Wana CCM acheni unyonge - Kikwete

Wana CCM acheni unyonge - Kikwete

eti waachw unyonge....wizi wanofanya wa kura police wao...bado wanyonge kweli hawa?
 
Amani haiwezi kulindwa kwa kuwachonganisha watu. italindwa na sheria. Haiwezekani Kiongozi mzima tena raisi ulopoke na watu wakuache unaendekeza ujinga. Nivizuri atumie akili na busara.
hizo akili na busara atavitoa wapi?
 
Naunga mkono kauli ya JK, ccm kama ilivyo kwa raia wengine wana haki ya kujilinda. Ningeshangaa kama JK angesema ccm wawe wanyonge. Kazi ya kujilinda sio jukumu la polisi ambao ni wachache kukidhi mahitaji, ni kazi ya kila chama na kundi la watu wenye nia moja njema. Kwanza JK kachelewa kutoa hii kauli kiasi cha watu kupoteza maisha kwa unyonge. Baba aliniambia usichokoze ila ukichokozwa na mchokozaji akadhamilia kukujeruhi, usiwe mnyonge. Pigana naye then baba yake na mimi tutakaa kuongea nakumaliza.

Hongera JK, tuko nyuma yako.



Nafikiri mgojwa ukimwi midadi ya uchama ndiyo inakuongoza. Fikiria kila chama, makundi ya kikabila, dini na wengine wakihamasisha waondoe unyonge na kukubiliana na wengine. Nchi hii itakwenda wapi? Fikiri kwa makini huyu ni rais wa watanzania wote. Cio CCM tu.
 
Jk sio mtu coz hana utu alisha leta ishu mbali mbali za ubaguz mfano watu wakaskazin kutopata mdaraka,na sasa anaendeleza ishu za kutugawa watz nadhani angependa kuona tz inaingia katika machafuko makubwa mfano ya kidini na ukanda pia kisiasa
 
Ccm ni hatari sana,mimi nlikuwa kata mojawapo siku ya uchaguz mdogo tarehe 9 mwezi watu walipigwa sana na kundi la vijana ambao inasemekana ni walinzi wa chama.
Kwa kauli hii ya mh rais watu watachinjwa mchana kweupe.
Mungu aepushe haya
 

viva rais wetu...

viva mwenyekiti wetu....

tunaukataa unyonge kwa nguvu zetu zote... kwa mioyo yetu yote na kwa akili zetu zote...

binadamu ana kikomo cha uvumilivu na hatuwezi vumilia madhila makubwa namna hii yawapate wenzetu

nilimwambia Baba V kuwa safari hii KALENGA ccm hatutakuwa wanyonge....

Vipi kama wanao nyumbani watakuambia baba/mama unyonge sisi sasa baci utawaelewa wanamaanisha nini? Utafurahia au utachukua hatua kukemea? Fikiri kwa makini usiurupuke tu kupongeza kauli za hovyo
 
Last edited by a moderator:
me nadhani safari za mara kwa mara zimemchosha akili. uwezo wa kufikiri unapungua sana.

Nadhani Rais anamajukumu mengi sana ya chama na serikali kwani kote mambo hayaendi vizuri Serikalini viongozi wanajihusisha na mauaji ya tembo faru chui nk, kashfa za mihadarati, serikali kutokuwa na ukwasi
Kwenye chama kuna mambo kama hayo ya watu kutakaka kuanza kampeni za urais kabla ya muda, baadhi ya viongozi wenzake kutokuwa na furaha haswa kuhusu sakata la mawaziri..... Hivyo Rais lqzima atakuwa mtu mwenye stress tu kwani kila jambo linamsubiri yeye atoe kauli au maamuzi
 
Ameidhinisha piga nikupige jino kwa jino
Bila kufuata tatatibu za kisheria
Anaungana sasa na waziri mkuu aliyesema "utapigwa tu"
Ni kiashirio kwamba uchaguzi ujao kutakuwa na vipigo kwa sababu kibali kuacha unyonge kimetolewa rasmi.

Hapana Huyu amenganabna Bwana ustaadh Ilunga Kapungu. Kuna kitu inaitwa ALKUM KISASI
 
Amano haiwezi patikana kwa kuagiza watu walipe kisasi....tumia akili ndugu sio unawaza kama uko MSALANI....

Ametaka tu kusisitiza kauli ya shehe Ilunga Kapungu. ALKUM KISASI ndugu watukufu wa............
 
Last edited by a moderator:
Nafikiri mgojwa ukimwi midadi ya uchama ndiyo inakuongoza. Fikiria kila chama, makundi ya kikabila, dini na wengine wakihamasisha waondoe unyonge na kukubiliana na wengine. Nchi hii itakwenda wapi? Fikiri kwa makini huyu ni rais wa watanzania wote. Cio CCM tu.
Jensene, kwahiyo unachosema mwenyeketi wa chama alitakiwa aseme kwamba wana chama wake wawe wanyonge wanapochokozwa au kutolewa macho, ati kwasababu yeye ni rais? Yeye ni mwenyekiti kwanza kabla ya urais na a lion gear kwenye mkutano wa chama chake. Akina Lipumba walipokua wanasema watakuwa ngangari au Slaa aliposema nchi haitatawalika mbona walieleweka bila chenga? Ukweli hauchagui wala kuchaguliwa msemaji.
 
Hiyo kauli ingetolewa na kiongozi yeyote wa chama cha upinzani ingechukuliwa ama kutafsiriwa kuwa ni uchochezi na inahasisha kuvunja amani, Inashangaza mno rais na mkuu wa nchi anadiriki kuhamisha vurugu na matendo maovu kwa wananchi wake,

Kwa kauli kama hiyo inanifanya niamini kuwa hata yanayosemwa na Wanyarwanda yanaweza kuwa na ukweli
 
Mungu anaona haya yote, anajua mipango yao yote, anajua njama zote, na anajua jinsi ya kuwaepusha watu wake, kilichopangwa na Mungu binadamu hawezi kupangua.
 
Sikuwa karibu na Runinga, ila nilipofika nyumbani binti yangu akanieleza hakumuelewa Kikwete na kauli yake. Nikamuuliza kauli gani? Akaniambia amewambia ccm waache unyonge! wasitishwe na wapinzani, wagombee nafasi yoyote wanayotaka'.

Hii nchi JK haiachi salama, take my word! Nilishasema sisem wako tayari kua ilimradi wasalie madarakani. Hii haikubaliki. CDM nendeni jimbo la kalenga bila uoga. Wambie tume ya uchaguzi kuboresha daftari. Wambie polisi wasithubutu kulinda waiba kura, wasithubutu kuingilia kampeni za uchaguzi huo. Waandaeni green guard kulinda kura za wapiga kura. Nchi hii yetu sote....hakuna mwenye hati miliki ya uongozi. Ni box la kura linalohamua nani awe nani. si polisi, si jk, si mahakama. Ccm acheni haki ndiye awe mtawala.

Mkuu nimekusoma vizuri upo upande wetu wapenda haki. Ila CDM ina Red Brigerd na sio Green.
Asante.
 
JAKAYA Mrisho Kikwete, mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) taifa, anapaswa kushitakiwa kwa uchochezi.

Akifungua mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama chake mjini Dodoma leo, Kikwete alichochea wanachama wa CCM kuwapiga wapinzani kwa kudai kuwa, “Uvumilivu una kikomo.”

Amewataka wana CCM kuacha unyonge kwa madai kwamba wapinzani wamekuwa wakiwapiga huku wao wakisubiri polisi kuchukua hatua za kisheria.

Hii ina maana kwamba, Kikwete ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano, amewataka wanachama wa CCM, kuchukua sheria mkononi. Ametaka wananchi kuumizana, kupingana na kuuana. Huu ni uchochezi unaoweza kuingiza nchi katika machafuko ya kisiasa, kidini na kijamii.

Kama Kikwete alitaka urais, bila shaka alijipima na kujiona anaweza kufanya kazi hiyo. Kama alikuwa anajua anakwenda Ikulu kujaribu, basi alikuwa amekosea. Ikulu siyo sehemu ya kujaribu.

Kauli ya Kikwete ya kutaka wananchi wajibu mapigo, ni ishara kwamba ameomba kazi ambayo haiwezi.

Rais wa nchi hawezi kuchochea raia wake kupigana. Anapaswa kutumia vyombo alivyonavyo kusimamia sheria.

Ni lazima akumbushwe kwamba nchi hii ikiingia katika machafuko au mauaji ya halaiki, yeye ndiye atakuwa wa kwanza kuulizwa. Anaweza asiulizwe na vyombo vya sheria vya hapa, lakini ataulizwa na vyombo vingine vya dunia.
 
Chadema tunawatahadharisha mwisho wa kujifanya mnajua kurusha ngumi umefika.

Anzeni tena fujo muone.
 
sijaielewa hii kauli ya kikwete alikuwa anamaanisha nini.
ameyasema hayo wakati wa kikao cha NEC alipokuwa anazungumzia machafuko yanayotokea kwenye chaguzi ndogo especially ile ya kahama.
amewataka wana CCM kuacha unyonge. hapa nimeshindwa kumuelewa; anataka wana CCM wareact vipi? kwa kuua au?
na amejihami kwa kusema kwamba hata kama alichokisema kitakuwa ndio habari nzito kwenye vyombo ya habari sawa tu.

source: news, TBC1

Kikwete kwa kuropoka hovyo jamani kha! anajisahau kuwa yeye ni mkuu wa nchi anaanza kuwagawa watanzania
 
Back
Top Bottom