Kuna sakata linafukuta kuhusu uuzaji kiholela wa nyumba 12 za serikali huko mbeya, mambo yako hivi:
1.0, serikali kupitia wizara ya miundo mbinu inamiliki nyumba 12, eneo la RRM nje kidogo ya jiji la mbeya, nyumba hizi zilizojengwa kwa archtecture ya kiyugoslavia, zilijengwa na kampuni ya kiyugoslavia inayoitwa partzank put, wakati wanajenga barabara ya igurusi-songwe miaka ya 1992. walipomaliza ujenzi walizikabidhi nyumba hizi serikalini, yaani wizara ya ujenzi
2.0 nyumba hizi zinakaliwa na watumishi wa muda mrefu wa serikali mjini mbeya, na ziko 12 kwenye compound moja
3.0, wakati wa uuzaji wa nyumba za serikali, watumishi hawa waliomba na kukubaliwa na wakauziwa kwa bei ya soko, wengi wa watumishi hawa ni wa kada ya kati wakiwepo wahandisi
4.0 wengi wamemaliza kulipa, na walipoanza process za kuomba hati miliki wakakutana na kigongo hiki kuwa hati haitaweza kutolewa kwa kuwa, nyumba hizo aliuziwa mama ana mkapa na ndo mmliki halali, TAYARI ANA MKAPA ANA HATI YA ENEO LOTE LENYE NYUMBA 12
5. mtu mmoja aitwae zongo, ambaye alikuwa afisa ardhi wa the then manispaa ya mbeya, na ambaye inasemekana ni mtu wa karibu na mama ana mkapa ndo aliyefanikisha huu ufisadi
kwa maana hiyo, manispaa ya mbeya imeuza nyumba isizomiliki kwa mtu asiyestahili, na kwa gharama za wafanyakazi wa serikali wliostahili. mmiliki halaili ni katibu mkuu, wizara ya ujenzi
waliozulumika katika zoezi hili wameniomba nilete hili swala hapa jf kuomba msaada wenu wakuu