Wana CCM acheni unyonge - Kikwete

Wana CCM acheni unyonge - Kikwete

Nadhani ataomba radhi kwa hili; nayeye ni binadamu ulimi unaweza kuteleza tuuu hasa kama mtu ana hangover
 
TUANZE KUMSHITAKI HUYU aliyesema" NCHI HAITATAWALIKA"- Huyu ndiye mleta vurumai zote Kisha Tuje kumshitaki kikwete

Kikwete ni Rais wa JMT ambapo pia ni Amiri Jeshi Mkuu na aliyesema "nchi haitawaliki" ni raia ambaye alipaswa kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria kujibu tuhuma kama kuna sheria iliyokuwa imevunjwa! Lakini Rais wa JMT (awe ni CCM, CDM, au CUF) anakuwa amevunja katiba kwa kutoa kauli yo yote ya uchochezi (kama kweli amesema yaliyonukuliwa). Shame on JK (pengine ana kiherehere🙁)
 
wewe mweneawazimu sana sasa ulitaka tupigwe hafu tukae kimya kwa lipi la zaidi mlkionalo sasa nasema anzeni tena ugomvi uone maiti zitakazo okotwa
 
Viongozi wetu hawana uzalendo kabisa anatamka haya akijua yakitokea machafuko yeye anaouwezo wakwenda kuishi popote duniani, ikumbukwe kunawatu maskini hawawezi hatakuhamia mkoa mwingine japo wanaishi ktk hali ngumu. Napata wasiwasi yawezekan wanaongozwa na nguvu giza hawezekan ukasema hayo maneno kama hujatumwa kutoa kafara watu.( Fake tz leaders).
 
hayo ni matakwa ya cdm
kumbe matakwa ya cdm ni kutaka watu wengi washirki zoezi LA kupiga kura ambayo ni haki yao kikatiba?na matakwa ya ccm ni yapi?no wonder rais wenu alipatikana kwa uchaguzi ulioshirikisha wapigakura milioni nane,kwenye nchi yenye watu wenyekustahili kupiga kura milioni 22.
 
Inasikitishs sana wananchi hawajamwelewe raisi wetu haswa hawa wafuasi wa cdm,alichoimanisha ni kwamba wanachama wa ccm ni lazima wawaeleza watanzania kuhusu ubakaji wa demokrasia unaofanywa na cdm
 
Tuliponga, Huyo Mwenyekiti wa ccm anataka kutuhamisha kutoka katika Mjadala wa Katiba.Hizi kaauli za viongoz wa CCM zina sharabu uelewa wao na akili zao zilivyo hebu Tizama na hizi za wengine;

1. Inaseme kana Mbunge wa zamani wa Karatu (Marehemu Patrick QORO aliwahi kuwambia watu wa mang`ula Karatu kwamba vichwa vyao Viko Kama Vitunguu! na wengine walipo mhoji kuhusu tatizo la maji aliwa jibu ...sasa mnataka mimi nikojoe ndo mpate maji?
2.Basil Pesa mbili Mramba alisema wananchi wa Tanzania hata walalamike vipi na ikibidi kula majani wale ila ndege ya Rais itanunuliwa
3.Mzee David Cleop Msuya akiwa Waziri alipata kutamka kwamba Kila mtu atabeba mzigo wake Mwenyewe.
4.Mzee Benjamin Mkapa akitetea kukabidhi mashirika ya uma kwa Bei chee kwa makaburu alisema Paka ni paka ilimradi anakamata Panya?
5.Waziri Mkuu mstaafu F.Sumaye...Wafanyabiashara mkitaka mufanikiwe katika Biashara zenu mujiunge na CCM.
6.Mh.George Simbachawene alipata kuwaambia wanaodhani Umeme ni gharama watumie vibatari!?
7.Mh.John Pombe Magufuli alipata kusema wanao shindwa kulipa nauli ya Tsh Miambili kwenda Kigamboni wapige mbizi?!
8.Mheshimiwa Mizengo Peter Pindi alipata kusema nimechoka sasa wanchi wapigwe Tu na alipoambiwa kuhus mafisadi akasema hao wasiguswe nchi itatikisika.
9.Rais Kikwete amenukuliwa akiwahamasisha ccm kutokuwa wnyonge na kutoa mifano ya Igunga na kwamba sasa anawataka kujibu Mapigo?! na kwamba katika uchaguzi wa Kalenga wana enda kupambana na Chama cha Vurugu.

Kauli ya nene na tisa hapo juu zisipofanyiwa kazi kikamilifu na wanamageuzi wote pamoja na watanzania na kuhakikishieni watajuuutah?! kuifahamu CCM ,KWA MAONI YANGU HILO AGIZO CONSTURCTIVELY WALIKUWA WANAPEWA WAKUU WAVITENGO VYA ZIADA VYA ccm YAANI POLISI,JESHI NA BAADHI YA MAAFISA USALAMA WA TAIFA MAAKE HAWA NDO TUMEWAONA WAKIPIGA WATU KWA NIABA YA CCM NA SERIKALI YETU.

Swali la kujiuliza je tutaendelea mpaka lini kusubiri Kupigwa,kungolewa meno,kulipuliwa mabomu ,kubambikiwa kesi?! Baba wataifa alipata kusema iwapo mambo haya yataendelea kufanywa na wananchi wakendelea kuvumilia basi WANCHI HAO WATAKU MATAAHIRA!

muwe mnawauliza mapdre wenu wawatafsirie wamesoma sana biblia ambayo kwa kiwango kikubwa imeandikwa kwa mafumbo la sivyo hamutaweza kujua viongozi wasomi wa CCM wanakuwa wanamaanisha nini kwenye kauli zao. Usitegemee vichwa matope kama cha MBOWE, LEMA, MSIGWA , LISSU, VICENT NYERERE na ninyi wote mjue wanakuwa wana maanisha nini?

1. CHADEMA ikiingia madarakani , mfuko wa cement 5000/= . gharama ya kuzalisha mfuko mmmoja shilingi ngapi?
2. CHADEMA ikiingia madarakani elimu, afya bure. tupe mfano wa nchi mojawapo afrika na hata ulaya inayotoa elimu bure?
3.Itaichukua CHADEMA mwaka mmoja kuibadilisha Tanzania kuwa nchi ya viwanda. unajua mapinduzi ya viwanda ulaya yalichukua muda gani?
4. Bomba la gesi kutoka Mtwara linjaengwa kwenda Ulaya na siyo Dar es Salaam, SLAA huyo.
5. Itaichukua CHADEMA siku 100 kuipatia Tanzania Katiba mpya. Tangu mchakato wa Katiba mpya uanze siku 100 bado? au hiyo ya CHADEMA wangelkaa mtaa wa UFIPA na kuiandika ili ndani siku 100 iwe imekamilika?

Kama ni matamshi ya kijinga CHADEMA wanaongoza.
 
naona hapa anashambuliwa Kubenea wakati aliyeweka post bila hataa kutaja source ni Yeriko Nyerere.

Hata hivyo kama Kubenea kayasema hayo (mapendekezo yake) nafikiri yuko sahihi. Raisi wa nchi lazima uchuje maneno kabla ya kutamka. Raisi (hata anapokuwa mwenyekiti wa chama) anatakiwa kujua kuwa lolote analotamka linaweza kuathiri watanzania wote.

Hata hivyo tunajua kuwa raisi wetu si makini na tumemzoea, hamna jipya!
 
Nadhani ataomba radhi kwa hili; nayeye ni binadamu ulimi unaweza kuteleza tuuu hasa kama mtu ana hangover

kauli moja tu mmewehuka je hiz za slaa 1.nchi haitawalika 2.tutapambana mpaka kieleweke.hakuna kuomba radh
 
Huyu ni Rais kweli? Je, anajua madhara ya kauli zake kweli akiwa kama Rais? Mimi kwa maoni yangu naona ni bora akapimwe kama ana akili sawasawa, bila shaka ana tatizo kubwa ambalo washauri wake wanatakiwa wamsaidie.

Cjawahi kuona Rais dhaifu kama huyu.
 
Hapa hatushindani kuorodhesha maovu wanayofanyiwa wafuasi wa vyama, kikubwa hapa ni kuwa JK kaongea kama RAIS na AMIRI JESHI MKUU.

Acha kuchanganya habari wewe, JK kaongea kama mwenyekiti wa chama.
 
Hii mada ya YERIKO inahusiano gani na daftari la kupigia kura? au kuwapiga watu kuna uhusiano gani na daftari kuboreshwa? shughulisha akili yako mkuu.
umeona niliye mquote kaandika nini?rudi kasome alafu ulinganishe Kisha useme kitu.
 
Mbona hukusema haya wakati wana CCM wamechomewa nyumba, wamekatwa mikono na kutolewa macho huko kahama?

Mbona hukuwashitaki Mbowe na Slaa wanaotembea kwa chopper kushinikiza ngumi na mapanga kila siku?

Mchochezi ni nani? Umemwelewa JK we Kubenea au ni muendelezo wa majungu yako ya kukosa kuteuliwa nae tangu 2005?

JK hakumaanisha mapanga wala ngumi, na kama unapenda haki dhidi ya wachochezi basi faili la kwanza Mahakamani washitakiwe Mbowe na Slaa pamoja na wabunge wao kwa uchochezi na utekelezaji wa mauaji.

Nenda Bugando Mwanza ukawaone majeruhi ndo uje uandike makala yenye haki.

Kubenea unajiaabisha.
Hata wao chadema watakushangaa kama unasimama kuwatetea.

Ushahidi wa mwanzo ni namna wananchi walivyoamua kuwakataa kupitia kura na kuambulia kata 3, je unadhani hiyo ni kawaida?

Kubenea vua miwani ya ushabiki uitendee haki kalamu yako.

wewe ndiye mshsbiki tena asiye na akili maana kushabikia ccm ni kuua watu indirectly,ccm ni wauaji wanaharibu miundo mbinu ya hospitali huku wao wanatibiwa ulaya,gharama za maisha zik juu wao wanajilimbikizia mali,juzi jk kasema anajua wauza meno ya tembo unadhani atafanya nini?hamna lolote,mangapi anayafahamu na hajachukua hatua yoyote?au na yeye ni muhusika?acha ujinga wewe.
 
Mbona hukusema haya wakati wana CCM wamechomewa nyumba, wamekatwa mikono na kutolewa macho huko kahama?

Mbona hukuwashitaki Mbowe na Slaa wanaotembea kwa chopper kushinikiza ngumi na mapanga kila siku?

Mchochezi ni nani? Umemwelewa JK we Kubenea au ni muendelezo wa majungu yako ya kukosa kuteuliwa nae tangu 2005?

JK hakumaanisha mapanga wala ngumi, na kama unapenda haki dhidi ya wachochezi basi faili la kwanza Mahakamani washitakiwe Mbowe na Slaa pamoja na wabunge wao kwa uchochezi na utekelezaji wa mauaji.

Nenda Bugando Mwanza ukawaone majeruhi ndo uje uandike makala yenye haki.

Kubenea unajiaabisha.
Hata wao chadema watakushangaa kama unasimama kuwatetea.

Ushahidi wa mwanzo ni namna wananchi walivyoamua kuwakataa kupitia kura na kuambulia kata 3, je unadhani hiyo ni kawaida?

Kubenea vua miwani ya ushabiki uitendee haki kalamu yako.

wewe mjinga usisababishe tukapata hasira bure hivi unajua ni watu wa ngapi wa chadema wameishauwawa na kuumizwa na wengine mpaka sasa ni vilema kuanzia wakati wa uchaguzi wa Kiteto 2007,Tarime, busanda, biharamulo,na mpaka igunga kumbe Kikwete alinyamazia yale mauji kwasababu yeye ni sehemu ya mpango huo amehusika kupanga huu upuuzi wa kuwaua Watanzania kwasababu wana mawazo mbadala huyu anatangaza umwagaji damu na hatuatakubali hata kidogo.
 
kumbe matakwa ya cdm ni kutaka watu wengi washirki zoezi LA kupiga kura ambayo ni haki yao kikatiba?na matakwa ya ccm ni yapi?no wonder rais wenu alipatikana kwa uchaguzi ulioshirikisha wapigakura milioni nane,kwenye nchi yenye watu wenyekustahili kupiga kura milioni 22.

Lakini 14 kati mil.22 ambao hawakupiga kura walijiandikisha? kosa la nani mpiga kura au daftari la mpiga kura kutoboreshwa? hata wakijiandikisha watanzania wote hata aliyezliwa leo, CCM itashinda tu, coz CCM ina wapiga kura, CHADEMA ina wapiga viroba.
 
“Tunashindana na wenzetu wagomvi, maana wao ugomvi ndiyo sehemu ya mwongozo wa kufanya kazi ya siasa,”alisema Kikwete bila kutaja chama chochote cha siasa kwa jina.

“Tulizungumza nalo hilo kwenye Kamati Kuu, tulikubaliana kuacha unyonge. Ndiyo, kwenye Kamati Kuu tumekubaliana, tumesema jamani watu wote waende wakaseme tumekubaliana kuacha unyonge,” alisema huku akicheka na kupigiwa makofi na wajumbe wa Nec.

Rais Kikwete ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu, alitolea mfano wa tukio lilitokea Kahama mkoani Shinyanga, ambapo kijana mmoja alitolewa macho kwa bisibisi, na tukio la Igunga ambapo kijana mmoja alimwagiwa tindikali katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo.

“Acheni unyonge na hata katika taarifa ya habari leo (jana) mtoe hivyo hivyo. Na mwache habari zote mseme hii tu (waandishi wa habari). Uvumilivu una ukomo wake,” alisema huku wajumbe wakiendelea kumpigia makofi.

“Nalisema kwa sababu yanayotokea yanasikitisha sana. Pale Igunga kijana yule wamemwagia tindikali, pale Kahama kijana ametolewa macho kwa bisibisi,”alisema.

Hata hivyo, Rais Kikwete aliwataka
wanachama wa CCM kujipanga vizuri katika uchaguzi huo, ili kuhakikisha wanapata ushindi mnono.

Chanzo....Mwananchi.
 
Lakini 14 kati mil.22 ambao hawakupiga kura walijiandikisha? kosa la nani mpiga kura au daftari la mpiga kura kutoboreshwa? hata wakijiandikisha watanzania wote hata aliyezliwa leo, CCM itashinda tu, coz CCM ina wapiga kura, CHADEMA ina wapiga viroba.

Jaribuni kuboresha kama hamjaaibika!
 
Viongozi wetu hawana uzalendo kabisa anatamka haya akijua yakitokea machafuko yeye anaouwezo wakwenda kuishi popote duniani, ikumbukwe kunawatu maskini hawawezi hatakuhamia mkoa mwingine japo wanaishi ktk hali ngumu. Napata wasiwasi yawezekan wanaongozwa na nguvu giza hawezekan ukasema hayo maneno kama hujatumwa kutoa kafara watu.( Fake tz leaders).
Umenikumbusha ndugu,katika orodha ya wanachama wa freemason na Rais wenu yumo,hivyo yawezekana ni zamu yake kutoa damu za watu,ndiyo anatafuta hizo damu kwa njia za uchochezi wa Raia wake ili Damu ipatikane.
 
Back
Top Bottom