Wamiliki wa Mabasi na mafuso hutoa wapi hela?

Wamiliki wa Mabasi na mafuso hutoa wapi hela?

nikufahamishe tu unaowaona wanaaagiza mabus mengi wako in business for 7+ years wako na reputation kwanzia ndani ya nchi mpaka nje ya nchi kwenye kampuni za mabus wako na njia zao nyingi za kupata mitaji either ya pesa au mabasi yenyewe ......kuna kupata mikopo(pesa au mabus yenyewe) through assets kama viwanja ,mashamba,nyumba,viwanda,bonds+hisa,sales agreement contract ,cheo chake ....jamani bandugu hii option ni risk sana na wengi unaowaona wanaishi na madeni makubwa ila "ujasiriamali " lazima usonge wengi mtakataaa ila mnakumbuka story ya mo dewji kutafuta mkopo wa 500bl ...asset alikuwa nazo ila pesa ndo ilikosekana mpaka alivyopigiwa pande la kwa madiba ndo akapata

nyingine ni kuchangiana mitaji au hayo mabus yenyewe kutoka kwa ndugu ,jamaa na marafiki kutoka ndani ya nchi mpaka nje hii inajumuisha pia investors ila kwa makubaliano wanayoyajua wao hili lilikuepo hata kwenye ukoo wetu nanililishuhudia kabisa japokuwa alikuja yauza alivyoona biashara haiendi vizuri

kuna wengine through saving na analipa cash pesa yake mfukoni na anaagiza kuna watu wanapesa tz hii hatujui tu bank statement za watu.....correct me if iam wrong wote tuko hapa kujifunza kutokana na swali la mtoa mada
MO alienda Kopa RMB sababu ya Riba ndogo, anadai walimpa chini ya Asilimia 8 wakati huo Mabenki ya Tz yalikuwa yakitoza 21%
Pia RMB ilimsaidia wa kuunganisha Bank mbali mbali kupata mkopo wa dollar milioni 200

Ni sawa na Azam alivyokopa Standard Chartered kwenye mradi wa Bagamoyo Sugar
 
Pambana,Pambana anza na kujenga uaminifu kwa waliokuzunguka.

Baba yangu hakunipa mtaji (pesa) wa maisha zaidi ya ELIMU.

na kingine siku 1 aliniambia,Unaenda huko duniani Mtaji wako mkubwa ili ufanikiwe ni UAMINIFU kwa waliokuzunguka.

KUWA MWAMINIFU hata kama huna kitu sasa,epuka kuchukua cha mtu fanya kazi kwa bidiii ukipewa 10,000 ukatumwa kitu cha 1000 ukaenda ukakuta kile kitu kinauzwa 500 usibanie ile 500 rudisha chenchi 9500 kisha mwambie aliekutuma Bidhaaa imeshuka bei chenchi hii hapa.

Kweli yako iwe Kweli na Hapana yako iwe Hapana.

Ukiaminika na waliokuzunguka, ni sifa namba 1 ya kutoka kimaisha huitaji kuwa na kipande cha Ardhi, huitaji kuwa na Pesa.

UKIAMINIKA wewe ni Tajiri hata kama unajiona huna kitu sasa lakini kama kuna mtu akiwaza kumtuma mtu kitu mahali akili yake inakufikiria wewe ndie mtu sahihi (Umemaliza mwaisa).
Wee jamaa nimekuelew na nimekukubali.Neno moja tuu
kwenye kumiliki ardhi tuwahase vijana wawe waangalifu.

Binafsi nimepata hasara kwenye ardhi nilizonunua nikawaachia watu waniangalizie bila kufanya utaratibu wa kuzipatia vibali vya kuzimiliki.Ni habari ndefu ila ni hivyo.
Ardhi ukibahatika ukaipata kwa watu waaminifu hasa wazee wanaojitambua na ikiwa ni huko ndani ndani unaipata kwa bei nafuu na si ya kitapeli .utaipenda, Ukienda kichwa kichwa unaangukia mikononi mwa matapeli wanakuuzia mashamba ya MO hata kidogo ulichonacho kinasepa.

Naunga mkono hoja ya uaminifu na kufanya kazi kwa bidii popote unapopata fursa.
Kuna vijana walijenga uaminifu kwenye nyumba za ibada,waumini wenye fursa wakawaona,wakawafanya
wafanyakazi wao sababu ya uaminifu wakatoka kimaisha n.k
Tusijifariji kwa kusema kila aliyefanikiwa kaiba au kaloga
 
..ngoja nikupe mfano mmoja tu wa jinsi wanapata pesa....uone wanavyopiga hela.....chukua basi moja la sh. mil.300...anakopa benki mil.300..ananunua basi......hili basi lina viti hadi 55....kwa safari ya dar moshi nauli sh. 45,000/...kwa viti 55 ni sh. mil. 2,475,000/ kwa trip moja kwenda dar (hapo hujaweka bei ya mzigo)....hapo ukitoa mafuta na service labda mil. 1....anabakiwa na mil. 1,475,000/anakunja kwa siku....piga mara siku 30 (mwezi)....ni mil.44,250,000/ kwa mwezi....piga kwa mwaka (miezi 12) unapata mil. 531,000,000/ hilo ni basi jingine jipya na baki zaidi...hapo ni basi moja limeleta hiyo pesa......kama ana mabasi mawili??au matatu??...kila mwaka ana uwezo wa kununua basi...hata mawili.....na alianza na mkopo wa mil.300 tu benki.....HAKUNA UCHAWI HAPA...NI KUJARIBU TU...KWA KUAMINIWA NA BENKI....SASA HAWA WENYE MABASI WANACHUKUA HELA BENKI WANAVYOTAKA....HIYO NDIO SIRI...
umesahau malipo ya wahudumu wa basi,Latra,Pesa ya kulipia kila stand wanayoingia ,bima ya gari etc
faida ipo ila siyo kama ulivyopiga hesabu..
 
MO alienda Kopa RMB sababu ya Riba ndogo, anadai walimpa chini ya Asilimia 8 wakati huo Mabenki ya Tz yalikuwa yakitoza 21%
Pia RMB ilimsaidia wa kuunganisha Bank mbali mbali kupata mkopo wa dollar milioni 200

Ni sawa na Azam alivyokopa Standard Chartered kwenye mradi wa Bagamoyo Sugar
Kumbe kikubwa tutafute pesa za mwanzo then tukope tu huko mbele

Sent from my 220333QAG using JamiiForums mobile app
 
Mfano GSM ana malori 1000

Wolrd Oil ana Tanker zaidi ya 300

Alistair ana lori zaidi ya 100

Lake Oil ana Mende zaidi ya 100, Tanker zaidi ya 200, Cement Truck zaidi ya 300 kwenye SGR

MO ana magari zaidi ya 1000

Azam ana magari zaidi ya 500

Shabiby ana Mabasi 50+
Hivi hizi mali za watu huwa mnazihesabu?au mnajuaje idadi yake....Mfamo hayo magari ya MO....Inamaana ulizihesabu ulipofika 1000 ukachoka kuhesabu?
 
Siku tukiingia barabarani na kuwatoa hao MAJIZI katika system basi Kila raia wa nchi hii ataweza kumiliki angalau gari na nyumba ambayo ni standard,NCHI IMESHAOZA HII
 
Chain n muhimu lakn hua n vitu vya muda , kama akili huna utapoteza kila kitu , nafaham mmoja enz za JK , mpaka unajuliza huyu mtu pesa anapata wapi , mwaka mmoja baada ya jk kustaafu karud kijiwen pesa yote kwisha
Kaka.. kuna watu wanajua kutumia fursa. Akiiba . Mapesa anaenda tumia vzur... Asilimia 80 ya matajir wa bongo mitaji wamepatia kwenye hizo chain.. wenye mahotel.. wamiliki wa tv na redio station weng .. wamilik wa mabasi na malori.. na wanasiasa weng. Infwaact... Serikal za africa ni kichaka cha majiz yaliyo halalika. Mpaka siku wananch watakapo amua mabadiliko ndio wiz huo utapungua .
 
Hivi hizi mali za watu huwa mnazihesabu?au mnajuaje idadi yake....Mfamo hayo magari ya MO....Inamaana ulizihesabu ulipofika 1000 ukachoka kuhesabu?
Kwenye website yao wameandika , kampuni nzima ina magari zaid ya 2000 yanayo operates kwenye nchi 12
 
Kaka.. kuna watu wanajua kutumia fursa. Akiiba . Mapesa anaenda tumia vzur... Asilimia 80 ya matajir wa bongo mitaji wamepatia kwenye hizo chain.. wenye mahotel.. wamiliki wa tv na redio station weng .. wamilik wa mabasi na malori.. na wanasiasa weng. Infwaact... Serikal za africa ni kichaka cha majiz yaliyo halalika. Mpaka siku wananch watakapo amua mabadiliko ndio wiz huo utapungua .
Sio kweli

Hii nchi idadi ya matajiri n wengi kuliko unavyoweza fikiri , wote wangepata pesa kupitia njio hiyo hili taifa lisingeweza fanya kitu chochote
 
Sio kweli

Hii nchi idadi ya matajiri n wengi kuliko unavyoweza fikiri , wote wangepata pesa kupitia njio hiyo hili taifa lisingeweza fanya kitu chochote
Unahis hili taifa limefanya nn cha maana... Tulio ughaibuni had tunaona aibu kujitambulisha tunatoka nchi hzi za east africa... Mtu unaona bora utaje hata south africa.. ni aibu tupu.. ni vile wa Tz waamezoea umasikin.. ila unapokuja dunian huku ndio unaelewa kuwa watu wanaish kwenye ufukara wa hal ya juu.
 
Unahis hili taifa limefanya nn cha maana... Tulio ughaibuni had tunaona aibu kujitambulisha tunatoka nchi hzi za east africa... Mtu unaona bora utaje hata south africa.. ni aibu tupu.. ni vile wa Tz waamezoea umasikin.. ila unapokuja dunian huku ndio unaelewa kuwa watu wanaish kwenye ufukara wa hal ya juu.
Ni wewe ni sehem ya huo umasikini
 
Back
Top Bottom