Wachezaji wetu kucheza ligi moja na Pacome, Mpanzu, Diara ni bahati kwao, tumieni ujuzi wao kushinda CHAN.

Wachezaji wetu kucheza ligi moja na Pacome, Mpanzu, Diara ni bahati kwao, tumieni ujuzi wao kushinda CHAN.

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,247
Reaction score
16,169
Kuna uzoefu ambao wachezaji wetu wa ndani wangeweza kukutana nao kwa timu zetu kualika timu za kigeni au kushiriki mashindano ya CAF, lakini wachezaji wetu waishukuru TFF kuruhusu na timu zetu kusajili wachezaji wenye viwango vikubwa sana kama Pacome, Mpanzu, Diara, Camara, Aziz Ki, Sowah, Sila, Kipre, Mayele, nk kucheza nao kwenye timu au ligi moja. Hii ina maana kuwa wachezaji wetu ni kama vile wamepata mechi za kigeni karibu msimu mzima. Hivyo, wachezaji wetu hawana sababu ya kushindwa kutumia uzoefu wanaoupata kutoka kwachezaji wageni hawa kubeba kombe la mashindano ya CHAN mwaka huu.

Wenzetu wanacheza wachezaji wa ndani lakini sisi ni kama vile tunachezesha timu yenye hadi wachezaji wanaocheza mataifa ya kigeni. Hatutakuwa na kisingizio cha kushindwa kuubeba ubingwa wa CHAN.
 
Sawa sawa
Wachezaji wetu ambao walistahili kwenda kucheza nje ya nchi wako hapa kwa msaada wa kubakizwa kwa fedha nyingi na timu za Yanga, singida, Simba na Azam, hivyo kuwa na sifa ya kucheza CHAN. Wachezaji Hawa akina FEI, Dickson, mzize, muda, msindo, nado, kapombe, tshabalala, chikola, nk hawana excuses.
 
Mzize mtoe hapo mzito sana,hajui kujiongeza. Angetemwa mapema mno
Wachezaji wetu ambao walistahili kwenda kucheza nje ya nchi wako hapa kwa msaada wa kubakizwa kwa fedha nyingi na timu za Yanga, singida, Simba na Azam, hivyo kuwa na sifa ya kucheza CHAN. Wachezaji Hawa akina FEI, Dickson, mzize, muda, msindo, nado, kapombe, tshabalala, chikola, nk hawana excuses.
 
Mzize mtoe hapo mzito sana,hajui kujiongeza. Angetemwa mapema mno
Ana magoli mangapi kwenye ligi? Shida ni anaocheza nao.

Messi walimuuliza swali kuwa kwanini ukiwa Barcelona unafunga magoli mengi kuliko ukiwa timu ya taifa Argentina. Akajibu "acha kuifananisha Barcelona na Argentina" inamtegemea unazunguukwa na akina nani
 
Back
Top Bottom