Mkuu kama umekuwa msomaji na mpitiaji mada humu hizo topic hata za kusema au kuelimishana mambo kama hayo hazipo siku hizi ni majanga tuu humu kwa sasa na sana sana tunaishia kulishwa magarasa tuu ya thread ambazo unajiluza hapa niseme nini sasa
ni kweli kuna mada humu zinakuwaga hazina mashiko , mpaka kuna siku nilishawahi kuandika mtu atakuja kuomba ushauri hata kiatu kikimbana,,,,,,,,,,,, msingi wa hoja zangu mimi umeegemea hapo kwenye suluhisho lako ulilolipendekeza........
ngoja nitoe mfano labda,,,,,,,,, kukiwa kuna mada unaiona imekaa kipuuzi/kitoto unapita tu , na unaelekea kwenye mada iliyonamashiko mnaijadili mwanzo mwisho mwisho wa siku watu watajifunza kuleta mada nzuri na kuachana na mada zisizona kichwa wala miguu.........ila hili la kuanzaa kuwa polisi na mahakimu na wachangia mada hapo hapo jukwaani halifai,,,,,,,,, tujifunze kuvumiliana huku tukifundishana na siyo kutumia mamlaka tuliyonayo au kutaka watu tuwe na ufikiri wa aina moja.
kama mada imekiuka sheria za jf , hatua zichukuliwe mara moja ila kama haijakiuka ni vema tujifunze kuishi na tunaotofautiana.