Waislam nijibuni hili

Waislam nijibuni hili

Toka enzi na enzi kipau mbele cha waislamu ni elimu ahera elimu dunia na maendeleo mengine ni kitu cha badae ndo maana ukifuatilia viongozi wengi wa zamani ambao ni waislamu ukifuatilia elimu zao wamezipata kwenye shule za wakristo.
 
Wewe wakijenga misikiti inakuuma nini? Probably their priority sio maisha ya dunia hii, unafikili kila MTU ana fikra kama zako? Wengine priority yao ni mahusiano yao na Mungu wao. Stay back and chill, achana na dini za watu.
 
Nimepitia karibu comment zote zilizotangulia humu

Nilichogundua waTanzania wengi hatupendi kujifunza na kuchukua hatua

Mimi ni Mkristo ila sio kila kitu kwenye ukristo nakiamini! Na hii ni baada ya kujifunza baadhi ya vitu nikiwa na "open mind"! Unajifunza kitu pasipo kufungwa na hisia au kushikilia ulichokwisha aminishwa!

Mfano, mpaka leo kuna watu wanabandika picha za yule mzungu aliyeigiza picha ya Yesu kwamba ndio Yesu Mwenyewe! Na huwaambii chochote wakakuelewa maana hata baadhi ya vitu vya dini vina picha yake! (Angalau siku hizi waandishi wengi hawaitumii)

Mpaka leo kuna watu ukiwaambia padri fulani amezaa na mwanamke fulani watatamani kukupiga mawe! Hawaamini kitu kama hicho! Wanasahau kwamba sote ni binadamu!

Na hayo ni madhara ya mapokeo ya hizi dini! Tuliaminishwa sana vitu visivyo na uhalisia!

Kwa mfano, wenzetu waislam wanaamini ukitoa Swadaka ya kujenga Msikiti wewe tayari umeshaiona pepo! Yaani kwa Swadaka ya Msikiti tayari umetengeneza njia ya kufika peponi bila kujalisha Maisha yako mengine yakoje!

Kuna vitu hutakiwi kuvimeza kama vilivyo! Kuna vingine unatakiwa utafune, tena vingine utafune kwa uangalifu maana vinaweza kuwa na vipande vya mawe ukatakiwa uteme!

Kwa mfano, Mimi nilishawahi kuhoji! Ukiangalia mitaani hasa Morogoro mjini karibu kila mtaa kuna msikiti na pengine mtaana mmoja kuna misikiti hadi mitatu!

Ukiangalia sio kwamba huwa inajaa yote na wala sio kwamba iko mbali mbali kiasi cha kusema watachelewa wale wanaoswali swala tano! Jibu ni Hapana! Ipo karibu karibu tu!

Cha zaidi utakuta kila Msikiti una jina lake! Huu Msikiti wa fulani na ule Msikiti wa fulani.

Halafu mtaa huo huo utakuta hamna hata zahanati. Wote wakipata shida utakuta wanakutanikia zahadi moja kiasi cha kukaa foleni kwa muda mrefu na kupoteza muda mwingi wa kufanya shughuli nyingine.

Ukienda shule ya msingi au sekondari iliyopo ndani ya kata husika (ambamo kuna misikiti kibao) utakunana na shule moja, yenye upungufu mkubwa wa madarasa, yenye mrundikano mkubwa wa wanafunzi wasio na madawati ya kukalia kitu kinachopelekea ufaulu hafifu!

Unakutana na shule inazaidi ya miaka mitano wahitimu wake hakuna aliyewahi kupata division one na wanaopata division two ni kuanzia watatu hadi watano Kati ya wahitimu zaidi ha 150!

Mbaya zaidi wakishatoka hapo, hakuna hata vyuo vya ufundi watakavyokutana navyo huko msikitini!

Ni kweli kabisa serikali haijengi misikiti wala makanisa hivyo ni jukumu la waumini kujenga nyumba zao za ibada. Lakini hili haliwanyimi fursa waumini hao hao kujenga shule, vyuo, hospital kwa ajili ya maendeleo ya waumini wao na jamii nzima kwa ujumla

Tanzania kuna madhehebu mengi sana, lakini yenye waumini wengi nadhani ni mawili! Uislam na Ukatoliki

Hawa maana yake wanawaumini wengi. Kwa maana nyingine hata huko mashuleni kuna waumini wao wengi. Hospital kuna waumini wao wengi wanaenda kutibiwa huko

Kuna shida gani mtaa ukiwa na Msikiti mmoja halafu badala ya kuongeza misikiti mingine miwili (ambapo sio kwamba huo wa kwanza unajaa) wakajenga shule au zahanati?

Tunaaminishwa kwamba mambo ya Imani za watu sio vizuri kuyahoji, lakini hii sioni kama ni sahihi kwasababu walio kuja na hizi dini ndio hao hao wanatukazania tuache kuhoji hoji baadhi ya mambo.

Mwenyezi Mungu anatupenda sana, ametupa akili ili tuzitumie. Hakuna mipaka ya kuhoji kwasababu anayehoji anatafuta maarifa au majibu ya kutatua tatizo fulani

Wao walipokuja huku walihoji Imani za Babu zetu wakaziita Imani potofu! Kwanini sisi tuamini tu wao wako sahihi kwenye kila jambo? Inamaana wao walipewa akili nyingi kuliko sisi? Hii sio sahihi! Kuna vitu vingi tu wanataka tuvitimize kwa kigezo cha Imani za dini za kutohoji baadhi ya mambo

Kwamba ukijenga shule au hospital wakatumia wote wenye dini na wasio na dini peponi panakuwa mbali!?

Kwamba kukikwa na Msikiti kila baada ya mita kumi ndio kumfarahisha Mungu wakati jamii hiyo hiyo yenye Msikiti kila baada ya mita kumi kuna janga la umasikini, watu wake wakiumwa watahitaji kutembea zaidi ya kilometa kadhaa kufuata huduma na watalazimika kuisubiria kwa masaa kadhaa.

Watu hao hao watoto wao hawana shule za chekechea, wana shule moja ya msingi mkondo mmoja wanafunzi 100 na robo tatu wanakaa chini

Watu hao hao wanashule moja ya sekondari ya kata yenye uhaba mkubwa wa madawati, matundu ya vyoo hayatoshi, hakuna maji, mkondo mmoja wanakaa wanafunzi zaidi ya 90 !



Sent using Jamii Forums mobile app
 
changamoto za shule,zahanati, vyuo na kero chungu mzima ,jiongezeni
Hii kazi ya serikali ya CCM usiwapangie watu cha kufanya pesa za kununua ndege mnazo za maendeleo mnasubiri za msaada aibu kwenu.
 
kila panapo karibia uchaguzi, CCM hutoa ahadi kede kede kwa waislam na wao bila kutambua wanaingia chaka kwa ahadi za uongo, ma CCM wakiisha pata wanachokipa kutoka kwa waislam ( kura) & ungwaji mkono wanawaacha kwenye mataa wanalalama weeee lakini uchaguzi ukija tena walifanyiwa yale yale……….. adui mkubwa wa waislam ni CCM!
 
Ila wafanyabiashara wakubwa wa nchi hii wengi wao ni hao hao waislam ambao ndio ma giants wa kulipa kodi kubwa serikalini.Usisahau hilo mkuu.
Waislam utawambia kitu gani cha maendeleo wakuelewe? We chek biashara zinazozunguka miskiti afu ndo utaelewa: kalimati, vitumbua, miti shamba, udi/ubani, kanzu used ...

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaaani watu Wana jibu kwa mihemko tuu bila kujali Wana jibu nini

Lengo la mtoa MadA likikuwa zuri Sana

Kuna jamaa kasema kutoka kwenye din yao kuwa unatakiwa ufanye kitu ambacho kina Endelea kama ndivyo

Je zahanati vip?
Shule?

Kuna vitu vingine uki vitazama kwa undani ni ubaguzi frani tuu

Je naomba kuuliza ni Lazima sadaka atoaye mtu ni mhusus kwa watu wa dini yake tuu?



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Msiwaamshe waliolala, awali walimlaumu mwalimu kwa kutaifisha shule eti walikuwa wameanza kujipanga kwa kasi.."Al anuuri gazeti..",ili hali Wakristu ndio walikuwa wahanga zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilisikia na baadae kuona Mbwana Samatta katoa sadaka ya kujenga msikiti eneo lile lingetosha shule, hospital au kiwanda kidogo, kwa nini msikiti na pale kuna misikiti kibao ina maana zawadi ni msikiti tu hamtaki maendeleo zaidi ya misikiti?

Wakati nikiwa Morogoro nilishuhudia IGP Mstaafu Mzee Mahita akikabidhi msikiti licha ya eneo lile kuwa kubwa angeweza kujenga shule, zahanati au kitega uchumi chochote kitoe ajira watu wanufaike, nikajiuliza zawadi ya maana ni msikiti?

Misaada mingi ya mataifa ya kiislamu yaliyopiga hatua kama Qatar, Saudi Arabia,Brunei, Irani, Kuwait ,Oman na n.k wanaleta pesa wajenge misikiti mfano ule msikiti mkubwa pale Dodoma wa Gadaffi angeweza kujenga chuo, shule, zahanati na pale Dodoma misikiti ipo kibao kwa nini msikiti?

Juzi nimemuona msanii mkubwa yule ambaye angeweza kujenga shule pale Kigoma, zahanati au hata kiwanda amechoma pesa kwa kujenga msikiti na pale Kigoma misikiti imejaa kila mtaa hivi hakuna cha maana zaidi ya misikiti.

My take:
Kuna haja mjipange maana mnatumia nguvu kubwa kujaza misikiti lakini maeneo mnayokaa yamejaa changamoto za shule, zahanati, vyuo na kero chungu mzima.

Jiongezeni

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kile Chuo Kikuu Cha RUCO Yaani Rusha University College kabla ya hapo kilikuwa Chuo Cha Benki Amon Nsekela Institute, Serikali ikatangaza kuuza Roman Katoliki wakapeleka mapendekezo yao kukinunua na waliandika andiko kubwa kuelezea ikiwa watanunua premises hizo jamii itanufaikaje. Nao ndugu zetu Waislam wakapeleka maandiko yao wakielezea nini watakifanya ikiwa watafanikiwa kununua eneo lile. Romani Katoliki kama kawaida wakasema wao watakigeuza kuwa Chuo Kikuu. Na jamii yote itanufaika kusomesha watoto wao elimu ya juu bila kujali dini ya mtu. Hawa wenzetu Waislam nao kama ilivyo kawaida yao wakapeleka andiko kuwa wao watapageuza kuwa MADRASA kubwa Afrika Mashariki na kati na watajenga Msikiti mkubwa sana eneo hilo. Ikawa ndiyo hivyo tena.
Hisia zangu ni kwamba hata nyumba zao tusije kushangaa zote zikageukia kibla zikawa misikiti.
 
Nilisikia na baadae kuona Mbwana Samatta katoa sadaka ya kujenga msikiti eneo lile lingetosha shule, hospital au kiwanda kidogo, kwa nini msikiti na pale kuna misikiti kibao inamaana zawadi ni msikiti tu hamtaki maendeleo zaidi ya misikiti?

Wakati nikiwa Morogoro nilishuhudia IGP mstafu mzee mahita akikabidhi msikiti licha ya eneo lile kuwa kubwa angeweza kujenga shule, zahanati au kitega uchumi chochote kitoe ajira watu wanufaike ,nikajiuliza zawadi ya maana ni msikiti

Misaada mingi ya mataifa ya kiislamu yaliyopiga hatua kama Qatar, Saudi Arabia,Brunei, Irani, Kuwait ,Oman na n.k wanaleta pesa wajenge misikiti mfano ule msikiti mkubwa pale Dodoma wa ghadafi angeweza kujenga chuo,shule ,zahanati na pale Dodoma misikiti ipo kibao kwa nini msikiti?

Juzi nimemuona msanii mkubwa yule ambaye anhmgeweza kujenga shule pale kigoma,zahati au hata kiwanda amechoma pesa kwa kujenga msikiti na pale kigoma misikiti imejaa kila mtaa hivi hakuna cha maana zaidi ya misikiti.

My take
Kuna haja mjipange maana mnatumia nguvu kubwa kujaza misikiti lakini maeneo mnayokaa yamejaa changamoto za shule, zahanati, vyuo na kero chungu mzima, jiongezeni

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app

Hio kazi ya serikali inayo pokea kodi ni wajibu wao.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Wewe wakijenga misikiti inakuuma nini? Probably their priority sio maisha ya dunia hii, unafikili kila MTU ana fikra kama zako? Wengine priority yao ni mahusiano yao na Mungu wao. Stay back and chill, achana na dini za watu.
Punguza jazba muelewe alichosema kwa jicho la tatu. Kuna waislamu baadhi wanalalamika juu ya mfumo kristo kwamba unetawala tanzania viongozi wengi wa serikali ni wakristo hata teuzi za raisi nyingi ni wakristo sababu ndio hiyo aliyoitoa jamaa kuwa waislamu tupo bize na madrasa na misikiti bila kujenga shule na vyuo,hatukatai tusijenge misikiti lkn tukumbuke na shule na vyuo.

Vitu wanavyomiliki wakristo Tanzania ni St.thomas St mary st joseph chuo SAUT mwanza ruvuma mtwara st john dodomast francis chuo cha tumaini iringa st agnes chipole na kadha wa kadha.Haya tuje waislamu tuna mabasi yaendayo mikoani abood mashalah tawfiq pia tuna wasanii diamond kiba konde boy tid mnyama chid benz fid q msodoki mzee wa bwax manfongo shilole msaga sumu dulla makabila mo dweji azam bakharesa na nk.kwahiyo wao wanamiliki elimu sisi tunamiliki biashara na wasanii wavuta bangi.ndio mana wakristo wanatutawala kwa hiyo jamaa yupo sahihi kabisa inabidi tuamke tuanze kujenga shule zaidi vyuo vingi zaidi hii misikiti inatosha sasa.
 
Nenda Saudi Arabia,Dubai,Oman na Kuwait halafu tuone kama utarudia hii kauli yako ya kwamba hamuangalii mambo ya dunia

Sent using Jamii Forums mobile app
Nahisi una uvimbe kichwani. Hayo ya kwao lakini misaada wanayotoa inalenga kujenga akhera zao. Una jipya?!

Cᵃʳᵉᵉᵐ ᵀʰᵉ ᴸᵉᵍᵉⁿD
 
Mtoa mada sio wa kubezwa hata kidogo ana hoja ya msingi anahitaji majibu yenye kina
 
Mimi naunga mkono wazo la kujenga Misikiti mingi kila inapowezekana. Na ninashauri Ndugu Waislamu msiache kujenga Misikiti. Jengeni misikiti kila iitwapo leo ili kusaidia wajawake mnyaazi
 
Kingjr2, Nimeishia kusoma hapo uliposema "Kwa Tanzania kuna madhehebu makuu mawili! Uislam na Ukatoliki" rekebisha kwanza ili nirudi kuelendelea kusoma.

Cᵃʳᵉᵉᵐ ᵀʰᵉ ᴸᵉᵍᵉⁿD
 
Back
Top Bottom