Waliotuibia mabilioni ya shilingi za pesa za Umma, kama wamegona kutupisha, ni kwanini Rais aliyewateua, anashikwa na "kigugumizi" kuwafukuza kazi?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,162
Hilo ndilo swali kubwa ninalojiuliza, ni kwanini hao watendaji wetu wa Serikali, ambao wanafahamika hata Kwa majina, waliotajwa kwenye ripoti ya CAG, kuwa wamefisadi mabilioni ya shilingi za Umma, ni kwanini Rais Samia Suluhu Hassan, hawatengui kwenye nafasi zao, wakati ni yeye mwenyewe ndiye aliyewateua na ni yeye mwenyewe pekee mwenye uwezo wa kuwatengua kwenye hizo nafasi na badala yake anawasihi Kwa unyenyekevu mkubwa, kuwa watupishe??

Ukiangalia kutokana na ripoti ya CAG, ameyataja mashirika ya Umma ambayo yanaitafuna hii nchi bila huruma, ambao wenyeviti wao wa Bodi, wanateuliwa na Rais, ni kwanini Rais hatumii mamlaka aliyo nayo ya kikatiba, kuwatengua wenyeviti hao wa mashirika yanaotuibia hayo mabilioni ya shilingi za pesa za Umma??

Vile vile wakurugenzi wa Halmashuri za wilaya, ambako huko nako, CAG amefichua madudu ya kutisha, jinsi wanavyojipigia hizo pesa, wakurugenzi hao nao, wanateuliwa na Rais, hivi Kwa nini hawatengui kwenye nafasi zao??

Kama Katiba yetu ya nchi inasema kuwa watu wote tuko sawa mbele ya Sheria, ni kwanini Jela zetu zimejaza wafungwa wenye makosa madogo madogo, kama vile wezi wa simu za mkononi, wakati wezi wakubwa wa mabilioni, wakiachwa huru??

Naona hii nchi imekuwa ya kulalamika miaka yote, wananchi tunalalamika maisha yalivyo magumu, kutokana na gharama za maisha kuwa juu Sana na Rais naye mwenye mamlaka ya kuwatengua hao watendaji wa Serikali wabadhirifu naye analalamika!

Hicho ni kitendawili, naomba mwenye kuweza kukitengua hapa JF, anipe jibu
 
Hizi haki huwa zinazingatiwa kwa wenye nacho tu ila kwa wanyonge ni option unaweza kupewa au usipewe kiasi ambacho imekuwa mtaji kwa wanasiasa wakifanya haki kwa raia wanachukulia credits kana kwamba wananchi hawakustahili ila wamefanyiwa upendeleo.
 
Hilo ndilo swali kubwa ninalojiuliza, ni kwanini hao watendaji wetu wa Serikali, ambao wanafahamika hata Kwa majina, waliotajwa kwenye ripoti ya CAG, kuwa wamefisadi mabilioni ya shilingi za Umma, ni kwanini Rais Samia Suluhu Hassan, hawatengui kwenye nafasi zao, wakati ni yeye mwenyewe ndiye aliyewateua na ni yeye mwenyewe pekee mwenye uwezo wa kuwatengua kwenye hizo nafasi na badala yake anawasihi Kwa unyenyekevu mkubwa, kuwa watupishe??

Ukiangalia kutokana na ripoti ya CAG, ameyataja mashirika ya Umma ambayo yanaitafuna hii nchi bila huruma, ambao wenyeviti wao wa Bodi, wanateuliwa na Rais, ni kwanini Rais hatumii mamlaka aliyo nayo ya kikatiba, kuwatengua wenyeviti hao wa mashirika yanaotuibia hayo mabilioni ya shilingi za pesa za Umma??

Vile vile wakurugenzi wa Halmashuri za wilaya, ambako huko nako, CAG amefichua madudu ya kutisha, jinsi wanavyojipigia hizo pesa, wakurugenzi hao nao, wanateuliwa na Rais, hivi Kwa nini hawatengui kwenye nafasi zao??

Naona hii nchi imekuwa ya kulalamika miaka yote, wananchi tunalalamika maisha yalivyo magumu, kutokana na gharama za maisha kuwa juu Sana na Rais naye mwenye mamlaka ya kuwatengua hao watendaji wa Serikali wabadhirifu naye analalamika!


Hicho ni kitendawili, naomba mwenye kuweza kukitengua hapa JF, anipe jibu
Mkuu tunaambiwa ni haki za binadamu na utawala Bora.
Kinachofanywa ni Kuwa suta tu afu wanaachwa.

Huoni wanavyosemwa semwa afu MWISHO la SIku nothing
 
Report ya CAG inapotoka na kukabidhiwa kwa bunge kujadiliwa wabunge huja na maazimio na hapo ndipo humshauri Rais juu ya nini wanaona kifanyike.

Hata JK alifanyia sana kazi mapendekezo ya bunge.
 
Naileta Hii Halafu Mtajiongeza Wenyewe
Wahuni Wameshika Hatam
 
The white man say it's the black man,the black man say it's the Indians,the Indians says it's all of us - Sijui alikuwa bob au lucky dube ...
 
IMG_20230406_214327.jpg


Kudeal na Fisadi unatakiwa uwe chuma hasa, fisadi sio mtu mdogo, mama ashaufyata
 
View attachment 2579307

Kudeal na Fisadi unatakiwa uwe chuma hasa, fisadi sio mtu mdogo, mama ashaufyata
Ni kitu ambacho kinatuvunja nguvu na kutukatisha tamaa wananchi, kama huko magerezani wamejaa wafungwa wa makosa madogo madogo, kama vile wezi wa kuku, wakati majambazi hasa yanayotuibia mabilioni ya shilingi, yakiachwa yawe huru, huku wakitucheka na kujisemea moyoni, kuwa wajinga ndiyo waliwao!
 
Kwa kifupi SSH ni muhujumu uchumi aidha kwa makusudi au kwa kutokufahamu.
Utaratibu haupo hivyo, tulishazoeshwa na ule mzimu wa chato kufanya vitu nje ya utaratibu ili ajipatie sifa mwenyewe!

Utaratibu ni report inapelekwa bungeni kujadiliwa na wabunge wanatoa mapendekezo yao kwa Rais ambaye ndiye kaipeleka ile report. Na kama umeangalia bunge hata kidogo hii wiki itaona ni jinsi gani wabunge wamewapania hao wabadhirifu akiwemo yule mvaa tai ya taifa. Yule mvaa tai tayari kaanza kuweweseka, kule twitter kamwaga miela kwa watu maarufu wa kule waanze kumsafisha na kumsifia na nadhani hata mule bungeni itakuwa anawatafuta wale wanoko noko awalambishe mamilioni wasimwajibishe!!
 
Report ya CAG inapotoka na kukabidhiwa kwa bunge kujadiliwa wabunge huja na maazimio na hapo ndipo humshauri Rais juu ya nini wanaona kifanyike.

Hata JK alifanyia sana kazi mapendekezo ya bunge.
Muju4
Ngoja nikuulize swali Moja tu jepesi, hivi kuna ambaye amewahi kuuliza sababu za Rais kumtumbua mteule wake?

Ni kwanini Rais hatumii mamlaka aliyopewa Kwa mujibu wa Katiba, Kwa kuwatengua wale wote waliotuibia mabilioni ya shilingi na badala yake tunajionea, Rais akiwateua walewale, miaka nenda, miaka Rudi, utadhani kwenye nchi, ni wao pekee ndiyo wenye hati miliki ya kupewa nyadhifa kubwa kubwa?😎
 
Back
Top Bottom