Wamiliki wa Mabasi na mafuso hutoa wapi hela?

Wamiliki wa Mabasi na mafuso hutoa wapi hela?

Nipo hizo connection za wizi,na ufisadi basi,yani haiwezekani MTU amiliki mabasi karibu 30 ya million 400 Mimi sina hata kibanda.
Mfano GSM ana malori 1000

Wolrd Oil ana Tanker zaidi ya 300

Alistair ana lori zaidi ya 100

Lake Oil ana Mende zaidi ya 100, Tanker zaidi ya 200, Cement Truck zaidi ya 300 kwenye SGR

MO ana magari zaidi ya 1000

Azam ana magari zaidi ya 500

Shabiby ana Mabasi 50+
 
Kuna mtu namfahamu Ana Shimo pale mererani, shimo lake lina uwezo wa kutema vyombo kila mwezi,makinikia ndio usiseme.

Huyu akisema anakopa Anauwezo wa kukopa kununua hayo mabus yote uloyataja na chenchi ikabaki.

Kuna watu wana miliki Assets ambazo ndio maisha yao, Nyingi zisizoonekana.

Mabus na Malori ni vinyongeza tu...
Hivi Tanzanite nayo ina marudio?
 
Unatoa ushauri gani kwetu sisi ambao hatuna vigezo vya kukopesheka hata laki moja?
Pambana,Pambana anza na kujenga uaminifu kwa waliokuzunguka.

Baba yangu hakunipa mtaji (pesa) wa maisha zaidi ya ELIMU.

na kingine siku 1 aliniambia,Unaenda huko duniani Mtaji wako mkubwa ili ufanikiwe ni UAMINIFU kwa waliokuzunguka.

KUWA MWAMINIFU hata kama huna kitu sasa,epuka kuchukua cha mtu fanya kazi kwa bidiii ukipewa 10,000 ukatumwa kitu cha 1000 ukaenda ukakuta kile kitu kinauzwa 500 usibanie ile 500 rudisha chenchi 9500 kisha mwambie aliekutuma Bidhaaa imeshuka bei chenchi hii hapa.

Kweli yako iwe Kweli na Hapana yako iwe Hapana.

Ukiaminika na waliokuzunguka, ni sifa namba 1 ya kutoka kimaisha huitaji kuwa na kipande cha Ardhi, huitaji kuwa na Pesa.

UKIAMINIKA wewe ni Tajiri hata kama unajiona huna kitu sasa lakini kama kuna mtu akiwaza kumtuma mtu kitu mahali akili yake inakufikiria wewe ndie mtu sahihi (Umemaliza mwaisa).
 
Imagine, kuna haya mabasi

ESTER LUXURY
TILISHO
HAPPY NATION
SAULI
NEW FORCE
ARUSHA EXPRESS
SHABIBY
ABOOD
MACHAME EXPRESS
KAPRICON
KILIMANJARO EXPRESS
DAR EXPRESS
ZUBE
SARATOGA
MGAMBA
KIMBINYIKO
ABC
ALLY'S



SAIBABA

etc etc


Malori ndo usiseme.


Unakuta mtu ana basi 10, 20 au 60!

Basi moja bei yake ni Milion 300, 400 hadi 500.

Jamaa wanapata wapi hela aisee?
Hayo mabasi unayoyaona ni chamtoto hawa jamaa Wana mahoteli ya hatari,Petro station za kutosha,ukija kwenye kilimo na ufugaji ukiona utalia brother!! Yan ng'ombe wao wanatoa maziwa kama Wana kisima tumboni!! Wana magest daaaa acha tuu
 
Ukiwaza ghorofa bado umeenda mbali, sasa hivi mnaambiwa nunueni viwanja huko chanika mnaona n maporini.

Utajiri upo katika ARDHI miliki ARDHI kadri uwezavyo siku 1 itakuheshimisha.

Msidharau viwanja vinavyouzwa kama hela unayo sasa hivi, tupia Ardhini. it will pay you back siku 1.

utakua ktk historia za matajiri hii nchi,Ardhi haijawahi ni dissapoint.
Viwanja vya Dsm ndo vina thamani hata viwe KM 50 toka Posta
 
Mfano GSM ana malori 1000

Wolrd Oil ana Tanker zaidi ya 300

Alistair ana lori zaidi ya 100

Lake Oil ana Mende zaidi ya 100, Tanker zaidi ya 200, Cement Truck zaidi ya 300 kwenye SGR

MO ana magari zaidi ya 1000

Azam ana magari zaidi ya 500

Shabiby ana Mabasi 50+
Abood mwaka huu tu mwanzoni alishusha basi 20 pale urafiki.
Ndio maana ile stendi ya mbezi wanaweza kujaza matajiri pengine hata kumi wasifike.
 
Hivi mwanaume unawezaje kuuliza swali kama hili. Hivi kampuni kama kilimanjaro kwann asiwe na gari nyingi kaanza kitambo anajua biashara nashangaa sana mtu kuuliza fulani katoa wapi hela mgawa riziki yupo juu ww pambana kama unaskia zipo pesa za uchawi loga upate ukiski Zipo za dili tafuta madili fanya huu upuuzi wa kuhoji hela za mwanaume mwenzako zitakusaidia nn au unatafuta stor za vijiweni ukawadanganye wajinga wenzako
 
Back
Top Bottom