Wadada, Mkisalimiwa Jibuni Salaam, Sio Kila Salaam Ina Ubaya Ndani Yake.

Mkuu hawa viumbe wanakera Sana,
Juzi kati nilikutana na dada mmoja kijijini kwetu ni miaka mingi sijaonana nae kwani alikuwa udsm anasoma

Basi bwana nikamuita kwa bashasha maana ni jirani yangu,,aliishia kunishusha tu duuh sikuamini aisee,,

Malipo apa apa duniani

#Jana kaja kuomba namba ya dada angu anatafuta connection nikamwambia ww hapa uondoke na ukiendelea kukaa napiga kelele unanishawishi tufanye ngono#

Kama alikaa tena

Watu mmevurugwa
 
Salaam/Shalom.

Kuna hili suala huwa linanishangaza sana, utakuta unamsalimia mtu halafu matokeo yake huyo unayemsalimia utakuta anakuangalia tu.

Huwa najiuliza sana hili swali, hivi mkijibu salaam huwa mnapungukiwa na kitu gani dada zangu...?

Leo nilikuwa Mount Meru Hospital kwa ajili ya kupima COVID 19 coz kuna kasafari kidogo cha nje, basi nikasema hebu ngoja nitoke nje ya geti nikanunue maji ya kunywa then nirudi ndani na muda wa kuona wagonjwa ulikuwa umeshaisha na askari akawa anazuia watu wasiingie.

Basi wakati natoka nje nikapishana na mdada mmoja mweupeeee anaingia ndani kumuona mgonjwa wake, nikamsalimia yule dada akawa ananiangalia tu, basi nikapishana nae nikanunua maji nikawa narudi ndani.

Nafika getini nikamkuta yule mdada amezuiwa kuingia ndani kwa kuwa muda wa kuona wagonjwa ulishaisha, basi nilivyofika getini askari akaniambia MKUU INGIA INGIA nikapita zangu nikamuacha yule mdada anamsihi, anambembeleza na kumuomba sana askari wa getini amruhusu aingie ndani kumuona mgonjwa wake, lakini bila ya mafanikio hakuweza kuingia ndani.

Ningeweza kumwambia tu askari MRUHUSU AINGIE na askari asingeuliza mara 2, ila unaanzaje kumuombea msaada mtu ambaye hata salaam yako ameshindwa kujibu akabaki anakuangalia tu...?

Matokeo yake ikabidi arudi nyumbani kama alivyokuja. Hivi, mnaposalimiwa then mkajibu salaam huwa mnapungukiwa na kitu gani dada zangu...?

Badilikeni aisee sio kila salaam ina ubaya ndani yake salaam nyingine zina baraka ndani yake, hivyo msiwe wenye kujikosesha baraka wenyewe kwa kushindwa kujibu kitu kidogo tu dada zangu. SALAAM.

NAWASILISHA.
Ubaya unalipwa kwa wema

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu hawa viumbe wanakera Sana,
Juzi kati nilikutana na dada mmoja kijijini kwetu ni miaka mingi sijaonana nae kwani alikuwa udsm anasoma

Basi bwana nikamuita kwa bashasha maana ni jirani yangu,,aliishia kunishusha tu duuh sikuamini aisee,,

Malipo apa apa duniani

#Jana kaja kuomba namba ya dada angu anatafuta connection nikamwambia ww hapa uondoke na ukiendelea kukaa napiga kelele unanishawishi tufanye ngono#

Kama alikaa tena

Aisee ni kweli kiongozi utakuta wanaleta dharau halafu baadae wanajikuta wamekwama hata pa kutokea hawana, ndio utaona wanavyotafuta huruma.

Ni shida sana kwa kweli...!
 
Sasa kwa nini wahusishe salaam na nia ya ngono...? Kwani salaam imekaa ki-ngono ngono mkuu...?
Nakumbuka mwaka Jana niliwahi msalimia mda mmoja njiani 'mambo dada angu' matokeo yake akanifyonya!! Halafu akanambia, "kawazoee hao hao Malaya uliowazoea"
Nikabaki najiuliza, kosa langu hapo ni lipi, Kuna mama mmoja alikuwa ni rafiki yake mama yangu, alikuja nyumbani, nikatambulishwa pale, yule mama akanambia "kama utaweza naomba nikupeleke nyumbani ukawe unanifundishia mwanangu"
Kweli, siku ya kwanza nimefika nikakakuta kavulana ka darasa la sita nikakafundisha, siku iliyofuata wakati namfundisha yule mtoto, yule mdada akaingia ndani, kumbe ni dada wa huyo mwanafunzi ninayemfundisha, mama yake akanitambulisha kwake!! Hiyo aibu iliyomjaa siku iyo bhana!! Nyie acheni tu!! Na Kwa hasira nilizonazo sikuwahi kuongea nae mpaka siku namaliza huo mkataba!! Ingawaje alikuwa ananipa salamu, ila namnyamazia tu!!
 
Mawazo ya mtu husadifu kile akisemacho au kukiandika, anyway nimekuelewa uwe na mchana mwema.
Nilichoandika sio mawazo,ni kitu kipo...mimi ni wa kike,nina marafiki wa kike wenye hizo tabia na wananipa hiyo sababu

Ninae rafiki hakubali salamu ya mwanaume asiye na gari
Kwake yeye mwanaume mwenye gari ndio mwenye haki ya kuongea nae
 
Binafsi ni afadhali Mtu anipite bila kunisalimia kuliko nimsalimie na asipokee salamu yangu !!

Pole sana Mkuu Niache Nteseke ila wadada wengi ni watu wa jinsi hiyo nadhani wanafikiri wasipoitikia salamu TOKA kwa ME basi hadhi yao inakuwa Bab-K....It's a stupidity behavior !!

Sure brother ni bora mara kumi tena, actually huwa nikimsalimia mtu mara moja hata kama tunaishia mtaa mmoja, asipoitikia tu basi hatakaa asikie sauti yangu hata siku 1.

Kuna wengine unakuta wanaonesha dharau at the same time unamkuta njiani au kituoni kasimama then hata lift huwezi kumpa, kiukweli huwa wanajikosesha vingi sana bila ya wenyewe kujijua mkuu.
 
Nilichoandika sio mawazo,ni kitu kipo...mimi ni wa kike,nina marafiki wa kike wenye hizo tabia na wananipa hiyo sababu

Ninae rafiki hakubali salamu ya mwanaume asiye na gari
Kwake yeye mwanaume mwenye gari ndio mwenye haki ya kuongea nae
Uyo rafiki yako ni mshamba sana ..unaweza kua msomi lakini still ukawa na ushamba
 
Mtu mwenye muonekano wa hovyo anafananaje!ni tabia za dharau kutoitika salamu ya mtu usiyemjua au kwa sababu siyo nadhifu,wakati mwengine anataka kukufahamisha uelekeo unaoelekea kwa muda huo siyo kuzuri rudi au labda umedondosha kitu.

Dunia hii siyo ya kuishi kwa maringo unapojiona wewe mzuri kuna sehemu ukiingia wanakuona kinyago tu ila huwa wanakusikiliza kwa sababu ni binadamu mwenzao!

You nailed it kiongozi...!

Watu wana dharau za ajabu sana bila ya kujua huyo anayekusalimia anaweza akakusaidia kwa njia moja au nyingine.
 
Ni mwehu pekee ana kataa salamu

Thanks Nuzulati mi nafkiri hii pia inachangiwa na malezi huko walipolelewa walipewa malezi ya hovyo utakuta.

Coz ukishapewa malezi yalo mazuri toka udogoni unakua ukiwa na tabia njema kwa yeyote utakayekutana nae, ila kama malezi ni ya hovyo basi hata tabia nayo inakuwa ni ya hovyo kabisa.
 
Nilichoandika sio mawazo,ni kitu kipo...mimi ni wa kike,nina marafiki wa kike wenye hizo tabia na wananipa hiyo sababu

Ninae rafiki hakubali salamu ya mwanaume asiye na gari
Kwake yeye mwanaume mwenye gari ndio mwenye haki ya kuongea nae
Huyo rafiki yako ana dalili mojawapo za ugonjwa wa akili. Mpelekeni kwa mtaalamu wa magonjwa ya akili kabla hamjachelewa!
 
Back
Top Bottom