Nilikuwa nauliza ndugu zangu naomba kupata ufafanuzi wa hili jambo binafsi linanichanganya hawa wajumbe wa Serikal za mitaa au balozi wa nyumba kumi ndio hao hao wajumbe wa chama (CCM)?
Kuna wajumbe wa nyumba kumi. Hawa ni CCM tu walio na utaratibu huu ambao umeanza tangu zama za chama kimoja.
Kisha kuna wajumbe wa serikali ya Mtaa. Hawa hupigiwa kura na watu wote.
Mkanganyiko ni pale unapokwenda serikali ya Mtaa unaulizwa mjumbe wako wa nyumba kumi ni nani na kutakiwa upate barua ya utambulisho kutoka kwake.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.