Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 37,200
- 86,413
Hamjambo!
1. Dc Magoti japokuwa anapenda kuongea kwa misifa, majigambo, na kidogo utani Jambo ambalo wakati mwingine anatoaga Boko. Round hii ninaungana naye kwenye hoja yake hii;
2. Mamlaka hailalamiki. Mamlaka inayolalamika hiyo sio mamlaka.
3. Kauli hiyo ameitoa huku akiwahusisha Wanaume kama watu waliopewa Mamlaka ya kuongoza Mke, watoto na Familia kwa ujumla.
4. Hata Sisi Watibeli falsafa zetu zinamtaka Mwanaume au mwenye mamlaka kutokuwa MTU wa kulalamika Bali kuchukua hatua.
5. Mamlaka ni kuchukua hatua stahiki kwa maslahi ya Mamlaka husika na wale unaowaongoza.
6. Oooh! mke wangu haagi. Nini wewe! Kwamba mkeo haagi hujui chakufanya?
Huna maamuzi? Huna Sheria? Hujui kuongoza?
7. Ooh mke wangu akinuna tuu anaenda kwao. Heee! My friend nafikiri huyo mkeo ndio angepaswa awe Mwanaume alafu wewe uwe jike ili uone yeye angefanyaje.
8. Oooh! Mke wangu anakiburi. Hivi unajua maana ya mamlaka. Hivi uliwahi kuona kiburi kikizidi mamlaka? Nafikiri hujui maana ya Mamlaka.
9. Mamlaka yenye nguvu ipo tayari kufukuza yeyote bila kusita, bila kujali. Bila woga WA kufikiri matokeo. Mtu yeyote ambaye yupo kinyume na Mamlaka.
10. Mwanaume mzima ati unabembeleza Mke mjeuri, kiburi au msaliti. 😆 Hahaha! Kwamba Mamlaka ikubembeleze?
Alafu mamlaka hiyohiyo inatoa chakula, mavazi, na huduma zingine. Hiya labda mamlaka ya Misukule.
11. Usiogope wala kujishauri kupiga chini mtu yeyote asiyekuheshimu. Kwenye familia lazima Baba au mwanaume uhakikishe mambo yote yanaenda sawasawa na matakwa na sheria zako.
12. Mamlaka haiingiliwi. Unapoongoza mamlaka yako. Ukiwawajibisha watu wako hasa wasio na adabu lakini kwa Haki. Usiruhusu watu wa nje ya kukuamulia.
13. Sisi Watibeli, hata kama kuna Watibeli wenye Imani ya Kikristo. Kuna mafundisho hatuyafuati kabisa. Mfano fundisho la kutotoa talaka. Sisi mwanamke akikosa Adabu, na kuvunja baadhi ya Sheria zetu kuu atafukuzwa tuu. Bila kujali imeandikwa wapi, imesemwa na nani, hivyo yaani.
14. Mamlaka haiogopi kuanza Upya. Kufuta na kuanza upya.
15. Hakuna cha tunawatoto wangapi, hakuna tumeishi miaka mingapi, ukizingua unafukuzwa. Tunaanza upya...!
16. Uanaume sio tuu jinsia bali tabia za kifalme na kimamlaka
17. Sio Kulialia kama mtoto au kama mwanamke hapa!
Ijumaa Kareem
TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam
1. Dc Magoti japokuwa anapenda kuongea kwa misifa, majigambo, na kidogo utani Jambo ambalo wakati mwingine anatoaga Boko. Round hii ninaungana naye kwenye hoja yake hii;
2. Mamlaka hailalamiki. Mamlaka inayolalamika hiyo sio mamlaka.
3. Kauli hiyo ameitoa huku akiwahusisha Wanaume kama watu waliopewa Mamlaka ya kuongoza Mke, watoto na Familia kwa ujumla.
4. Hata Sisi Watibeli falsafa zetu zinamtaka Mwanaume au mwenye mamlaka kutokuwa MTU wa kulalamika Bali kuchukua hatua.
5. Mamlaka ni kuchukua hatua stahiki kwa maslahi ya Mamlaka husika na wale unaowaongoza.
6. Oooh! mke wangu haagi. Nini wewe! Kwamba mkeo haagi hujui chakufanya?
Huna maamuzi? Huna Sheria? Hujui kuongoza?
7. Ooh mke wangu akinuna tuu anaenda kwao. Heee! My friend nafikiri huyo mkeo ndio angepaswa awe Mwanaume alafu wewe uwe jike ili uone yeye angefanyaje.
8. Oooh! Mke wangu anakiburi. Hivi unajua maana ya mamlaka. Hivi uliwahi kuona kiburi kikizidi mamlaka? Nafikiri hujui maana ya Mamlaka.
9. Mamlaka yenye nguvu ipo tayari kufukuza yeyote bila kusita, bila kujali. Bila woga WA kufikiri matokeo. Mtu yeyote ambaye yupo kinyume na Mamlaka.
10. Mwanaume mzima ati unabembeleza Mke mjeuri, kiburi au msaliti. 😆 Hahaha! Kwamba Mamlaka ikubembeleze?
Alafu mamlaka hiyohiyo inatoa chakula, mavazi, na huduma zingine. Hiya labda mamlaka ya Misukule.
11. Usiogope wala kujishauri kupiga chini mtu yeyote asiyekuheshimu. Kwenye familia lazima Baba au mwanaume uhakikishe mambo yote yanaenda sawasawa na matakwa na sheria zako.
12. Mamlaka haiingiliwi. Unapoongoza mamlaka yako. Ukiwawajibisha watu wako hasa wasio na adabu lakini kwa Haki. Usiruhusu watu wa nje ya kukuamulia.
13. Sisi Watibeli, hata kama kuna Watibeli wenye Imani ya Kikristo. Kuna mafundisho hatuyafuati kabisa. Mfano fundisho la kutotoa talaka. Sisi mwanamke akikosa Adabu, na kuvunja baadhi ya Sheria zetu kuu atafukuzwa tuu. Bila kujali imeandikwa wapi, imesemwa na nani, hivyo yaani.
14. Mamlaka haiogopi kuanza Upya. Kufuta na kuanza upya.
15. Hakuna cha tunawatoto wangapi, hakuna tumeishi miaka mingapi, ukizingua unafukuzwa. Tunaanza upya...!
16. Uanaume sio tuu jinsia bali tabia za kifalme na kimamlaka
17. Sio Kulialia kama mtoto au kama mwanamke hapa!
Ijumaa Kareem
TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam