Nimepitia karibu comment zote zilizotangulia humu
Nilichogundua waTanzania wengi hatupendi kujifunza na kuchukua hatua
Mimi ni Mkristo ila sio kila kitu kwenye ukristo nakiamini! Na hii ni baada ya kujifunza baadhi ya vitu nikiwa na "open mind"! Unajifunza kitu pasipo kufungwa na hisia au kushikilia ulichokwisha aminishwa!
Mfano, mpaka leo kuna watu wanabandika picha za yule mzungu aliyeigiza picha ya Yesu kwamba ndio Yesu Mwenyewe! Na huwaambii chochote wakakuelewa maana hata baadhi ya vitu vya dini vina picha yake! (Angalau siku hizi waandishi wengi hawaitumii)
Mpaka leo kuna watu ukiwaambia padri fulani amezaa na mwanamke fulani watatamani kukupiga mawe! Hawaamini kitu kama hicho! Wanasahau kwamba sote ni binadamu!
Na hayo ni madhara ya mapokeo ya hizi dini! Tuliaminishwa sana vitu visivyo na uhalisia!
Kwa mfano, wenzetu waislam wanaamini ukitoa Swadaka ya kujenga Msikiti wewe tayari umeshaiona pepo! Yaani kwa Swadaka ya Msikiti tayari umetengeneza njia ya kufika peponi bila kujalisha Maisha yako mengine yakoje!
Kuna vitu hutakiwi kuvimeza kama vilivyo! Kuna vingine unatakiwa utafune, tena vingine utafune kwa uangalifu maana vinaweza kuwa na vipande vya mawe ukatakiwa uteme!
Kwa mfano, Mimi nilishawahi kuhoji! Ukiangalia mitaani hasa Morogoro mjini karibu kila mtaa kuna msikiti na pengine mtaana mmoja kuna misikiti hadi mitatu!
Ukiangalia sio kwamba huwa inajaa yote na wala sio kwamba iko mbali mbali kiasi cha kusema watachelewa wale wanaoswali swala tano! Jibu ni Hapana! Ipo karibu karibu tu!
Cha zaidi utakuta kila Msikiti una jina lake! Huu Msikiti wa fulani na ule Msikiti wa fulani.
Halafu mtaa huo huo utakuta hamna hata zahanati. Wote wakipata shida utakuta wanakutanikia zahadi moja kiasi cha kukaa foleni kwa muda mrefu na kupoteza muda mwingi wa kufanya shughuli nyingine.
Ukienda shule ya msingi au sekondari iliyopo ndani ya kata husika (ambamo kuna misikiti kibao) utakunana na shule moja, yenye upungufu mkubwa wa madarasa, yenye mrundikano mkubwa wa wanafunzi wasio na madawati ya kukalia kitu kinachopelekea ufaulu hafifu!
Unakutana na shule inazaidi ya miaka mitano wahitimu wake hakuna aliyewahi kupata division one na wanaopata division two ni kuanzia watatu hadi watano Kati ya wahitimu zaidi ha 150!
Mbaya zaidi wakishatoka hapo, hakuna hata vyuo vya ufundi watakavyokutana navyo huko msikitini!
Ni kweli kabisa serikali haijengi misikiti wala makanisa hivyo ni jukumu la waumini kujenga nyumba zao za ibada. Lakini hili haliwanyimi fursa waumini hao hao kujenga shule, vyuo, hospital kwa ajili ya maendeleo ya waumini wao na jamii nzima kwa ujumla
Tanzania kuna madhehebu mengi sana, lakini yenye waumini wengi nadhani ni mawili! Uislam na Ukatoliki
Hawa maana yake wanawaumini wengi. Kwa maana nyingine hata huko mashuleni kuna waumini wao wengi. Hospital kuna waumini wao wengi wanaenda kutibiwa huko
Kuna shida gani mtaa ukiwa na Msikiti mmoja halafu badala ya kuongeza misikiti mingine miwili (ambapo sio kwamba huo wa kwanza unajaa) wakajenga shule au zahanati?
Tunaaminishwa kwamba mambo ya Imani za watu sio vizuri kuyahoji, lakini hii sioni kama ni sahihi kwasababu walio kuja na hizi dini ndio hao hao wanatukazania tuache kuhoji hoji baadhi ya mambo.
Mwenyezi Mungu anatupenda sana, ametupa akili ili tuzitumie. Hakuna mipaka ya kuhoji kwasababu anayehoji anatafuta maarifa au majibu ya kutatua tatizo fulani
Wao walipokuja huku walihoji Imani za Babu zetu wakaziita Imani potofu! Kwanini sisi tuamini tu wao wako sahihi kwenye kila jambo? Inamaana wao walipewa akili nyingi kuliko sisi? Hii sio sahihi! Kuna vitu vingi tu wanataka tuvitimize kwa kigezo cha Imani za dini za kutohoji baadhi ya mambo
Kwamba ukijenga shule au hospital wakatumia wote wenye dini na wasio na dini peponi panakuwa mbali!?
Kwamba kukikwa na Msikiti kila baada ya mita kumi ndio kumfarahisha Mungu wakati jamii hiyo hiyo yenye Msikiti kila baada ya mita kumi kuna janga la umasikini, watu wake wakiumwa watahitaji kutembea zaidi ya kilometa kadhaa kufuata huduma na watalazimika kuisubiria kwa masaa kadhaa.
Watu hao hao watoto wao hawana shule za chekechea, wana shule moja ya msingi mkondo mmoja wanafunzi 100 na robo tatu wanakaa chini
Watu hao hao wanashule moja ya sekondari ya kata yenye uhaba mkubwa wa madawati, matundu ya vyoo hayatoshi, hakuna maji, mkondo mmoja wanakaa wanafunzi zaidi ya 90 !
Sent using
Jamii Forums mobile app