Wachora ramani za nyumba mna shida gani?

Wachora ramani za nyumba mna shida gani?

Nani aliyekudanga architect hajui load analysis,Eti naweza kuchora cantilever then ikafeli ,hivi unadhani maarchitect tunachora tu Kama tunabahatisha ?? Au unadhani miaka mitano tunayokomaa hatuelewi chochote kuhusu structure??
Tuanziee Hapa mzee.. Nadhani ni Mwaka wa kwanza.. Kuna somo linaitwa Statics Architects wanasoma hili? Dynamics architects wanasoma? Mwaka wa Pili kuna Determinate/Indeterminate Structures Architects wanasoma? Mwaka wa Tatu kuna RC design Architects wanasoma?

na kama hawasomi hizo Load analysis wanazijua vipi? we Jamaa unachekesha!
 
600,000 ramani? Aisee sio mimi mkuu. Never sifanyi huo ulofa

Basi blaza kachore tu ya kwako mwenyewe, yaani utajifanyia buuree kabisa wala hata kumi usijilipe. Unasumbuka nini sijui.. ☹️☹️
 
Tuanziee Hapa mzee.. Nadhani ni Mwaka wa kwanza.. Kuna somo linaitwa Statics Architects wanasoma hili? Dynamics architects wanasoma? Mwaka wa Pili kuna Determinate/Indeterminate Structures Architects wanasoma? Mwaka wa Tatu kuna RC design Architects wanasoma?

na kama hawasomi hizo Load analysis wanazijua vipi? we Jamaa unachekesha!
Ngoja nikuulize swali dogo Sana
Unajua ni kwanini leo nikiamua kwenda kusomea masters ya civil engineer ninaqualify Moja kwa moja na bachelor yangu ya architecture ,lakini wewe mwenye bachelor ya civil engineer huruhusiwi hata kidogo kwenda kuchukua masters ya architecture duniani kote hata ungekua na GPA ya Tano.
Pili kwanini architect ndio kiongozi kwenye ujenzi na sio Engineer Wala Qs

Ukijibu hayo tunaweza kwenda sawa
 
Moja kwa Moja bila hata salamu.

Niko kwenye mchakato wa kuanza kujenga ka kibanda hapa downtown kwa Bashite.

Sasa kama mjuavyo lazima uwe na ramani ya unachotaka kujenga. Nikaamua niende instagram kucheki baadhi ya wadau wanaochora ramani.

Nikafanya utafiti wa gharama. Cha ajabu kwenye page hawaweki gharama za kuchora wala gharama roughly za kujenga nyumba.

Nikamtext mmoja kumuuliza gharama ya baadhi ya ramani ambazo amepost (ni zile za kawaida vyumba vitatu) ananiambia 600,000 pomoja na makadirio ya gharama 800,000. Ikumbukwe hii anayo na ameshaichora ni suala la kuiuza.

Nikaamua kusepa. Nikaenda kwa mwingine kasema 700,000/= nikamfuata mwingine kaniambia 550,000.

Swali: Hivi njie jamaa mnafikiri sisi tunaokota hela au hamuwezi hata soma status ya wateja wenu (purchasing Power).

Natambua kazi mnayoifanya ila jaribuni kuregeza bei. Mimi mshahara 250,000 take home. So mnataka nikusanye miezi mitatu bila kula nije kununua ramani kweli.

Nilitegemegea ukiwa na ramani mtu akiitaka unamsukumia hata kwa 50,000 maisha yanaendelea.

Anyway sina maneno mengi sana. Sasa nafikiri napita mtaani nikiona mtu ananyumba nzuri nitaenda kumuomba ramani nyie zenu kaeni nazo.
Ile ni taaluma, watu wamesomea kama mshahara mdogo endelea kuishi kwa mama mwenye nyumba
 
Kuna jamaaa yupo stendi ya gerezani kariakoo ni chinga kaeka hadi mic anatangaza ana ramani za nyumba balaaaa afu anauza alfu 20 hadi 30.Ni we kukaa na kuanza kuchaguwa tu
 
Mkuu nina mpango wa kujenga Banda la ngombe kwa matofali je nahitaji kibali ??

Ha ha ha, Sheria itakutaka utengeneze ramani tena, na kuijumuisha hilo banda la ng'ombe kisha wakupe idhini.. Maana kubwa ya kupata kuomba na kupewa kibali ni kuhakikisha unachofanya kinaenda na mazingira na taratibu ya sehem hiyo, bila ya kuwakera wengine.. Na ndo maana wanaweza kukataa kukupa kibali pindi wanapoona unachotaka kujenga hapo either hakiendani na mazingira ya hapo, au kitahatarisha usalama, au kuwa kero hapo..
 
Archicard ni rahisi mno. Ingia youtube jipige pindi mwenyewe uanze kuchora.
Baada ya mwezi tu utaweza kuchora ramani yako mwenyewe.
Hawa wanaokuchorea mtaani uku ni madogo tu wa diploma au degree koz mbalimbali wenye idea tu za archicard hakuna proffesionalism kiviile kwenye raman ya nyumba ndogo
 
Labda tumpe ramani ya lipumba alipovuja jasho ikulu[emoji23][emoji23]
 
Moja kwa Moja bila hata salamu.

Niko kwenye mchakato wa kuanza kujenga ka kibanda hapa downtown kwa Bashite.

Sasa kama mjuavyo lazima uwe na ramani ya unachotaka kujenga. Nikaamua niende instagram kucheki baadhi ya wadau wanaochora ramani.

Nikafanya utafiti wa gharama. Cha ajabu kwenye page hawaweki gharama za kuchora wala gharama roughly za kujenga nyumba.

Nikamtext mmoja kumuuliza gharama ya baadhi ya ramani ambazo amepost (ni zile za kawaida vyumba vitatu) ananiambia 600,000 pomoja na makadirio ya gharama 800,000. Ikumbukwe hii anayo na ameshaichora ni suala la kuiuza.

Nikaamua kusepa. Nikaenda kwa mwingine kasema 700,000/= nikamfuata mwingine kaniambia 550,000.

Swali: Hivi njie jamaa mnafikiri sisi tunaokota hela au hamuwezi hata soma status ya wateja wenu (purchasing Power).

Natambua kazi mnayoifanya ila jaribuni kuregeza bei. Mimi mshahara 250,000 take home. So mnataka nikusanye miezi mitatu bila kula nije kununua ramani kweli.

Nilitegemegea ukiwa na ramani mtu akiitaka unamsukumia hata kwa 50,000 maisha yanaendelea.

Anyway sina maneno mengi sana. Sasa nafikiri napita mtaani nikiona mtu ananyumba nzuri nitaenda kumuomba ramani nyie zenu kaeni nazo.
Ulimchangia ada ya Shule? kutokuwa na Hela ww kwanini iwe tabu kwenye fani za watu kwani lazima kujenga kwa kuchora Ramani kama huna hela inatakiwa ramani uwe mwenyewe site fundi ajenge kutokana na maelezo yako
 
Tuanziee Hapa mzee.. Nadhani ni Mwaka wa kwanza.. Kuna somo linaitwa Statics Architects wanasoma hili? Dynamics architects wanasoma? Mwaka wa Pili kuna Determinate/Indeterminate Structures Architects wanasoma? Mwaka wa Tatu kuna RC design Architects wanasoma?

na kama hawasomi hizo Load analysis wanazijua vipi? we Jamaa unachekesha!
Huyo jamaa architect ameniacha hoi Sasa kama structural analysis anafanya,kwa nini structural drawings wapewe wengine architect asimalize? Anazingua huyo jamaa michoro yote ikiwemo ya architects au structural inaweza badilika kulingana na nature ya site ndio maana kuna site instructions,management site meetings etc
 
Watu wana tamaa aise, eti field ya watu mbona wengine tuko kweny field za kutumia akili balaa but no easy money! Kazi ya 1million ni umeenyeka nayo almost 1 week..na unaimaliza akili imechoka balaa, kuchora ramani kazi ya masaa matatu au chini ya hapo upewe laki 6 hahaha..
 
Ulimchangia ada ya Shule? kutokuwa na Hela ww kwanini iwe tabu kwenye fani za watu kwani lazima kujenga kwa kuchora Ramani kama huna hela inatakiwa ramani uwe mwenyewe site fundi ajenge kutokana na maelezo yako
Ndo mentality mlionayo. Things doesn't work that way. Kuweni flexible to respond to labour market demand. Sasa kama wewe ulisoma uliambiwa mshahara mil 3 kwa mwezi ila uhalisia ni 1m. Nenda kafanye tu ndio nguvu ya soko hio.
 
Watu wana tamaa aise, eti field ya watu mbona wengine tuko kweny field za kutumia akili balaa but no easy money! Kazi ya 1million ni umeenyeka nayo almost 1 week..na unaimaliza akili imechoka balaa, kuchora ramani kazi ya masaa matatu au chini ya hapo upewe laki 6 hahaha..
Ndo mana nasema jamaa hawatumii akili. Kwa mtaalamu siku moja unaweza chora ramani ikaisha halafu unataka 600k unaishia kupata 0
 
Back
Top Bottom