Tumshauri Rais ateue vijana wasio na uzoefu lakini wana vipaji vya uongozi kwenye taasisi za Umma, hawa ni watu ' potential' sana

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Apr 10, 2019
2,590
4,601
Nitaanza na swali kabla ya 'content' ya mada hii na swali langu ni: kuongoza taasisi za Umma au taasisi yoyote inahitaji uzoefu mkubwa au uwezo mkubwa wa kiuongozi?

swali la pili: Je, mtu ambaye hana uzoefu(graduate) hawezi kuongoza Taasisi Kwa mafanikio?

Lengo la mada hii ni kupata mtazamo juu ya kipaji Cha uongozi na uzoefu, kipi kinachohitajika zaidi ili kupata matokeo makubwa katika Taasisi za Umma na pia kumshauri Rais ikimpendeza badala ya kuteua watu wenye uzoefu mkubwa basi awatazame na vijana ambao hawana uzoefu lakini wana vipawa kikubwa Cha uongozi ambavyo vingine vinapotea kutokana na uzoefu.

Uteuzi na utenguzi ni siri ya mteuaji, wengi wa wateuliwaji wanateuliwa wakiwa hawana taarifa za uteuzi wao kabla na vivyo hivyo wanaotumbuliwa wanatumbuliwa bila Umma kujulishwa sababu lakini Kwa mtazamo wa wengi sababu kuu za kutenguliwa ni za utendaji zaidi kama Kushindwa kufikia malengo husika.

Wengi wa wanaoteuliwa kwenye utendaji wa taasisi za Umma ni wenye uzoefu mkubwa lakini pia inashangaza baada ya muda mfupi huyu aliyeteuliwa na CV inaonesha ana uzoefu mkubwa anatumbuliwa au anasimamishwa. Je, ni nini huwa kinawakumba?

Ninatambua uzoefu ni msingi mzuri wa matokeo makubwa ya kiutendaji lakini kujaribu njia nyingine pia ni jambo jema na linaweza kuleta matokeo chanya kwenye utendaji.

Tumshauri Rais ikimpendeza aangalie kwenye uteuzi vijana ambao hawana uzoefu lakini wana kipawa Cha uongozi ' hawa ni watu 'potential' sana na wanaweza kusaidia kuleta matokeo makubwa Kwa sababu:

i. Vijana wanapoaminiwa kuongoza taasisi watatumia Kila mbinu kusaidia taasisi kukua Kwa sababu ndani ya ufahamu wao wataamini matokeo ndio yatakayowabeba

ii. Vijana ni watu wa matokeo, watapambana kufanikisha matokeo na 'spirit' ya kutaka matokeo itasaidia kuleta ufanisi ndani ya Taasisi husika. Mfano ni makonda

iii. Vijana wana uthubutu na utayari wa kujaribu mawazo mapya ili kuona matokeo makubwa.

iv. Mtazamo wa vijana kwenye mambo mengi ni wa kileo na kisasa, mabadiliko mengine yanakuja Kwa kuendana na usasa. Vijana watakuja na mbinu na mikakati ya kisasa.

Kwa kuwa lengo la mada hii ni ushauri Kwa Rais wetu, Kwa namna ya pekee kabisa namshauri Rais aangalie vijana wenye utayari na kipwa Cha uongozi na sio lazima awe na uzoefu mkubwa kwenye nafasi ya Kamishna wa NCAA , naamini mtu wa namna hii atatusaidia kukuza utalii na kuongeza mapato na fedha za kigeni.
 
Akili ya asili ni bora kuliko makaratasi, ila makaratasi yanaboresha akili ya asili.
 
Nitaanza na swali kabla ya 'content' ya mada hii na swali langu ni: kuongoza taasisi za Umma au taasisi yoyote inahitaji uzoefu mkubwa au uwezo mkubwa wa kiuongozi?

swali la pili: Je, mtu ambaye hana uzoefu(graduate) hawezi kuongoza Taasisi Kwa mafanikio?

Lengo la mada hii ni kupata mtazamo juu ya kipaji Cha uongozi na uzoefu, kipi kinachohitajika zaidi ili kupata matokeo makubwa katika Taasisi za Umma na pia kumshauri Rais ikimpendeza badala ya kuteua watu wenye uzoefu mkubwa basi awatazame na vijana ambao hawana uzoefu lakini wana vipawa kikubwa Cha uongozi ambavyo vingine vinapotea kutokana na uzoefu.

Uteuzi na utenguzi ni siri ya mteuaji, wengi wa wateuliwaji wanateuliwa wakiwa hawana taarifa za uteuzi wao kabla na vivyo hivyo wanaotumbuliwa wanatumbuliwa bila Umma kujulishwa sababu lakini Kwa mtazamo wa wengi sababu kuu za kutenguliwa ni za utendaji zaidi kama Kushindwa kufikia malengo husika.

Wengi wa wanaoteuliwa kwenye utendaji wa taasisi za Umma ni wenye uzoefu mkubwa lakini pia inashangaza baada ya muda mfupi huyu aliyeteuliwa na CV inaonesha ana uzoefu mkubwa anatumbuliwa au anasimamishwa. Je, ni nini huwa kinawakumba?

Ninatambua uzoefu ni msingi mzuri wa matokeo makubwa ya kiutendaji lakini kujaribu njia nyingine pia ni jambo jema na linaweza kuleta matokeo chanya kwenye utendaji.

Tumshauri Rais ikimpendeza aangalie kwenye uteuzi vijana ambao hawana uzoefu lakini wana kipawa Cha uongozi ' hawa ni watu 'potential' sana na wanaweza kusaidia kuleta matokeo makubwa Kwa sababu:

i. Vijana wanapoaminiwa kuongoza taasisi watatumia Kila mbinu kusaidia taasisi kukua Kwa sababu ndani ya ufahamu wao wataamini matokeo ndio yatakayowabeba

ii. Vijana ni watu wa matokeo, watapambana kufanikisha matokeo na 'spirit' ya kutaka matokeo itasaidia kuleta ufanisi ndani ya Taasisi husika. Mfano ni makonda

iii. Vijana wana uthubutu na utayari wa kujaribu mawazo mapya ili kuona matokeo makubwa.

iv. Mtazamo wa vijana kwenye mambo mengi ni wa kileo na kisasa, mabadiliko mengine yanakuja Kwa kuendana na usasa. Vijana watakuja na mbinu na mikakati ya kisasa.

Kwa kuwa lengo la mada hii ni ushauri Kwa Rais wetu, Kwa namna ya pekee kabisa namshauri Rais aangalie vijana wenye utayari na kipwa Cha uongozi na sio lazima awe na uzoefu mkubwa kwenye nafasi ya Kamishna wa NCAA , naamini mtu wa namna hii atatusaidia kukuza utalii na kuongeza mapato na fedha za kigeni.
Aanze na Mimi GENTAMYCINE hatojutia.
 
Kipimo gani utatumia kujua hilo kuwa huyu ana akili ya asili
Uwezo binafsi wa kuchakata na kutatua changamoto kwa ufanisi wa mambo ya kila siku katika maisha.

Unaweza kukuta mtu ameishia darasa la 4 ila watu wanaenda kwake kutafuta hekima, maarifa na jinsi ya kutatua changamoto za kila siku na huyo anatoa namna iliyo bora kabisa, hivyo tambua huyo ana akili kubwa ya asili kuliko msomi mwenye PHD ambaye hawezi tumia maarifa aliyoyapata japo kujiajiri tu.

Pia kila mtoto katika makuzi, jamii huwa inatambua watoto wote wenye tabia za tofauti ambao wanafanya vitu tofauti na wenzao, hivyo ukifuatilia hilo, linatosha pia kukujuza nani ana akili kubwa ya asili kuliko wengine.
 
Unaweza kukuta mtu ameishia darasa la 4 ila watu wanaenda kwake kutafuta hekima, maarifa na jinsi ya kutatua changamoto za kila siku na huyo anatoa namna iliyo bora kabisa, hivyo tambua huyo ana akili kubwa ya asili kuliko msomi mwenye PHD ambaye hawezi tumia maarifa aliyoyapata japo kujiajiri tu.
Hiki kipimo chako kigumu kukielewa sababu hizo kazi wajumbe wa nyumba kumi na viongozi wa serikali za mitaa nchi nzima ndio kazi zao watu hufurika kwao kutafuta ufumbuzi
 
Hiki kipimo chako kigumu kukielewa sababu hizo kazi wajumbe wa nyumba kumi na viongozi wa serikali za mitaa nchi nzima ndio kazi zao watu hufurika kwao kutafuta ufumbuzi
Kwa viongozi hao hawafuati busara, hekima wala utatuzi wa amani bali kutafuta usuluhishi kwa mjibu wa kanuni, taratibu, miongozo na sheria.

Haujawahi jiuliza kwa nini flani akitoa maelekezo watu wote wanamsikiliza na kufuata huku huyo mtu akiwa ni raia wa kawaida tu?, umewahi jiuliza uwezo huo kautoa wapi ilihali kauli hiyohiyo ingetolewa na mwingine isingezingatiwa?.

Haujawahi ona mtoto mdogo tu anafanya vitu mpaka watu wanashangaa?.

IQ haitegemei kiwango cha taaluma mtu alicho nacho bali ni kitu cha kuzaliwa nacho kiasili, hivyo usitegemee makaratasi yakawa kipimo pekee cha kutambua wenye IQ kubwa au ndogo.
 
Hao vijana mnaowazungumzia kumshauri Rais aangalie kuwateua, hawapo hapa Tanzania..wapo wenye akili za kwenye makaratasi, walalamikaji wategemezi na wasaka fursa!
 
Kuna baadhi ya watu wamekuwa viongozi wa mashirika makubwa duniani katika umri wa miaka 20 mpaka 30 na wamefanya vizuri sana. Mtu mwenye miaka 20 sidhani kama ana uzoefu mkubwa
Vijana wadogo wanaoongoza kampuni kubwa ulaya na marekami hata hapa Tanzania tunao kampuni mfano kubwa za wahindi na waarabu na wapemba vijana wao wadogo husimami biashara zao za familia.Lakini.sababu hukulia ndani ya kampuni wanazijua toka wadogo wanashinda na wazazi wao wanaachiwa kampuni hivyo uwezo wake wa kuendesha kampuni.unakuwa mkubwa sana

Lakini hata ulaya na marekani huwezi kuta kijana anaongoza kampuni ya serikali ni watu wazima .Kwanza serikali huwa hazina kampuni nyingi zaidi ya kampuni chache kama posta reli na umeme chache sana na viongozi wengi huwa watu wazima sana sababu wana.mifumo.kama yetu kwenye kampuni za umma unapanda taratibu

Hata majeshini au polisi ulaya na marekani polisi.au mwanajeshi mkubwa huwezi mkuta kijana.

Ila kampuni binafsi wapo .Hata Tanzania wajukuu vijana wadogo wa bhakresa wanadimamia vitengo vikubwa tu kwenye kampuni.Wamekulia humo wanajua.Lakini sisi shida huwezi okata tu kijana kuwa hajasoma hata udereva hajui hata kuendesha gari unamwambia wewe ndie utakuwa Transport Manager una akili ya asili sio kweli
 
Hao vijana mnaowazungumzia kumshauri Rais aangalie kuwateua, hawapo hapa Tanzania..wapo wenye akili za kwenye makaratasi, walalamikaji wategemezi na wasaka fursa!
Nakubaliana na wewe mtu kama kweli ana akili.ya asili cha kwanza aitoe familia yake kwenye umaskini.Sababu mfano wachaga wanaamini akili ni kitu kinachoonekana

Mchaga anakwambia wewe kama una akili nionyeshe una shilingi ngapi kwenye akaunti,una gari ,una nyumba una biashara gani
Mchaga mtu akisema nina akili anamwambia onyesha vilivyozalishwa na hiyo akili yako iwe nyumba,gari zuri nk sio ohh mimi nina akili unaongea kaa mlevi

Unatakiwa kuonyesha vitu tangible vinavyoonekana physically vya kubadili maisha yako meenyewe na familia yako
 
Back
Top Bottom