Wana MMU tushirikiane kuboresha Jukwaa letu

Wana MMU tushirikiane kuboresha Jukwaa letu

Status
Not open for further replies.
AshaDii umeongea na naomba nimwambie tena Husninyo hatuna nia ya kumtaja mtu wala kutaja thread ambazo zinaonekana kabisa hazina mshiko ila mwenye uelewa ataelewa tunamaanisha nini tunapoongea haya na sio kwa faida yang au yako ila kwa faida ya wote ambao ni member wa hili jukwaa na jukwaa jingine lolote.
Nia haswa ni kujua kuwa tunaingia hmu kufundishana na kupata uelewa wa mambo mengi na kujua hata kama niko mtaani ni wapi nimeenda wrong na wapi nirekebishe sio kwenda tuu kama kuku aliyekatwa kichwa

kuna watu upeo wao ni mdogo na hawajui kama wanakwaza watu. vizuri basi wawe wanaambiwa hata kwa pm basi.
 
Last edited by a moderator:
Avemaria ukichakachua thread ya mtu bado unaongeza comments kwenye thread yake na hapo ndo unaikuta iko page ya 10 kutokana na watu wataacha kuchangia mada wataanza kuchangia ule uchakachuzi

Mkishamaliza mniambie nikaanzishe thread. Kuna binti kamwambia bibi yenu kuwa ananipenda.
 
Last edited by a moderator:
Ohh plzzzzz Lara, Kaunga ni mdada ninaeenda nae sambamba sana humu jukwaani, napenda michango yake haswaa, na hajawahi kunikera hata kidogo na kuna watu na watu ninaweza kupishana nao maneno humu ndani na nikaingia PM kuwekana sawa na mambo yakasonga, mmoja wa watu ninaoweza kufanya hivyo ni Kaunga, soo plz hausiki hapa hata kidogo! namheshimu Kaunga sana sana! ohh yes ni mada uliianzisha wewe! na sichukii mada zako kabisa, hayo ni maoni yako wewe, huyo mdada/mmama ndio alienikera kwa kufanya kukutetea kwamba anakujua kiuhalisia sijui haupo hivyo, na blah blah, jamaa aliekukosoa labda hamjuani/fahamiani haruhusiwi kukukosoa? kuna wanaokukosoa wengi humu na unawaweka sawa, sijaona tatizo hapo, ishu ni huyu mama kuingilia, ungejibu wewe kama nilivyozoea kukusoma ukiwajibu isingenipa shida hata kidogo.
Basi itakuwa Ticha ! Manake ndo hao tu wananiteteaga! Ila alisema vile coz mtu alinitukana mimi personally sio mada of which was not fare too. Hakusema mada anaiunga mkono but mtoa mada mitusi sikuistahili. Lol!
 
Avemaria ukichakachua thread ya mtu bado unaongeza comments kwenye thread yake na hapo ndo unaikuta iko page ya 10 kutokana na watu wataacha kuchangia mada wataanza kuchangia ule uchakachuzi
Mr Rocky
Sidhani kama kuna threads zote zitaondolewa kwa mantiki kwamba hazina mashiko.
 
Last edited by a moderator:
ila mi nasema aunt msiseme ni under 18. kuna watu wazima humu ila akili za kitoto na wapo watoto wamekomaa akili. best optn ni kuwaelimisha tu badala ya kuwashambulia hao. halafu nimekumiss kiukweli ukweli.
Husninyo:Hapo tu mimi...hoiii.Kweli hizi mada zenye mashiko zina wenyewe....LOL.
 
Last edited by a moderator:
Mie siku hizi namaliz hadi siku nne na kuendelea na bado nikiingia nakuta hakuna cha maana,kiukweli kuna watu ambao wako na vipaji vya kuweka post zenye kujenga lakini wametokomea kusikojulikana matokeo yake kina asnam ndo tumetake over na kuweka udambu udambu wetu.
 
MC Umeongea vitu muhimu sana ktk kuboresha hili jukwaa!
Thanks!
Lakini umeegemea sana, sana, sana kuwatetea memba wakongwe!!!! Ni kweli memba wapya hujisahau sana! Ila memba wakongwe wanaongoza kwa kuchati!!!!!
Vile vile, wanadharau ya hali juu! Ngoja nikupe mfano hapa! Unamkuta kwa vile yeye kajiunga mapema, bila shaka ameshaona mada nyingi zikijadiliwa, hivyo basi akikuta mada yenye content kama ile, badala ya kutoa mchango unaufaa (hata kueka link) yeye anakejeli na kujiona anajua kila kitu! This is not fair!!!!!!!
...

Umeongea ya msingi sana... Na nimefupisha post but nimekusoma yote.

Mashaxizo, hata siku moja usikubali kuonewa or to feel inferior kwa member sababu tu eti ID yake inaonekana ni kongwe. Inawezekana akakuzidi katika matumizi ya Jukwaa kulifahamu vizuri, but linapokuja suala la mjadala kila mtu ana haki yake ya kujadili mradi haivunji sheria za Jf. Pamoja na uhuru huo, kuna wale wanao tumia uhuru huo vibaya kwa kuweka vitu ambavyo havina tija na wala havijadiliki.

Pia naomba nigusie dhana ya ukongwe... Naona hapa inachukuliwa tafsiri mbaya. Ambayo hata mimi sijapenda. Tunapozungumzia MMU kwa mada za kujenga, tunazungumzia kuwa hapo nyuma mada nyingi zilikuwa za kujenga (si kwamba sasa hivi hakuna... Zipo ila kwa uchache sana hivyo kumezwa na zile ambazo hazina maana wala kutojenga).

Members wengi wa hapo nyuma wamepotea, hivyo katika harakati za kurudisha jukwaa katika hadhi ya pale nyuma inakuwa tu kuhimizana wale waliokuwepo wakongwe na wamepotea waanze tena kushiriki. Kumbuka kuwa hata hao the so called wakongwe walikuwa ni members wapya at one time.
 
kuna watu upeo wao ni mdogo na hawajui kama wanakwaza watu. vizuri basi wawe wanaambiwa hata kwa pm basi.

Zamani tulikuwa na kampeni. Thread ya kitoto tunaipotezea mazima. Kama hakuna thread ya maana basi tunachagua thread moja ya kitoto tunanachakachua kwa kupeana michongo ya ulabu na kusalimia.

Siku hizi hata thread za kitoto unakuta watu wako bize kutoana mapovu. Watoto wakiona hivyo wanafurahi na kuzidi kumimina mithread yao.

Mi huwa nakasirikaga na kujikuta nimezimia kwenye jukwaa la wakubwa.
 
ila mi nasema aunt msiseme ni under 18. kuna watu wazima humu ila akili za kitoto na wapo watoto wamekomaa akili. best optn ni kuwaelimisha tu badala ya kuwashambulia hao. halafu nimekumiss kiukweli ukweli.


My favourite niece... Upo sawa kabisa! Na ndio mana wana jajiwa kwa mada zao. Mtu yupo over 30 huko akili anayowasilisha hapa ni as if yupo 16. Hapo hapo tambua kuna members wadogo sana humu jamvini.... But michango yao ipo so positive kiasi kwamba ukija kujua umri wake unashangaa kuwa yupo that young and so much wise.
 
Zamani tulikuwa na kampeni. Thread ya kitoto tunaipotezea mazima. Kama hakuna thread ya maana basi tunachagua thread moja ya kitoto tunanachakachua kwa kupeana michongo ya ulabu na kusalimia.

Siku hizi hata thread za kitoto unakuta watu wako bize kutoana mapovu. Watoto wakiona hivyo wanafurahi na kuzidi kumimina mithread yao.

Mi huwa nakasirikaga na kujikuta nimezimia kwenye jukwaa la wakubwa.

Kabisa.
Mpaka limada lake la hovyo linapoteza muelekeo!
 
Kila kitu kilichofanyika 'zamani' kilikuwa kizuri, zamani tulikula vizuri, zamani tulivaa vizuri, zamani tulikuwa na muziki mzuri, zamani tulijadiliana vizuri, zamani tulikuwa na viongozi wazuri, zamani maisha yalikuwa mazuri, zamani forum ilikuwa inanifanya, n.k. Inaonekana basi ni tatizo la wakati sio watu.
 
Zamani tulikuwa na kampeni. Thread ya kitoto tunaipotezea mazima. Kama hakuna thread ya maana basi tunachagua thread moja ya kitoto tunanachakachua kwa kupeana michongo ya ulabu na kusalimia.

Siku hizi hata thread za kitoto unakuta watu wako bize kutoana mapovu. Watoto wakiona hivyo wanafurahi na kuzidi kumimina mithread yao.

Mi huwa nakasirikaga na kujikuta nimezimia kwenye jukwaa la wakubwa.
kweli babu mi pia wananiuzi na juzi bado kidogo nivunje mozilla firefox yangu kwa hasira. kama vipi hizo mada zisichangiwe.
 
Polee sana kwa kuku disappoint Lara. Kwa post hii ndio nime note kuwa hukujua mie ni mtu mzima sana (kuzeeka as you call it) sipo enzi zenu kama ulivyo dhani. Ndio mana unakuta katika mambo mengi tunaweza kuwa tofauti mana mitazamo imetofautiana.

Naomba pia nikusahihishe... Lara, it seems you are sensitive sana na kuwa you would think this is about you - una mwaka mzima hapa JF with this ID; You do not qualify ugeni, na wewe ni mkongwe. Na from this post ina insinuate kuwa mada zako waona ni moja ya categories... Yawezekana wapo wanao ona hivyo na chache ya threads zako zaashiria hivyo, ila it won't be the truth kusema mada zako hazipo insightful. Huwa unaleta hoja zako na wazitetea why you see so! That is how a discussion is presented.

Hivi huwa unapita mada zingine hapa MMU? Ina maana hujawahi ona kuwa kuwa kuna tatizo la kukithiri mada za kitoto?

Sina shida wewe keeping a close eye on me. It's an honor... Mie tena naomba kila unapo pingana na mimi tell me so; for its learning in progress.

If it is abt me on not is not the issue at hand! Mi tatizo naliona ila SULUHISHO LENU LA REPORT ABUSE SIO SULUHISHO!!!!!!"""

I am just challanging you Asha n company mje na SOLUTION APPLICABLE!

Report abuse!!!!!!!!!!! Hahahaaaaaaa!
 
nashukuru mkuu Mr Rockykwa kutukumbusha yaliyo mema kwa mustakabali wa jukwaa letu , kwani kumekuwa na mada nyingi tu za ajabu ajabu humu. kimsingi nakubaliana na hoja zako nyingi za kujenga sana ili kupunguza uvamizi wa hili jukwaa letu. ila kunabaadhi ya mambo ambayo naomba kutofautiana na wewe.

2. Tujitahidi kurusha mada za kujenga na sio kubomoa au kumkomoa fulani au kuonyesha madhaifu fulani ya jamii yetu kwa kila atakae weza.
4. Kuondoa dharau kwa Mwanamke na Mwanaume pia. Mada za kusanifu Mwanaume ama Mwanamke hazijengi, zinabomoa tu.
5. Tujitahidi kuangalia pande zote za mijadala, isiwe vitu negative tu. Mfano sasa hivi kila inapokuja mada inayohusiana na ndoa huwa ni ya kukatisha tu tamaa, hata wale ambao hawapo kwenye taasisi hiyo hukatishwa tamaa kwa kukuza negatives tu na hali kuna positives pia kwa upande wa ndoa na sio kila ndoa ni majangaa au ina matatizo wapo wenye raha na furaha kwa ndoa zao

1. hapo namba 2 sidhani kama kujadili madhaifu ya jamii yetu kama ni sehemu ya kubomoa jamii , mimi kwa maoni yangu kujadili au kujua madhaifu yangu ni sehemu ya kunijenga.

2. hapo namba 4 ni kweli kuleta dharau na kejeli kwa jinsia nyingine haifai , ila kwenye mijadala kama hii ya kimahusiano utofauti wa wanaume na wanawake ni lazima utajitokeza kwani hata namna ya kufikiria na kutatua matatizo mbalimbali tumetofautiana pia.

3. hapo kwenye namba tano ni kama unataka watu waongee kuelekea mlengo mmoja ila kwa lugha tofauti ,,,,, hata kwenye debate yoyote mjadala kunakuwa na wanaokubaliana na mada na kunakuwepo wapinga mada........

hivyo mjadala wowote ukiletwa hapa ni jukumu la mkubalia na hoja kuitetea na ni jukumu la asiyekubaliana na mada kutoa hoja za kupinga........ mfano hapo kwenye ndoa huwezi kumlazimisha mtu aione ndoa kwenye positive perspective wakati sehemu kubwa ya maisha ya kwenye ndoa ameteseka , ,,,,,,,,, kwa maoni yangu ni kuwa mada ziwekwazo humu ziwe na mashiko tu , na watu wachangie kulingana na msimamo wa kila mmoja wetu.
 
Last edited by a moderator:
hahahha, kumbe na wewe unamjua hamisi, basi naomba ufikishe ujumbe. sio hapa lakini. hii thread nimeipenda kweli, leo sibanduki hapa.

Nisipomjua Hamisi ntamjua nani tena!!!!!!!Ujumbe umefika

mi nafatilia kwa makin maana kuna mda nakuwaga bored sana nikiingia hum

sa hivi nimetafuta majukwaa mengine ya kwenda.........
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom