Moja kwa Moja bila hata salamu.
Niko kwenye mchakato wa kuanza kujenga ka kibanda hapa downtown kwa Bashite.
Sasa kama mjuavyo lazima uwe na ramani ya unachotaka kujenga. Nikaamua niende instagram kucheki baadhi ya wadau wanaochora ramani.
Nikafanya utafiti wa gharama. Cha ajabu kwenye page hawaweki gharama za kuchora wala gharama roughly za kujenga nyumba.
Nikamtext mmoja kumuuliza gharama ya baadhi ya ramani ambazo amepost (ni zile za kawaida vyumba vitatu) ananiambia 600,000 pomoja na makadirio ya gharama 800,000. Ikumbukwe hii anayo na ameshaichora ni suala la kuiuza.
Nikaamua kusepa. Nikaenda kwa mwingine kasema 700,000/= nikamfuata mwingine kaniambia 550,000.
Swali: Hivi njie jamaa mnafikiri sisi tunaokota hela au hamuwezi hata soma status ya wateja wenu (purchasing Power).
Natambua kazi mnayoifanya ila jaribuni kuregeza bei. Mimi mshahara 250,000 take home. So mnataka nikusanye miezi mitatu bila kula nije kununua ramani kweli.
Nilitegemegea ukiwa na ramani mtu akiitaka unamsukumia hata kwa 50,000 maisha yanaendelea.
Anyway sina maneno mengi sana. Sasa nafikiri napita mtaani nikiona mtu ananyumba nzuri nitaenda kumuomba ramani nyie zenu kaeni nazo.
MREJESHO: Kuna mdau kanipa ramani full 2 (Nichague kama zitanifaa) ambazo yeye alijenga na amekubali kunipigia mihuri kwa 50 then nikafuatilie vibali Halmashauri. Actually ni ramani ziko very clear kuliko hata zile za malofa wa 700k.