Wana CCM acheni unyonge - Kikwete

Wana CCM acheni unyonge - Kikwete

tutobolewe macho kwa nondo tucheke?

unyonge basi

Wabunge wa chadema walivyopigwa nondo na wana ccm kwenye uchaguzi mdogo wa kirumba mwanza mlichekelea leo mmetandikwa leo mnajifanya nyie ni watu zaidi, we are ready for whatever and we got nothing to lose.
 
Furahieni sana kauli za kipumbavu za mwenyekiti wenu, yeye na familia yake hawataguswa, kazi kwenu uswahilini.


nani anakaa uswahilini?

upumbavu kutuambia tuache unyonge?

macho yetu ataturudishia nani?

CCM chama dola unyonge ni Aibu

njooni kalenga na nondo muone
 
Ndio dalili ya anguko la chama chetu twawala! Mwenyezi Mungu tusaidie kuyaepuka machafuko haya yajayo!
 
Kikwete ataingia kwenye battle field au atakuwa amejifungia magogoni. Mzee wa kuangushwa na upepo nae anatangaza vita haya ni maajabu.

Naye itabidi aache unyonge, ajitee na wana CCM. Akiwa kama baba anatakiwa kuwa mstari wa mbele.
 
Dahh!!
Nmemkumbuka JK wa kwanza! Juu ya huyu wa pili.
 
tumechoshwa na fujo zenu

unyonge basi
Tangu lini CCM tukawa wanyonge? Majeshi yote yetu, usalama wa taifa wetu. Inakuaje tuanze kupambana na hao tunaowaita wanatuonea kwa fujo zao? Kwanini tusipambane nao kwa kuwapa huduma bora wananchi ili kuwaziba midomo na kudhibiti fujo zao?
 
Jk ana matatizo! Nakumbuka akiwahutubia wajumbe wa NEC mwaka jana pale Dodoma aliwaambia "...Na nyinyi acheni kutegemea polisi jibuni hoja za wapinzani majukwaani..." kauli hii ilikuwa inaleta ujumbe kuwa CCM walikuwa wanatumia Polisi kujibu hoja za wapinzani ikiwa ni pamoja na vurugu kwenye mikutano iliyosababisha vifo ambavyo kimsingi baadhi ya vifo wauwaji walikuwa Polisi, mfano kifo cha Ally Zona kule Morogoro na Daud Mwangosi kule Iringa.

Lakini pia kukatwa shingo kwa mashine ya mbao kada wa chadema kule Arumeru kipindi cha uchaguzi mdogo na baadae kukamatwa kada wa ccm aliyehusika ambaye baadae alitoroka mbele ya polisi wenye silaha akiwa mahakamani; mtakumbuka kuwa uchaguzi wa Igunga iliokotwa maiti ya kada wa chadema aliyetoweka baada ya kutekwa na vijana walio hisiwa kuwa niwa Greenguard ikiwa na majeraha ya vipigo.

Kwa maono yangu, Jk kama amiri jeshi mkuu hakupaswa- kutoa kauli ile maana kwa maana nyingine ni sawa na kutangaza vita na kuhamasisha kujibu mapigo, jk alitakiwa kutafuta suluhisho la kudumu kuepusha machafuko yanayotokea kwenye chaguzi sio kuchochea vijana wa ccm wasiwe wanyonge huku akijua mara zote ndio wamekuwa chanzo cha vurugu; Lakini pia, naamini kuwa ametoa kauli ile huku akijua kuwa chaguzi zinapofanyika baadhi ya vyombo vya usalama huwa upande wa ccm.

Nimesikitishwa sana na kauli ya JK maana haina tofauti na ile kauli ya waziri mkuu ile ya piga tu. Huyu jamaa ameonyesha udhaifu tulioambiwa miaka 2 iliyopita.
 
Wewe unatapatapa sana mkuu,katika mchango wangu ulionijibu hakuna sehemu nimesema CHADEMA ni chama cha kidini , nashangaa unajizogoa mwenyewe kwa vile unajua kabisa ninyi ni wadini. Halafu ujue kuwa Katiba Mpya na elimu bure hazikuwa agenda zilizoanzishwa na CHADEMA, wapo watu kama akina MTIKILA, chama cha CUF na hata wabunge wa CCM walikuwa na hoja hizo tangu hata kabla haijafahamika kama KUNA SIKU CHADEMA kitakuja kuoenakana kwenye ramani ya vyama vya siasa nchini.

Naomba na mimi nikupe mfano mmoja tu wa namna ambavyo CHADEMA wanapenda kujichomeka kwenye hoja za wengine.

Miaka yote CUF waliwatuhumu CHADEMA kuwa wanashrikiana na chama cha CONSERVATIVE cha kule uingireza, chama ambacho ni wazi kinaunga mkono USHOGA. Hoja hii ya CUF imewatesa sana CHADEMA mpaka WENJE alipokuwa na udaku wake kuwa CUF nao wanashirikiana na chama cha ushoga, basi wakalibebea bango ili mradi tu wajinasue kuwa MASHOGA, lakini ukweli utaendelea kubaki pale pale kuwa CHADEMA wanashirikiana na mashoga wa Uingereza na hata juzi JK aliulizwa kuhusu msimamo wake juu ya ushoga na jibu lake likawa ni la herufi mbili tu kubwa yaani "NO"
CHADEMA wadandiaji wa hoja na sera za vyama vingine, ndicho chama kichanga kabisa ukilinganisha na CCM, CUF na NCCR-Mageuzi, hawa ni wazuri sana wa ku-copy na ku-paste.

Nashukuru sasa iwapo umekanusha Mwenyewe kwamba viongozi wa CHADEMA siyo wa Kidini kwa hiyo huko nako ni kukiri kwamba sihitajiki kufundishwa nao kitu cha kusema na kuzungumza hilo la udini halipo.. hujajibu hoja zangu za Msingi kwamba Mnatekeleza Ilani ya nani? Usimhusihe Mtikila kwani yeye amekataa kwamba hiki kinachokwenda Bungeni siyo kiloe alichokipigania! na kuhusu hili la Katiba ni kukumbushe Tu siyo CUF ni NCCR wakti huo linaanza kama mchakato wa Kudai Mageuzi ,baadaye wakaja sijui wakajiita KAMAKA kamati ya madai ya Katiba ila swali langu la Msingi lilikuwa mnatekeleza Ilani yanani CCM au CHADEMA. kwa sababu hujanijibu mimi kama mtu mzima nimesha kuelewa Mkuu.

Hili la ushoga hakusema "NO" bali kama kawaida alitoa "a chamelion like response capable of all interpretation" kwamba Muda wake bado...
 
Ahaaaa kumbe ndo maana PINDA alisema Wapigwe tu mi sikujua kama alipata ruhusa toka juu.
 
Lakini matokeo ya uchaguzi hayaonyeshivyo, labda tofauti ya takwimu ya idadi za kura.
Mkuu ushindi si kila kitu ingawaje ndio lengo la kila chama.
Peace and tranquility ndani ya chama ni muhimu.
Leo najiuliza kama Malecela, Msindai Ngeleja Lowasa na hata Kinana na Ngombale kama wanaweza shiriki yale matembezi ya kila mwaka aliyokuwa anaendesha mzee Kawawa, matembezi ya Mshikamano.
 
Hapa ndio tujue kuwa mateso ya wapinzani, wananchi, waandishi wa habari na mauaji yaliyowahi kutokea siyo ya bahati mbaya, ameona hayo hayatoshi sasa amekwenda public kuhamasisha. Natamani watanzania tuamke na tumpuuze kwa nguvu zote tuishi kwa amani na hii nchi yetu tunayoipenda.
 
liwalo na liwe na sisi tupo tayari kujilinda,nadhani umefika wakati wa kunoa sime zetu muraa!
 
Back
Top Bottom