JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,458
Wanafunzi watatu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) wamefariki Dunia na wengine watano wamejeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea Juni 4, 2022 jioni katika moja ya barabara zilizopo chuoni hapo.
Ofisa Uhusiano wa chuo hicho, Beatrice Baltazar amesema ajali hiyo imetokea jana Juni 4, 2022 saa 2.00 usiku.
Amewataja waliofariki kuwa ni Hana Meshack, Zira Mpenda na Mpeli Mahenge.
Amewataja waliojeruhiwa kuwa ni Fortunata Kingazi, Fibi Julius, Sifa Shora, Enica William na mwingine aliyetajwa kwa jina moja la Furahina.
Amesema majeruhi wa ajali hiyo wamelazwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa na hali zao zinaendelea vizuri.
Taarifa zinasema wanafunzi hao walikuwa wanatoka katika mahafali ya dini yaliyokuwa yakifanyika chuoni hapo.
Baada ya kuulizwa kuhusu tuko hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno amesema: "Ni kweli hiz?o taarifa ni za ukweli, ninaandaa taarifa nitaitoa baadaye kidogo."