Waliosomea shahada ya mifugo, misitu, kilimo, kuitwa Afisa mifugo, afisa misitu, afisa kilimo. Lakini waliosomea shahada ya elimu hawaitwi afisa elimu

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,663
18,037
Hii imekaaje? Waliosomea nyanja ya mifugo, misitu, kilimo, uuguzi, nk katika ngazi ya shahada na kuendelea hutambuliwa kama maafisa katika nyanja zao kama vile afisa mifugo, afisa misitu, afisa kilimo, afisa uuguzi nk, na jamii kukubali kuwa wanastahili kutunukiwa uafisa katika maeneo yao ya utaalamu.

Linapokuja suala la waliosomea nyanja ya ELIMU katika ngazi ya shahada ikaonekana HAWASTAHILI KUITWA MAAFISA katika eneo lao la utaalamu!! Waitwe tu waalimu!

Hapo awali walikuwa wanaitwa maafisa elimu, lakini WAKAFUTIWA hadhi hiyo ya uafisa!! Sielewi kitu gani kinafanya walimu wabaguliwe hivyo kwa wazi kabisa!

Hii ni dharau kubwa kwa wataalamu wetu wa elimu, halafu watu wanashangaa kwa nini elimu yetu inashuka!
 
Tafuta hela acha kulialia mwalimu.

#MaendeleoHayanaChama
Siongelei habari ya hela, naongelea kuhusu heshima. Walimu hawaheshimiwi na jamii yetu, haiheshimiwi na viongozi. Kama ni pesa hakuna tofauti kati ya mshahara wa aliyesomea elimu na yule aliyesomea kwa mfano kilimo, ustawi wa jamii nk. Lakini kwenye jamii bado mwalimu anaonekana hastahili hadhi anayostahili mwenzake aliyesomea nyanja nyingine.
 
Hii imekaaje? Waliosomea nyanja ya mifugo, misitu, kilimo, uuguzi, nk katika ngazi ya shahada na kuendelea hutambuliwa kama maafisa katika nyanja zao kama vile afisa mifugo, afisa misitu, afisa kilimo, afisa uuguzi nk, na jamii kukubali kuwa wanastahili kutunukiwa uafisa katika maeneo yao ya utaalamu. Linapokuja suala la waliosomea nyanja ya ELIMU katika ngazi ya shahada ikaonekana HAWASTAHILI KUITWA MAAFISA katika eneo lao la utaalamu!! Waitwe tu waalimu! Hapo awali walikuwa wanaitwa maafisa elimu, lakini WAKAFUTIWA hadhi hiyo ya uafisa!! Sielewi kitu gani kinafanya walimu wabaguliwe hivyo kwa wazi kabisa! Hii ni dharau kubwa kwa wataalamu wetu wa elimu, halafu watu wanashangaa kwa nini elimu yetu inashuka!
Hapana walimu wote mwenye degree wanaitwa maafisa elimu
 
Mleta mada ana hoja,na ni kweli hawaitwi maafisa elimu badala yake hicho ni cheo cha kiutendaji na si kwa ajili ya elimu (shahada).tuliweke sawa hili kwa mwenye uelewa atuweke sawa
 
Hii imekaaje? Waliosomea nyanja ya mifugo, misitu, kilimo, uuguzi, nk katika ngazi ya shahada na kuendelea hutambuliwa kama maafisa katika nyanja zao kama vile afisa mifugo, afisa misitu, afisa kilimo, afisa uuguzi nk, na jamii kukubali kuwa wanastahili kutunukiwa uafisa katika maeneo yao ya utaalamu. Linapokuja suala la waliosomea nyanja ya ELIMU katika ngazi ya shahada ikaonekana HAWASTAHILI KUITWA MAAFISA katika eneo lao la utaalamu!! Waitwe tu waalimu! Hapo awali walikuwa wanaitwa maafisa elimu, lakini WAKAFUTIWA hadhi hiyo ya uafisa!! Sielewi kitu gani kinafanya walimu wabaguliwe hivyo kwa wazi kabisa! Hii ni dharau kubwa kwa wataalamu wetu wa elimu, halafu watu wanashangaa kwa nini elimu yetu inashuka!
Umewahi kujiuliza maana ya neno "mwalimu" ?
 
Hapana walimu wote mwenye degree wanaitwa maafisa elimu
Ilikuwa zamani. Baadaye waligeuza na kuitwa waalimu kwa madaraja mbali mbali.

Mwalimu Daraja la III C - Mwenye Shahada ya Ualimu somo la Physics, Mathematics, Chemistry na Biology; v. Mwalimu Daraja la III C - Mwenye Shahada ya Ualimu wa somo la English Language, English Literature, Chinese Language, French Language na Kiswahili; vi. Mwalimu Daraja la III C - Mwenye Shahada ya Ualimu somo la Commerce, Accountancy na Economics.

AFISA MUUGUZI DARAJA LA II. Waombaji wawe na Shahada ya Uuguzi kutoka Chuo Kikuu kinachotambuliwa na Serikali.

Unaona hapo! Wote wana shahada!! Kimsingi hakuna shahada ya ualimu!! Lakini ili kufunika uovu, wanalazimisha aliyesomea shahada ya elimu iitwe shahada ya ualimu!! Kimsingi inaitwa Bachelor of Education in Science au Bachelor of Education in Arts. Au Bachelor of Science (Education).

Hayupo mtu mwenye shahada ya Ualimu somo la Physics, Mathematics, nk. Vyuo vinavyofundisha ualimu ni ngazi ya cheti na Stashahada tu!! Hawa Tamisemi wakoje?
 
IMG_9839.jpg

Maafisa Elimu wakipata chakula cha mchana siku ya tarehe moja mwezi huu baadae watashushia matikiti maji warudi makwao
 
Walimu hawana strategy za kudai haki zao halafu kila walipo ni fujo angalia mishahara ikitoka wao ndio wa kwanza kujaa benki idara nyingine wako zao taratibu tu
Walimu hawana posho ndiyo maana wanategemea mishahara 100%, sitaki kuwalaumu CCM imewageuza kuwa tegemezi
 
Siongelei habari ya hela, naongelea kuhusu heshima. Walimu hawaheshimiwi na jamii yetu, haiheshimiwi na viongozi. Kama ni pesa hakuna tofauti kati ya mshahara wa aliyesomea elimu na yule aliyesomea kwa mfano kilimo, ustawi wa jamii nk. Lakini kwenye jamii bado mwalimu anaonekana hastahili hadhi anayostahili mwenzake aliyesomea nyanja nyingine.
Heshima utaipata kwenye familia yako
 
Back
Top Bottom