Mkuu Deus Mallya, kwanza asante kwa kuamua kutaka kusema!. Kwenye jamii yetu, tuna watu wa jinsia mbili, ya kiume na ya kike!. Watu wa jinsia hizo wanakuwa na tabia na mienendo inayoendana na tabia zao. Yaani mwanaume anakuwa na tabia za kiume, na mwanamke anakuwa na tabia za kike!. Ila pia hutokea baadhi ya wanaume, kuzaliwa wanaume na maumbile ya kiume lakini wakawa na tabia za kike!, vivyo hivyo kuna wanawake wenye maumbile ya kike na tabia za kiume!.
Moja ya tabia za kiume kwa mwanamume ni kuwa na msimamo thabiti, msimamo imara, akiamua kitu, ameamua na anasimama nacho mpaka mwisho wake, na ikibidi kufa, anakufa na msimamo wake huku akiitwa shujaa!. Sasa wewe kama ni mwanamume na unazo tabia za kiume, ulipoamua kukaa kimya na kunyamaza, ni lazima uendelee kukaa kimya na kunyamaza mpaka mwisho!.
Hili tishio la oh mara ntasema, au wakati wa kusema umefika!, hizi ni tabia za kike!, mwanamume akiamua kusema, hasemi ntasema bali husema!. Mwanamke ndio huamua kutishia aseme au asiseme, na hata akitong..zwa anajijua kabisa amekubali, atajifanya hataki ili uonyeshe kuhangaika kumpata!.
Hii ya wewe kutishia kuwa utasema, its as if ulilipwa kiasi fulani hapo mwanzo ili unyamaze, na ukanyamaza, sasa umeishiwa, unataka kuendelea kulipwa siku zote kwa kukaa kimya!, yaani ukimwa wako ndio ajira yako, ili uendelee kulipwa, unatishia kusema ili watishike na kukulipa tena ili usiseme, ukae kimya!.
Nakushauri, kama umeamua kweli kusema, amua moja na useme sasa!, hukupaswa kusema utasema, ulipaswa useme tuu tujue moja, kitendo cha kutishia nyau kuwa utasema, kinaweza kupelekea wale waliokulipa siku zote kukaa kimya, wakakuona you are not an asset, you are a liability which needs disposal kabla haijawa too risky or threat, hivyo ukanyamazishwa jumla!.
Ni ushauri tuu.
Asante.
Pasco.