Wana CCM acheni unyonge - Kikwete

Wana CCM acheni unyonge - Kikwete

Hapa hatushindani kuorodhesha maovu wanayofanyiwa wafuasi wa vyama, kikubwa hapa ni kuwa JK kaongea kama RAIS na AMIRI JESHI MKUU.
Hao wanaofanya hayo maovu,
Hao wanaojiita Makamanda,
Hao wanaojiita Red Brigade,
Hao wote wanaongozwa na watu,

Watu hao ni Mbowe na Slaa Mkiti na Katibu wa Chama,

Washitakiwe hawa kwanza na wabunge kama Msigwa,Kasulumbayi na Lema hawa wamesababisha vifo,fujo na majeraha yasiyopona.

Mathalani watu wamekatwa mikono utamlipa nini masikini huyu kinacholingana na mkono wake? Kisa chadema.

Kuna watu Bugando wamenyofolewa Macho,utamlipa nini mtu huyo ili aone haki imetendeka? kisa Chadema.

Stahili ya mauaji,fujo,mapanga,Tindikali,uvamamizi na nondo ndio demokrasia?

Washitakiwe Mbowe na Slaa,Lema,Kasulumbayi na Msigwa ili haki ipatikane.
 
huyu mtu nasikia anatabia ya visilani visalani.....sasa asubili kwenda kule waliko kwenda akina ruto, kwa lolote litakalo tokea
 
Uongozi wa TBC ulishatoa taarifa serikalini kuwa mitambo yao ina tabia ya kubadirisha kauli za watu hasa viongozi wa juu, na kuwafanya wasikike tofauti na walivyoongea.
Hivyo basi tunapenda kuwahakikishia watanzania kuwa, rais hakupata kuongea kauli hiyo mahala popote, ni bahati maya kuwa tatizo hilo la kiufundi, safari hii limeathiri kauli ya rais.
Wizara imeshaongea na makandarasi kutoka China na Madagascar ambao wataingia muda wowote kuanzia mwezi October kwa ajili ya kushughulikia tatuzo hilo.
Tunawaomba radhi wananchi kwa usumbufu uliojitokeza baada ya kauli na maelezo ya rais kuharibiwa na mitambo.

Imetolewa na Kurugenzi ya mawasiliano hapa kwenye Magogo.

Mkurugenzi wa hayo mawasiliano.
Saa ya silva Rey na Mamuu.

hahaahaaaa
 
Wamutumia kila mbinu kuiangamiza chadema akini wameshindwa.
Bila shaka na hii itashindwa tu kwa mpango wa mungu!
 
Na Said Kubenea


JAKAYA Mrisho Kikwete, mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) taifa, anapaswa kushitakiwa kwa uchochezi.

Akifungua mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama chake mjini Dodoma leo, Kikwete alichochea wanachama wa CCM kuwapiga wapinzani kwa kudai kuwa, “Uvumilivu una kikomo.”

Amewataka wana CCM kuacha unyonge kwa madai kwamba wapinzani wamekuwa wakiwapiga huku wao wakisubiri polisi kuchukua hatua za kisheria.

Hii ina maana kwamba, Kikwete ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano, amewataka wanachama wa CCM, kuchukua sheria mkononi. Ametaka wananchi kuumizana, kupingana na kuuana. Huu ni uchochezi unaoweza kuingiza nchi katika machafuko ya kisiasa, kidini na kijamii.

Kama Kikwete alitaka urais, bila shaka alijipima na kujiona anaweza kufanya kazi hiyo. Kama alikuwa anajua anakwenda Ikulu kujaribu, basi alikuwa amekosea. Ikulu siyo sehemu ya kujaribu.

Kauli ya Kikwete ya kutaka wananchi wajibu mapigo, ni ishara kwamba ameomba kazi ambayo haiwezi.

Rais wa nchi hawezi kuchochea raia wake kupigana. Anapaswa kutumia vyombo alivyonavyo kusimamia sheria.

Ni lazima akumbushwe kwamba nchi hii ikiingia katika machafuko au mauaji ya halaiki, yeye ndiye atakuwa wa kwanza kuulizwa. Anaweza asiulizwe na vyombo vya sheria vya hapa, lakini ataulizwa na vyombo vingine vya dunia.

ndugu yangu kauli hii ya JK imenisikitisha sana.Nape alipotoa amri kwa green guard kupiga wapinzani nlisema katoa tamko baya hata hivyo " ni nape" alipotoa tamko waziri mkuu kuwa "wapigwe tu" nkasema ni kawaida yake na atatubu baadae kwa " machozi" .Sasa hii ya JK imenitoa usingizini na kumbe walikuwa vipaza sauti tu na mwenyekiti ndo kawatuma.Haya sasa kazi kwenu wana habari wana harakati na wana sheria
 
Hapana! Kujibu mapigo haipaswi kuwa justified unless we're a failed state which is far from being true. Ingawa sikupata nafasi ya kusikia alichokisema rais lakini sidhani kama tumeelewa kama alivyokusudia kueleweka. Sidhani kwa kuwaambia wana CCM wasiwe 'wanyonge' alimaanisha wapambane, nahisi alikuwa na maana wana CCM wasiogope kufanya halali kwa kuogopa nguvu ya upinzani kisiasa. Kama mwenyekiti wa CCM, si kama rais, ana jukumu la kuwatia moyo wanachama wake wafanye siasa za ushindani bila woga, bila mapambano ya nguvu. Siwalaamu wanaotafsiri kauli hii kama wito wa mapambano lakini siami ndivyo ilivyokusudiwa.

ni vema ukatafuta alichosema kwanza
 
Mbona hukusema haya wakati wana CCM wamechomewa nyumba, wamekatwa mikono na kutolewa macho huko kahama?

Mbona hukuwashitaki Mbowe na Slaa wanaotembea kwa chopper kushinikiza ngumi na mapanga kila siku?

Mchochezi ni nani? Umemwelewa JK we Kubenea au ni muendelezo wa majungu yako ya kukosa kuteuliwa nae tangu 2005?

JK hakumaanisha mapanga wala ngumi, na kama unapenda haki dhidi ya wachochezi basi faili la kwanza Mahakamani washitakiwe Mbowe na Slaa pamoja na wabunge wao kwa uchochezi na utekelezaji wa mauaji.

Nenda Bugando Mwanza ukawaone majeruhi ndo uje uandike makala yenye haki.

Kubenea unajiaabisha.
Hata wao chadema watakushangaa kama unasimama kuwatetea.

Ushahidi wa mwanzo ni namna wananchi walivyoamua kuwakataa kupitia kura na kuambulia kata 3, je unadhani hiyo ni kawaida?

Kubenea vua miwani ya ushabiki uitendee haki kalamu yako.
Tusitoke nje ya mada hapa,

Je hii kauli ya uchochezi kutoka kwa kikwete ni ya kuifumbia macho????
 
Aaah!! Kikwete ni Rais asiyejua madhara ya kauli zake. He's too weak to be the President.

But he is already The URT President what else would you like him not to become? Your argument is simply emotional transformations of your shame. Loading...........
 
ndio maana hadi j.makamba na ngeleja wanataka urais,kama huyu naye eti rais hawa watashindwaje..ikulu imekufa hadhi.
 
Hao wanaofanya hayo maovu,
Hao wanaojiita Makamanda,
Hao wanaojiita Red Brigade,
Hao wote wanaongozwa na watu,

Watu hao ni Mbowe na Slaa Mkiti na Katibu wa Chama,

Washitakiwe hawa kwanza na wabunge kama Msigwa,Kasulumbayi na Lema hawa wamesababisha vifo,fujo na majeraha yasiyopona.

Mathalani watu wamekatwa mikono utamlipa nini masikini huyu kinacholingana na mkono wake? Kisa chadema.

Kuna watu Bugando wamenyofolewa Macho,utamlipa nini mtu huyo ili aone haki imetendeka? kisa Chadema.

Stahili ya mauaji,fujo,mapanga,Tindikali,uvamamizi na nondo ndio demokrasia?

Washitakiwe Mbowe na Slaa,Lema,Kasulumbayi na Msigwa ili haki ipatikane.


Wewe unawafahamu kwa majina vizuri kabisa na matukio waliyofanya na watu walioathiliwa unawafahamu! Kwanini msiende kuwakamata hao akina Mbowe, Slaa, Lema, Kasulambaya , na Msigwa? Au km Wewe ni raia mwema Kwanini usitangulie mahakamani ukawafungulie kesi kutokana na matukio uliyo yaainisha? Mnashindwa nini na sheria zipo na dola ipo?
 
Na Said Kubenea



JAKAYA Mrisho Kikwete, mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) taifa, anapaswa kushitakiwa kwa uchochezi.

Akifungua mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama chake mjini Dodoma leo, Kikwete alichochea wanachama wa CCM kuwapiga wapinzani kwa kudai kuwa, “Uvumilivu una kikomo.”

Amewataka wana CCM kuacha unyonge kwa madai kwamba wapinzani wamekuwa wakiwapiga huku wao wakisubiri polisi kuchukua hatua za kisheria.

Hii ina maana kwamba, Kikwete ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano, amewataka wanachama wa CCM, kuchukua sheria mkononi. Ametaka wananchi kuumizana, kupingana na kuuana. Huu ni uchochezi unaoweza kuingiza nchi katika machafuko ya kisiasa, kidini na kijamii.

Kama Kikwete alitaka urais, bila shaka alijipima na kujiona anaweza kufanya kazi hiyo. Kama alikuwa anajua anakwenda Ikulu kujaribu, basi alikuwa amekosea. Ikulu siyo sehemu ya kujaribu.

Kauli ya Kikwete ya kutaka wananchi wajibu mapigo, ni ishara kwamba ameomba kazi ambayo haiwezi.

Rais wa nchi hawezi kuchochea raia wake kupigana. Anapaswa kutumia vyombo alivyonavyo kusimamia sheria.

Ni lazima akumbushwe kwamba nchi hii ikiingia katika machafuko au mauaji ya halaiki, yeye ndiye atakuwa wa kwanza kuulizwa. Anaweza asiulizwe na vyombo vya sheria vya hapa, lakini ataulizwa na vyombo vingine vya dunia.
Searching and looking for his name in Tanzania daima magazines but its always absent,

Because he is no body,just house negro of Dr.W.Slaa

He loves chadema more than he loves himself,

Trying to fool the mass that he is the grandson of nyerere,but gues what..!!,he is just stupid njaa kali and kanjanja lisilo na mbele wala nyuma.

Young boy u have to live yourlife now because there's no promise of a second time again,all what you have to do is just 'live'

Laiti chadema wangekuwa wana plan nawewe tokea pale ulipoanza kujikweza na kujichukulia nasaba ya nyerere na kuacha nasaba ya msambila ambae ni mzee wako mzazi,obviously wangekupa hata nafasi ya ufagizi pale ufipa,lakini ndio kwanza wanazidi kukupuuza,huoni kama unazidi kupoteza muda zaidi...!!

Njoo huku Mtwara tukupe mashamba ya korosho ulime,i think that will help you,mjini hapo pagumu sana na pameshakushinda usizidi kudhalilika
 
Last edited by a moderator:
ndio maana hadi j.makamba na ngeleja wanataka urais,kama huyu naye eti rais hawa watashindwaje..ikulu imekufa hadhi.
J.Makamba ameweza kufkia mafanikio makubwa kwa kipindi cha miaka minne, mama yako mzazi na baba yako mzazi hawajaweza hata kukuondoa wewe kwenye duara la umasikini kwa maisha yao yote. Rudi nyuma na uwe unafikiria chochote unachotaka kusema juu ya mtu aliyewazidi uwezo wazazi wako.
 
Tusitoke nje ya mada hapa,

Je hii kauli ya uchochezi kutoka kwa kikwete ni ya kuifumbia macho????

Hapana kabisa. Wanachosahau watu ni kuwa huyo sio tuu kuwa ni mwenyekiti wa chama chakavu CCM bali ni amiri jeshi mkuu wa Jamhuri ya Tanzania. Hiyo kauli yake inamaana hata Vyombo vya dola haviwezi kumchukulia hatua mfuasi yeyote wa CCM atakaye fanya vitendo kama hivyo kwa vile ni amri ya Amiri jeshi mkuu mwenyewe.
Huku kusema na kufikiri baadae kumewaponza wengi. Jee anajua kuwa wakina Kenyatta na Ruto kilichowapeleka The Hague ni kauli kama hizo hizo? Maana sasa hivi hao wafuasi wa CCM wakianza kushambulia watu na hao "wapinzani" wakaamua nao kujibu mapigo nchi haijaingia kwenye machafuko? Na endapo hayo machafuko yatatokea nani atapelekwa huko kujibu mashtaka?
Tatizo viongozi wa Afrika wanalalamikia mahakama hiyo wakati kauli zao hawazipimi kuwa ndizo chanzo.
 
Acha dharau wewe kila mtu ana haki ya kuandika anachokiona

Tony Gwanco ni product ya KIU(KAMPALS INT UNIV) na chuo chenyewe chajulikana ni majanga ni heri hata angeenda kusoma utalii management ghorofa ya 3 Kariakoo
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom