Wamiliki wa Mabasi na mafuso hutoa wapi hela?

Wamiliki wa Mabasi na mafuso hutoa wapi hela?

New combines can cost anywhere between $330,000 and $500,000 without add-ons (Source). For this reason, many farmers opt to purchase a used combine to save money. Just like buying a used car, a used combine can be just as reliable and useful as a new combine, depending on what you buy.
Used mpk milioni 70 unapata
 
Kwa kweli Mimi nimepanga kwenda kumuuliza tajiri mmoja yani yeye alifanyaje hadi akaweza kumiliki kuanzia Milioni 500.
Nimeamua nitumie njia yoyote ile kupata hela kwa kweli.
hatokueleza ukweli. sanasana ataishia tu kukwambia "alianza na biashara ya kuoka mikate miaka ya 90".

mwisho atakwambia "kijana jitume...ukipata hata shilingi mia itunze".
 
Mfano GSM ana malori 1000

Wolrd Oil ana Tanker zaidi ya 300

Alistair ana lori zaidi ya 100

Lake Oil ana Mende zaidi ya 100, Tanker zaidi ya 200, Cement Truck zaidi ya 300 kwenye SGR

MO ana magari zaidi ya 1000

Azam ana magari zaidi ya 500

Shabiby ana Mabasi 50+
kwa hali hiyo, hao matajiri wanaomiliki malori ya mizigo, wakiunganisha nguvu kuhujumu ujenzi wa sgr, sidhani kama kuna mbunge wa ccm pale dodoma ataweza kupanua kinywa chake kupinga hujuma hiyo.
 
Umeamua kutugombeza Broo!!!
Hapana sio kugombeza, ila nimegundua kuna haja ya kutoa elimu kwa watu/vijana ili wajue namna ya kupata mikopo ya bank kuendeleza biashara zao, mtu unamkuta anafuga kuku 1000 lakini hata document moja ya biashara yake hana, Bank zinapenda cash flow , ukiweza kuwaonyesha watakupa mkopo kupanua biashara yako, na ndio njia rahisi ya kukuza biashara na uchumi kwa ujumla, hakuna wafanyabiashara serious wanaotumia pesa zao binafsi, biashara zote za uhakika zinatumia pesa za mikopo, hao wahindi na waarabu wengi ni mikopo tuu, lazima tufundishe watu na vijana namna ya kutumia hii mitaji ambayo ipo wazi kwa kila mtu ili kupambana na umaskini
 
Pambana,Pambana anza na kujenga uaminifu kwa waliokuzunguka.

Baba yangu hakunipa mtaji (pesa) wa maisha zaidi ya ELIMU.

na kingine siku 1 aliniambia,Unaenda huko duniani Mtaji wako mkubwa ili ufanikiwe ni UAMINIFU kwa waliokuzunguka.

KUWA MWAMINIFU hata kama huna kitu sasa,epuka kuchukua cha mtu fanya kazi kwa bidiii ukipewa 10,000 ukatumwa kitu cha 1000 ukaenda ukakuta kile kitu kinauzwa 500 usibanie ile 500 rudisha chenchi 9500 kisha mwambie aliekutuma Bidhaaa imeshuka bei chenchi hii hapa.

Kweli yako iwe Kweli na Hapana yako iwe Hapana.

Ukiaminika na waliokuzunguka, Ni sifa namba 1 ya kutoka kimaisha huitaji kuwa na kipande cha Ardhi, huitaji kuwa na Pesa.

UKIAMINIKA wewe ni Tajiri hata kama unajiona huna kitu sasa lakini kama kuna mtu akiwaza kumtuma mtu kitu mahali akili yake inakufikiria wewe ndie mtu sahihi (Umemaliza mwaisa).
mimi ni mkirsto(ila huwa sina desturi ya kwenda church),ulichoandika kuhusu uaminifu kipo very relevant kwa ndugu zetu waislamu.

aliwahi kusema rev. kimaro wa kanisa la KKKT kuhusu baadhi ya vijana wa kiislamu na masuala ya uaminifu. baadhi ya wahafidhina ktk jamii yetu ya kikristo walichukizwa na kauli ile.

ni kweli baadhi yao ni waaaminifu sana. na ndio sababu ukichunguza vijana wajasiriamali waliofanikiwa, katika vijana 10, 6 utakuta ni waislamu.

tangia level ya madrasa, mafundisho ya dini ya kiislamu yanasisitiza sana kuhusu uaminifu.

kuna kijana fulani wa kiislamu aliaminiwa sana na familia moja ya kisomali. ikamkabidhi kituo cha mafuta(filling station) akisimamie.

yule kijana alipambana sana kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa. baada ya miaka mitatu, wale wasomali wakaongeza vituo vingine viwili vya mafuta

hivi ninavyoandika hapa, yule kijana sasa hivi na yeye anamiliki kituo chake kimoja cha mafuta huko shinyanga baada kupewa mtaji kama asante ya uaminifu kutoka kwa ile familia ya kisomali.
 
Fursa! fursa! fursa ndiyo mpango mzima. Fursa yoyote mpya ina super profit, yaani hata waliofanya bodaboda kipindi kile ndo zinaingia walipiga pesa balaa na wengi now wako mbali. Wekeza katika fursa mpya matokeo yake huwa ni makubwa na ya kunufaisha sana
Ata waliotumia Lipa kwa mpesa wakati zinaingia now wapo mbali sana.
 
Mbona hao wa viwango vya juu?...Mimi hapa nawaza nitapata hata ist wapi, au nitaanzaje biashara ya kunipatia 10,000 kwa siku....na type hii sms nikiwa kigoma vijijini.
Jiongeze mkuu. Punguza huruma na upole.
Kama huwezi toa kafara chukua hela za tozo za watanzania wala hutofungwa utahamishwatu kitengo
 
Imagine, kuna haya mabasi

Ester Luxury
Tilisho
Happy Nation
Sauli
New Force
Arusha Express
Shabiby
Abood
Machame Express
Kapricon
Kilimanjaro Express
Dar Express
Zube
Saratoga
Mgamba
Kimbinyiko
Abc
Ally's
Saibaba
etc etc

Malori ndo usiseme.
Unakuta mtu ana basi 10, 20 au 60. Basi moja bei yake ni Milion 300, 400 hadi 500. Jamaa wanapata wapi hela aisee?
Unataka kujua wamepata wapi hizo fedha?

Ni kujipanga tu na nidhamu ya pesa. Uanza kidogo kidogo. Fanya kazi/biashara kwa bidii weka akiba, wekeza kidogo kidogo...kuza mtaji....endelea kuwekeza na kukuza mtaji....fanya hivyo hivyo kwa miaka 30.
 
Yani hill swali kila siku nikipita hapa maeneo ta Shekilango huwa najiuliza nakosa jibu,Jana nimeona Haya mabasi ya BM kama 20 hivi-hawa watu walifanya kitu gani hadi wakapata hizo hela.
Mabasi 20 ni kama bilioni 6 hivi ambazo mkulima wa kawaida ana hiyo fedha achilia mbali wafanyabiashara.

Halafu ukinunua mabasi kadhaa hasa haya ya Kichina unakopeshwa mabasi mengine then unafanya marejesho ya mkopo taratibu.

Naongea haya kwa uzoefu na ushahidi ninaoufahamu.
 
Imagine, kuna haya mabasi

Ester Luxury
Tilisho
Happy Nation
Sauli
New Force
Arusha Express
Shabiby
Abood
Machame Express
Kapricon
Kilimanjaro Express
Dar Express
Zube
Saratoga
Mgamba
Kimbinyiko
Abc
Ally's
Saibaba
etc etc

Malori ndo usiseme.
Unakuta mtu ana basi 10, 20 au 60. Basi moja bei yake ni Milion 300, 400 hadi 500. Jamaa wanapata wapi hela aisee?
Tafuta hela utakufa kwa ugonjwa wa moyo
 
Back
Top Bottom