii sheria kwa shuruti!pole sana siku nyingine hutarudia na ndo ukubwa huo.
 
Acha masikhara mkuu zile jezi ( bakabaka) wanacheza kareti moja inaitwa combat karet kazi ni kuvunja na kuua ashukuru walimpiga kistaarabu wange apply hiyo na hisi saiv tungeongea mengine!!!!!!!!

Combat kareti wapi wengi raia tu wanajivunia unform hebu kutananae akiwa hajavaa hiyo unform tuone watafanya nn! acha mawazo mgando
 
Ilikuwa juzi kwenye heka heka za kusheherekea pasaka mimi na demu wangu.

Maeneo ya barabara ya chuo kikuu (UDSM) inayoelekea changanyikeni nikawa nimepaki gari pembeni kidogo na barabara siku ipaki pembeni kabisa kiukweli kwa namna fulani nikamuacha demu wangu mi nikaingia sehem (hillpark) kununua vocha pamoja kumtumia mtu hela, nilipo maliza nikawa natoka nje nikakuta lile gari kubwa kabisa la jeshi limesimama nyuma ya gari yangu halafu kuna wanajeshi wawili wapo kwenye gari yangu wanaongea na wife wakimuuliza mwenye gari yupo wapi namimi nikawa natokea akasema huyo hapo... mamamamaaaaaaaa............... kabla hawajaniuliza kitu walinipokea kwa makofi na vibao, walinipiga sana kwa kweli, sikuweza kupigana nao hata kidogo kwasababu kuna wengine walikuwa wametulia tu kwenye gari lao. Mke wangu alishuka kuamulia waniache hawakumpiga lakn walimsukuma akadondokea mkono wa kushoka umeteguka.

Namshukuru sana Mungu, akashuka mwanajeshi mwingine sijui ni boss wao akawaambia waniache ndipo wakaondoka.

Mke wangu amewekewa muhogo mkononi huku mimi naugulia tu maumivu, nimeaibika sana mbele ya mke wangu japo naona aibu lakni najifanya uso mkavu kama ndimu.

Pole baba.

kwa hiyo pasaka ulipigwa mbele ya mkeo, uliyesema ana mkosi.

leo umefukuzwa kazi!


https://www.jamiiforums.com/mahusia...o-wao-lazima-ufukuzwe-kazi-2.html#post9331092



Mwanzo ummtaja kama demu wako, kwenye uzi huo huo ukasema mke!

Ushauri:

Kama ni demu tu, mmpige chini. Juzi upigwe, leo ufukuzwe kazi............. unasubiri kifo? kitakujia hivi punde..................
 
Akili kidogo nguvu nyingi!

Acha matusi mkuu,,,mi jamaa nawapenda sana. Hua wanafanya ubabe wao kwa wanaojifanya wababe pia, ila ukitii wala hawana shida na wewe. Mungu ibariki JWTZ
 
Pole mkuu...ila inabidi iwe fundisho kwetu sote manake wabongo Kila mahali ni kupaki tu, Na ningefurahi kama hao wanajeshi wangekua wanashighulikia wale wazee wa kutanua tanua na kujifanya tuna haraka kuliko wenzetu... I hate hizi tabia zetu unakuta jitu zima limesimamisha gari barabarani linaongea na simu au limepaki kabisa, kwa nini usitafute mahali pembeni kabisa? na wale watanuaji... hakyanani wananikera basi tu sina uwezo wa kuwashughulikia
 
Acha matusi mkuu,,,mi jamaa nawapenda sana. Hua wanafanya ubabe wao kwa wanaojifanya wababe pia, ila ukitii wala hawana shida na wewe. Mungu ibariki JWTZ

mfano wanapokwenda kuwapiga traffic si akili ndogo nini?lazima uwapende kama unafanya shopping kwenye yale maduka yako
 
Ila kituo cha police kipo pale pale kaka, wakati mwingine tukiwa na vimwana basi tutajibu vibaya mpaka basi
 
Mbona ss tuko nao mitaani huku tunakula nao maisha bila shidaa, kwani nyie inakuagajee
 
hahahaa, yaani nimecheka sana, pole kwa maumivu. Wajeda tena ukute waliotoka kozi siku za karibuni, wanatoa kipigo kwa raia wenye makosa ni heshima kwa boss wao!!

Tujifunze matumizi bora ya barabara

SP
 
Ha ha ha !!! Sipendi kama nini mtu anapark gari barabarani ! Unaleta usumbufu usio wa lazima kwa watumiaji wengine wa barabara ! Naomba kuuliza ulikuwa na demu wako au mke wako, maana sikukuelewa!
 
Back
Top Bottom