Niache Nteseke
JF-Expert Member
- Apr 29, 2020
- 1,959
- 2,177
Salaam/Shalom.
Kuna hili suala huwa linanishangaza sana, utakuta unamsalimia mtu halafu matokeo yake huyo unayemsalimia utakuta anakuangalia tu.
Huwa najiuliza sana hili swali, hivi mkijibu salaam huwa mnapungukiwa na kitu gani dada zangu...?
Leo nilikuwa Mount Meru Hospital kwa ajili ya kupima COVID 19 coz kuna kasafari kidogo cha nje, basi nikasema hebu ngoja nitoke nje ya geti nikanunue maji ya kunywa then nirudi ndani na muda wa kuona wagonjwa ulikuwa umeshaisha na askari akawa anazuia watu wasiingie.
Basi wakati natoka nje nikapishana na mdada mmoja mweupeeee anaingia ndani kumuona mgonjwa wake, nikamsalimia yule dada akawa ananiangalia tu, basi nikapishana nae nikanunua maji nikawa narudi ndani.
Nafika getini nikamkuta yule mdada amezuiwa kuingia ndani kwa kuwa muda wa kuona wagonjwa ulishaisha, basi nilivyofika getini askari akaniambia MKUU INGIA INGIA nikapita zangu nikamuacha yule mdada anamsihi, anambembeleza na kumuomba sana askari wa getini amruhusu aingie ndani kumuona mgonjwa wake, lakini bila ya mafanikio hakuweza kuingia ndani.
Ningeweza kumwambia tu askari MRUHUSU AINGIE na askari asingeuliza mara 2, ila unaanzaje kumuombea msaada mtu ambaye hata salaam yako ameshindwa kujibu akabaki anakuangalia tu...?
Matokeo yake ikabidi arudi nyumbani kama alivyokuja. Hivi, mnaposalimiwa then mkajibu salaam huwa mnapungukiwa na kitu gani dada zangu...?
Badilikeni aisee sio kila salaam ina ubaya ndani yake salaam nyingine zina baraka ndani yake, hivyo msiwe wenye kujikosesha baraka wenyewe kwa kushindwa kujibu kitu kidogo tu dada zangu. SALAAM.
NAWASILISHA.
Kuna hili suala huwa linanishangaza sana, utakuta unamsalimia mtu halafu matokeo yake huyo unayemsalimia utakuta anakuangalia tu.
Huwa najiuliza sana hili swali, hivi mkijibu salaam huwa mnapungukiwa na kitu gani dada zangu...?
Leo nilikuwa Mount Meru Hospital kwa ajili ya kupima COVID 19 coz kuna kasafari kidogo cha nje, basi nikasema hebu ngoja nitoke nje ya geti nikanunue maji ya kunywa then nirudi ndani na muda wa kuona wagonjwa ulikuwa umeshaisha na askari akawa anazuia watu wasiingie.
Basi wakati natoka nje nikapishana na mdada mmoja mweupeeee anaingia ndani kumuona mgonjwa wake, nikamsalimia yule dada akawa ananiangalia tu, basi nikapishana nae nikanunua maji nikawa narudi ndani.
Nafika getini nikamkuta yule mdada amezuiwa kuingia ndani kwa kuwa muda wa kuona wagonjwa ulishaisha, basi nilivyofika getini askari akaniambia MKUU INGIA INGIA nikapita zangu nikamuacha yule mdada anamsihi, anambembeleza na kumuomba sana askari wa getini amruhusu aingie ndani kumuona mgonjwa wake, lakini bila ya mafanikio hakuweza kuingia ndani.
Ningeweza kumwambia tu askari MRUHUSU AINGIE na askari asingeuliza mara 2, ila unaanzaje kumuombea msaada mtu ambaye hata salaam yako ameshindwa kujibu akabaki anakuangalia tu...?
Matokeo yake ikabidi arudi nyumbani kama alivyokuja. Hivi, mnaposalimiwa then mkajibu salaam huwa mnapungukiwa na kitu gani dada zangu...?
Badilikeni aisee sio kila salaam ina ubaya ndani yake salaam nyingine zina baraka ndani yake, hivyo msiwe wenye kujikosesha baraka wenyewe kwa kushindwa kujibu kitu kidogo tu dada zangu. SALAAM.
NAWASILISHA.